-
Serikali ya Misri yamuweka mpinzani wa al Sisi katika orodha ya magaidi!
Feb 20, 2018 23:42Serikali ya Misri imemuweka kiongozi wa chama cha upinzani cha "Misri Imara" na wanachama wengine 15 wa chama hicho katika orodha ya magaidi.
-
Ethiopia yaakhirisha mkutano wake na Misri kuhusu bwawa la al-Nahdha
Feb 18, 2018 23:33Misri imekubali ombi la Ethiopia la kuakhirisha mkutano wa pande mbili wa kujadili suala tata la bwawa la al-Nahdha linalojengwa na Uhabeshi, baada ya Adiss Ababa kutangaza sheria ya hali ya hatari.
-
Jeshi la Misri laua magaidi 7 wakufurishaji na kukamata wengine 408
Feb 17, 2018 23:44Jeshi la Misri limetangaza kuwaaangamiza magaidi saba wakufurishaji katika oparesheni maalumu ya kijeshi inayoendelea katika eneo la Sinai nchini humo.
-
Misri yaonya kuhusu hatari ya magaidi wa Daesh kuvamia kaskazini mwa Afrika
Feb 17, 2018 00:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri ameonya kuwa magaidi wa Daesh (ISIS) waliosafishwa huko Syria na Iraq wanafanya kila wawezalo kuzivamia nchi za kaskazini mwa Afrika hususan Libya.
-
Amnesty International yakosoa oparesheni za jeshi la Misri huko Sinai
Feb 15, 2018 12:25Shirika la Msamaha Duniani (Amnesty International) limesema kuwa Misri ni lazima iache kutumia mabomu ya vishada haraka iwezekanavyo baada ya jeshi la nchi hiyo kutoa mkanda rasmi wa video unaoonyesha silaha waliozotumia katika oparesheni za hivi karibuni huko Sinai ya Kaskazini.
-
Kuendelea radiamali ya mashirika ya haki za binadamu kuhusiana na udikteta wa uchaguzi nchini Misri
Feb 14, 2018 09:06Katika radiamali ya hivi karibuni kabisa ya mashirika ya kimataifa kuhusiana na mchakato wa uchaguzi wa Rais nchini Misri, asasi na juumuiya kadhaa za haki za binadamu likiwemo Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch na waandishi wa habari wasio na mipaka zimetangaza kuwa, uchaguzi huo hauna hata vigezo vya chini kabisa vya kufanyika zoezi la upigaji kura katika mazingira ya wazi na huru.
-
Mashirika ya kutetea haki yautaja uchaguzi ujao wa Misri kama kichekesho
Feb 13, 2018 23:51Mashirika 14 ya kieneo na kimataifa ya kutetea haki za binadamu yameutaja uchaguzi ujao wa rais nchini Misri kama mchezo wa kuigiza.
-
Safari ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani nchini Misri
Feb 12, 2018 23:27Rex W. Tillerson, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani akiwa katika safari yake ya kiduru katika kuzitembelea nchi za eneo, aliwasili jana mjini Cairo, mji mkuu wa Misri.
-
Jeshi la Misri laua magaidi 12 katika Rasi ya Sinai
Feb 12, 2018 04:18Jeshi la Misri limesema kuwa limeua magaidi wasiopungua 12 na kuwatia mbaroni wengine wapatao 100 katika opereseheni kubwa iliyoanzishwa na jeshi hilo kaskazini mwa Rasi ya Sinai.
-
Wanachama wengine kadhaa wa Ikhwanul Muslimin wahukumiwa kifungo cha maisha jela Misri
Feb 12, 2018 01:06Wanachama kadhaa wa harakati ya Kiislamu ya Ikhwanul Muslimin ya Misri wamehukumiwa kifungo cha maisha jela na mahakama ya nchi hiyo.