-
Albanese: Vikwazo dhidi yangu si lolote kulinganisha na masaibu wanayopitia Wapalestina
Aug 06, 2025 12:41Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika ardhi za Palestina amepuuzilia mbali vikwazo vilivyowekwa hivi karibuni na Marekani kutokana na msimamo wake wa kuukosoa utawala wa Israel, akisema kuwa vikwazo hivyo si lolote si chochte ikilinganisha na masaibu wanayoyastahamili na kupitia raia wa Palestina katika ardhi yao.
-
Rais wa Ireland aitaka UN kutumia sura ya 7 ya Mkataba wa umoja huo kuhitimisha mgogoro wa Gaza
Aug 05, 2025 14:31Rais Michael Daniel Higgins wa Ireland ameutaka Umoja wa Mataifa kutumia utaratibu wa Sura ya 7 ya Mkataba wa umoja huo dhidi ya Israel ili kukomesha mauaji ya kimbari yanayoendelea dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Kwa nini majimbo ya Marekani yanaadhibiwa kwa sababu ya kuitetea Palestina?
Aug 05, 2025 14:24Rais wa Marekani, Donald Trump, ametishia kukata bajeti ya dharura ya kukabiliana na majanga ya asili na kudhamini usalama wa ndani wa majimbo na miji ya Marekani inayounga mkono Palestina na kususia makampuni ya Israel.
-
Australia: Palestina itatoweka kama mauaji ya kimbari ya Israel yataendelea
Aug 05, 2025 14:12Penny Wong, Waziri wa Mambo ya Nje wa Australia amesema kuwa kuna hatari kwamba hakutakuwa na Palestina inayoweza kutambuliwa iwapo mauaji ya kimbari ya Israel yataendelea katika Ukanda wa Gaza sambamba na kuongezeka vitendo vya mabavu dhidi ya Wapalestina wa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Albanese: Magharibi haiwi na uwezo wowote wa kutekeleza sheria za kimataifa inapohusu Israel
Aug 03, 2025 05:41Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa wa hali ya haki za binadamu katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu amesema, nchi za Magharibi haziwi na uwezo wowote wa kutekeleza sheria za kimataifa inapohusu utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Ujumbe wa Kongamano la Kimataifa la Palestina kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
Aug 01, 2025 15:03Mkutano wa Kimataifa wa Palestina umeafiki kuchukua hatua za pamoja za kumaliza vita vya Israel dhidi ya watuu wa Gaza, na kuunga mkono kile kilichoitwa kuwa suluhisho la "nchi mbili" na kuanzishwa kwa taifa la Palestina.
-
Mmarekani aliyemuua mtoto wa Kipalestina afariki dunia gerezani
Jul 29, 2025 02:41Mwenye nyumba huko Illinois aliyepatikana na hatia ya kumuua mtoto wa mpangaji wake Mmarekani mwenye asili ya Palestina amefariki dunia akiwa kizuizini.
-
HAMAS yakabidhi mapendekezo yake kuhusu makubaliano ya kusitisha vita Ghaza
Jul 24, 2025 06:52Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema katika taarifa iliyotoa mapema leo kwamba "imewasilisha majibu yake na yale ya makundi ya Wapalestina" kwa wapatanishi baada ya majuma kadhaa ya mazungumzo ya kusitisha mapigano yaliyoshindwa kuzaa matunda.
-
Brazil yajiunga katika kesi ya ICJ dhidi ya mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel Ghaza
Jul 24, 2025 06:48Wizara ya Mambo ya Nje ya Brazili imetangaza kuwa iko katika "hatua za mwisho" za kuwasilisha mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ uamuzi wa kujiunga na kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel kwa kuhusika na mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Ghaza.
-
Kwa nini Marekani imejiondoa rasmi UNESCO?
Jul 23, 2025 08:58Marekani ilitangaza Jumanne, Julai 22, kwamba imejiondoa rasmi katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO.