-
Kwa mara nyingine Russia yazionya nchi za Ulaya kuhusu misaada ya kijeshi kwa Ukraine
Sep 06, 2022 06:05Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia kwa mara nyingine tena imetoa onyo kali kwa Umoja wa Ulaya kuhusu madhara ya misaada yao ya kijeshi kwa Ukraine.
-
Russia yasisitiza kuhamishwa makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutoka New York
Sep 05, 2022 03:04Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imesisitiza kuwa Moscow inazingatia kikamilifu pendekezo la kuhamisha makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutoka Marekani hadi sehemu nyingine.
-
Russia yatishia tena kutumia silaha za nyuklia endapo uwepo wake utahatarishwa
Sep 04, 2022 06:33Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema upo uwezekano wa nchi hiyo kutumia silaha za nyuklia endapo uwepo wake utahatarishwa.
-
Mzozo mpya wa Russia na Magharibi kuhusu nishati
Sep 03, 2022 23:08Mawaziri wa fedha wa nchi saba zilizoendelea kiviwanda duniani, zinazojulikana kama G7, walikubaliana Ijumaa, Septemba 2, katika mkutano uliofanyika kwa njia ya video, kuweka mipaka ya bei kwa mauzo ya mafuta ya Russia.
-
Mazoezi makubwa ya kijeshi ya Russia, China, India; ishara ya kufeli Magharibi kuitenga Russia
Sep 02, 2022 23:56Licha ya shinikizo la Marekani kwa nchi nyingine kwa ajili ya kuitenga Russia kutokana na vita vya Ukraine, Moscow imeandaa mazoezi makubwa ya kijeshi ya nchi kavu, anga na baharini kwa kuzishirikisha nchi nyingine 13.
-
Kupamba moto vita vya nishati barani Ulaya
Sep 01, 2022 21:57Suala la kudhaminiwa mahitaji ya gesi kwa nchi za Ulaya sasa limekuwa tatizo sugu kwa nchi hizo. Nchi za Ulaya, ambazo ziliamua kuiwekea Russia vikwazo vya kila aina ili kuishinikiza katika vita vya Ukraine, sasa zinaituhumu Moscow kwamba inaitumia gesi kama silaha ya vita.
-
Russia: Ukraine imekiri kuwa na mpango wa kuunda bomu la atomiki
Aug 31, 2022 21:54Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema, serikali ya Ukraine imekiri kuwa na mpango wa kuunda bomu la atomiki na katu haijawahi kuficha kwamba ilikuwa ikijiandaa kwa ajili ya kukabiliana kijeshi na Russia.
-
Kifo cha Gorbachev na mafunzo ya kihistoria
Aug 31, 2022 05:56Mikhail Gorbachev, kiongozi wa mwisho wa Shirikisho la Sovieti, alifariki dunia Jumanne usiku akiwa na umri wa miaka 91 katika hospitali moja mjini Moscow baada ya kuugua kwa muda mrefu. Kifo cha Gorbachev kimekabiliwa na hisia nyingi za ndani na nje, ambapo Rais Vladimir Putin wa Russia, maafisa wa UN na Katibu Mkuu wake na wakuu kadhaa wa nchi, wametuma salamu za rambirambi.
-
Iran na Russia kujadili Ukraine na JCPOA mjini Moscow
Aug 30, 2022 23:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema lengo kuu la safari yake mjini Moscow ni kujaribu kutatua mgogoro wa Ukraine.
-
Russia: Mashambulizi dhidi ya Syria yamefichua undumakuwili wa Magharibi
Aug 30, 2022 21:52Balozi wa Russia katika Umoja wa Mataifa amelaani vikali mashambulio haramu ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Syria na kusisitiza kuwa, hujuma hizo zimefichua sura halisi ya Wamagharibi likija suala la haki za binadamu.