-
Baqaei: Marekani inapasa kudhamini ushiriki wa timu ya taifa ya Iran katika mashindano ya Kombe la Dunia
May 26, 2026 02:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amezungumzia uvumi unaoendelea kuhusu kushiriki wa timu ya taifa ya kandanda ya Iran katika Kombe la Dunia la FIFA la 2026, na kusisitiza kuwa Marekani inawajibika kuandaa mazingira yanayofaa kwa timu hiyo kushiriki katika mashindano bila vizuizi vyovyote.
-
Arsenal yatwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya Man City kulazimishwa sare na FC Bournemouth
May 20, 2026 03:56Hatimaye baada ya miaka 22 ya ukame, Arsenal au ukipenda waite The Gunners wametwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu wa 2025-26 baada ya Man City kulazimishwa sare ya bao moja kwa moja na The Cherries ambao nao walikuwa wanafukuzia angalau alama moja ili wafaulu kushiriki kombe la Uefa Conference Cup msimu ujao.
-
Waziri Mkuu wa Uhispania ampongeza Lamine Yamal kwa kusherehekea ubingwa na bendera ya Palestina
May 14, 2026 03:29Waziri Mkuu wa Uhispania, Pedro Sanchez, amesisitiza uungaji mkono wa nchi yake kwa haki ya Wapalestina ya kuanzisha nchi yao wenyewe, akitoa maoni yake kuhusu utata uliosababishwa na hatua ya nyoka wa timu ya soka ya Barcelona, Lamine Yamal, wakati timu yake ilipokuwa ikisherehekea taji la ubingwa wa ligi ya Uhispania.
-
Mkuu wa Shirikisho la Soka Iran akataa simu ya Waziri Mkuu wa Canada baada ya kutendewa vibaya
May 04, 2026 10:19Mkuu wa Shirikisho la Soka la Iran, Mehdi Taj, amekataa ombi la maafisa wa Canada la kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mark Carney baada ya wajumbe wa Iran kuvunjiwa heshima na maafisa wa mpaka wa Canada.
-
Iran yasema haitashiriki Kombe la Dunia la FIFA 2026
Mar 12, 2026 02:57Waziri wa Michezo wa Iran, Ahmad Donyamali amesema timu ya taifa ya soka ya Jamhuri ya Kiislamu haitashiriki katika fainali za Kombe la Dunia katika msimu ujao wa joto, licha ya Rais wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA, Gianni Infantino kusisitiza kuwa amehakikishiwa na Rais Donald Trump wa Marekani kwamba Iran inakaribishwa kushiriki mashindano hayo makubwa zaidi ya soka duniani, pamoja na vita vinavyoendelea.
-
Ulimwengu wa Spoti, Dec 29
Dec 29, 2025 03:34Hujambo mpenzi mskilizaji na hususan mfuatiliaji wa matukio ya spoti na karibu katika kipindi chetu cha mwisho mwaka huu 2025, tuangazie baadhi ya matukio muhimu ya michezo yaliyoshuhudiwa ndani ya siku saba zilizopita katika pembe mbali mbali za dunia ikiwemo michuano ya AFCON inayoendelea kurindima nchini Morocco.
-
UWW: Muirani Amouzad ndiye mwanamieleka 'Aliyetamalaki Zaidi' duniani 2025
Dec 25, 2025 02:12Muungano wa Mieleka Duniani (UWW) umemtaja Rahman Amouzad kutoka Iran kuwa mwanamieleka wa mtindo wa freestyle (kujiachia) "Aliyeng'ara Zaidi" kwa mwaka huu 2025.
-
Unyanyuaji Uzani; Muirani avunja rekodi ya dunia, ashinda dhahabu Misri
Oct 17, 2025 03:20Ali Akbar Gharibshahi, bingwa wa mchezo wa kunyanyua vitu vizito wa Iran ameweka rekodi mpya ya dunia na kushinda medali ya dhahabu katika kategoria ya kilo wanamichezo wenye 107, kwenye Mashindano ya Dunia ya Kunyanyua Uzani ya 2025 nchini Misri.
-
Timu ya voliboli ya wanawake ya Iran yatwaa ubingwa wa CAVA 2025
Oct 06, 2025 01:49Timu ya voliboli ya wanawake ya Iran iliigaraza Uzbekistan kwenye mashindano ya Kombe la Chalenji ya Wanawake wa Asia ya Kati (CAVA) jana Jumapili na kushinda taji hilo la kieneo kwa mara ya kwanza katika historia.
-
Ulimwengu wa Spoti, Okt 6
Oct 06, 2025 07:43Hujambo mpenzi msikilizaji na karibu tuangazie baadhi ya matukio muhimu ya spoti yaliyojiri ndani ya siku saba zilizopita katika pembe mbali mbali za dunia.