-
OIC: Baitul Muqaddas (Jerusalem) ni mji mkuu wa Palestina
Aug 22, 2019 07:41Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imesisitiza kuwa: Baitul Muqaddas utabakia daima kuwa mji mkuu wa Palestina.
-
Wabunge Waislamu wa Marekani watamka hadharani kuwa iko siku ya karibu wataizuru Palestina ikiwa huru
Aug 18, 2019 22:13Wabunge wawili Waislamu katika Kongresi ya Marekani, ambao wamezuiwa kutembelea ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu wametangaza hadharani kuwa, iko siku ya karibu mno, wataitembelea Palestina ikiwa huru.
-
Utawala wa Kizayuni unashirikiana na Trump katika hatua dhidi ya wabunge Waislamu katika Kongresi ya Marekani
Aug 17, 2019 03:20Wizara ya Mambo ya Nje ya Utawala wa Kizayuni wa Israel imetangaza kuwa haitawaruhusu wajumbe wawili wa Bunge la Marekani, Kongresi, kuingia katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Walowezi wa Kiyahudi wavamia Msikiti wa al Aqsa mara tatu siku ya Idi, wajeruhi makumi ya Waislamu
Aug 11, 2019 22:14Walowezii zaidi ya 1700 wa Kiyahudi jana walivamia Msikiti wa al Aqsa mara tatu katika siku ya Idul Adh'ha na kuwajeruhi makumi ya Waislamu waliokwenda eneo hilo takatifu kwa ajili ya kufanya ibada.
-
Saeb Erakat: Mamlaka ya Ndani ya Palestina inafuatilia kuundwa nchi ya Palestina
Aug 05, 2019 03:45Katibu wa kamati ya utendaji ya Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) ametangaza kuwa, mkakati wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ni kuhitimishwa uvamizi na ukaliaji mabavu wa Wazayuni na kuundwa nchi ya Palestina.
-
Waziri Mkuu wa Palestina: Bila mfumo wa madola mawili, Israel itafikwa na kifo cha kidemografia
Jul 31, 2019 08:21Waziri Mkuu wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mohammad Shtayyeh amesema, utawala wa Kizayuni wa Israel utakabiliwa na "kifo cha kidemografia" ikiwa utakataa kuunga mkono suluhisho la kuwepo madola mawili, kwa ajili ya kutatua mgogoro wa miongo kadhaa baina yake na Wapalestina.
-
Russia yakosoa kitendo cha Marekani kukwamisha kupasishwa tamko la kulaani kubomolewa nyumba za Wapalestina
Jul 30, 2019 06:28Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imekitaja kitendo cha Marekani cha kuzuia kupasishwa taarifa inayolaani kubomolewa nyumba za raia wa Palestina katika mji wa Quds kuwa ni ishara nyingine ya upuuzaji wa Washington wa sheria za kimataifa.
-
Mufti wa Syria: Waislamu waungane katika suala la Palestina
Jul 29, 2019 22:27Mufti Mkuu wa Syria amewahimiza Waislamu washikamane na kuwa kitu kimoja dhidi ya njama zinazopikwa na maadui dhidi ya kadhia ya Palestina.
-
Baraza la Taifa la Palestina lamuunga mkono Mahmoud Abbas kwa kusitisha utekelezaji wa makubaliano na Israel
Jul 27, 2019 23:36Baraza la Taifa la Palestina limetangaza kuwa, kusitishwa utekelezaji wa hati za makubaliano yaliyofikiwa kati ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina na Israel ni mwanzo wa awamu mpya ya makabiliano ya pande zote na Wazayuni maghasibu.
-
Katibu Mkuu wa UN: Ubomoaji nyumba za Wapalestina si halali kisheria
Jul 26, 2019 02:56Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema, anatiwa wasiwasi na ubomoaji nyumba za Wapalestina unaofanywa na utawala wa Kizayuni na kusisitiza kuwa, sera za Israel za kuharibu na kuteketeza mali za Wapalestina haziendani na sheria za kimataifa.