-
Kuchapishwa ripoti rasmi ya serikali ya Biden kuhusu kuondoka Afghanistan
Apr 08, 2023 22:44Ikulu ya Rais wa Marekani (White House) Alhamisi iliyopita iliwasilisha ripoti yake rasmi kuhusu namna serikali ya Biden ilivyoondoka kwa madhila na fedheha huko Afghanistan. Ndani ya ripoti hiyo, serikali ya Trump imetajwa mara kwa mara kuwa ndio inayopaswa kulaumiwa kwa jinsi Marekani ilivyondoka huko Afghanistan katika hali ya mivutano.
-
Ombi la Ufaransa na Marekani kwa China kuitaka iwe msuluhishi katika vita vya Ukraine
Apr 07, 2023 04:49Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa siku ya Jumatano aliwasili Beijing kwa ziara ya siku tatu nchini China. Ziara hiyo ni ya kwanza kufanywa na Macron nchini China tangu mwaka 2019. Rais huyo wa Ufaransa jana alifanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Xi Jinping.
-
Kukiri Biden kuhusu kutenga serikali ya Marekani bajeti kwa ajili ya kuingilia masuala ya ndani ya nchi zingine
Apr 03, 2023 08:46Rais Joe Biden wa Marekani amesema kuwa, nchi hiyo imetenga bajeti ya mabilioni ya dola ambayo yatatumika katika masuala ambayo ameyataja kama “kuufanya mwenge wa uhuru uendelee kuwaka”.
-
Rais wa Chad awasamehe waasi 380 'waliomuua' babake
Mar 26, 2023 22:41Rais wa mpito wa Chad, Mahamat Idriss Deby ametangaza msahama kwa mamia ya waasi waliohukumiwa kifungo cha maisha jela hivi karibuni, kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya rais wa zamani wa Mali Idriss Deby Itno, ambaye ni baba ya rais huyo wa muda.
-
Rais Kagame atangaza msamaha kwa shujaa wa "Hotel Rwanda"
Mar 24, 2023 23:43Serikali ya Rwanda imemuachia huru Paul Rusesabagina, nyota wa filamu ya "Hotel Rwanda" aliyegeuka na kuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya Rais Paul Kagame wa nchi hiyo.
-
Undumakuwili wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kuhusu jinai za kivita
Mar 19, 2023 04:11Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, ambayo inajiona kuwa mahakama ya kwanza ya kudumu ya kimataifa inayoshughulikia uhalifu wa mauaji ya halaiki, jinai dhidi ya binadamu, jinai za kivita na uchokozi, Ijumaa iliyopita ilitoa waranti wa kimataifa wa kukamatwa Rais Vladmir Putin wa Russia.
-
Mazungumzo ya Biden na Scholz: Kuongezeka mashinikizo dhidi ya Russia na misaada ya silaha kwa Ukraine
Mar 06, 2023 06:41Kitengo cha upashaji habari cha Ikulu ya Marekani, White House siku ya Ijumaa kilitoa taarifa baada ya mazungumzo ya rais wa nchi hiyo Joe Biden na kansela wa Ujerumani Olaf Scholz kikisema kuwa, nchi hizo mbili zimejipanga kuendelea na siasa za vvikwazo dhidi ya Russia hadi muda wowote zitakaohisi unafaa.
-
Rais Samia wa Tanzania: Wapinzani si maadui wa taifa
Mar 05, 2023 09:07Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameendelea kuukumbatia upinzani na kusisitiza kuwa, wapinzani si maadui wa taifa, bali ni nguzo muhimu ya demokrasia ya nchi hiyo. Serikali ya mtangulizi wake hayati John Magufuli ilikuwa inatuhumiwa kuwawekea mbinyo wakosoaji na viongozi wa upinzani.
-
Rais Ruto: Kenya haitaruhusu ndoa za watu wenye jinsia moja
Mar 02, 2023 23:11Rais William Ruto wa Kenya amekosoa uamuzi wa Mahakama ya Juu ya nchi hiyo wa kuruhusu kusajiliwa makundi ya kulobi ya mashoga na wasagaji (LGBTQ) na kusisitiza kuwa, taifa hilo la Afrika Mashariki kamwe halitaruhusu ndoa za watu wenye jinsia moja.
-
Raisi: Shahidi Soleimani, IRGC mashujaa wa vita dhidi ya ugaidi
Feb 24, 2023 23:53Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amepongeza rekodi ya kuvutia ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) katika vita dhidi ya ugaidi na kusema kuwa, Luteni Jenerali Qassem Soleimani ni nembo na shujaa wa mapambano dhidi ya magenge ya kigaidi katika eneo la Asia Magharibi.