-
Makamanda 23 wanaomuunga mkono Anan watiwa mbaroni Misri
Feb 03, 2018 04:18Idaya ya usalama nchini Misri imewatia mbaroni makamanda 23 miongoni mwa wafuasi wa Sami Hafez Anan, mkuu wa zamani wa majeshi nchini humo ambaye alitangaza azma yake ya kutaka kugombea uchaguzi wa rais wa nchi hiyo.
-
Misri yawahukumu maisha jela wanachama wa Ikhwani
Jan 30, 2018 23:52Katika kile kinachoonekana na mwendelezo wa hukumu za kidhalimu dhidi ya wafuasi wa harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri, Mahakama ya Jinai ya Cairo imewahukumu kifungo cha maisha jela wanachama sita wa harakati hiyo.
-
Wanasiasa Misri kususia uchaguzi wa rais
Jan 30, 2018 13:06Makumi ya wanaharakati wa kisiasa wa Misri wametia saini taarifa ya kususia uchaguzi ujao wa rais nchini humo wakisema kuwa, hautakuwa na sifa za awali kabisa za uchaguzi huru na wa haki.
-
Misri yapokea vyema kuboreka uhusiano wa Ethiopia na Sudan
Jan 29, 2018 11:43Rais Abdel Fattah el Sisi wa Misri amesema nchi yake imefurahishwa na kuboreka uhusiano baina ya Sudan na Ethiopia katika nyuga tofauti.
-
Wanasiasa Misri watoa wito wa kususiwa uchaguzi wa rais
Jan 29, 2018 02:42Wanasiasa wa kambi ya upinzani nchini Misri wamewataka wananchi wa nchi hiyo kususia uchaguzi ujao wa rais.
-
Mpinzani wa el Sisi katika uchaguzi ujao wa Misri atupwa katika jela ya kijeshi
Jan 28, 2018 11:41Wakili wa mkuu wa zamani wa jeshi la Misri ambaye ametangaza kuchuana na Rais Abdul Fattah el Sisi katika uchaguzi ujao wa rais nchini humo amesema kuwa, mteja wake emepelekwa katika jela ya kijeshi.
-
Ikhwanul Muslimin ya Misri yatahadharisha kuhusu kuwekewa mashinikizo wapinzani
Jan 26, 2018 13:12Harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri imetahadharisha kuhusu hatua ya serikali ya nchi hiyo inayoongozwa na Rais Abdel Fatah al Sisi ya kuwashinikiza wapinzani wa serikali na taathira zake mbaya za kisiasa.
-
Al-Sisi asafishiwa njia kutetea kiti cha urais baada ya wapinzani wake kutiwa mbaroni au kujitoa
Jan 25, 2018 03:58Mpinzani wa Rais Abdel Fattah al-Sisi wa Misri katika kinyang'anyiro cha uchaguzi ujao wa Rais ametangaza kujitoa katika mbio hizo hatua ambayo inamsafishia njia Rais wa sasa wa nchi hiyo kutetea kiti chake.
-
Ethiopia yakataa upatanishi wa Benki ya Dunia katika mgogoro wake na Misri
Jan 22, 2018 22:59Waziri Mkuu wa Ethiopia amekataa pendekezo la Misri la kuitaka Benki ya Dunia kuwa mpatanishi katika mgogoro wa ujenzi wa bwawa unaofanywa na serikali ya Addis Ababa juu ya Mto Nile.
-
Al Sisi kuwania urais wa Misri kwa muhula wa pili katika uchaguzi wa Machi
Jan 20, 2018 03:42Rais Abdel Fattah al-Sisi wa Misri ametangaza kuwa atawania muhula wa pili wa urais katika uchaguzi wa mwezi Machi ambapo anatazamiwa kushinda.