-
Mbunge wa Russia: Kambi za kijeshi karibu na bandari ya Odessa nchini Ukraine zilishambuliwa kwa mabomu
Jul 24, 2022 06:37Mbunge mmoja wa Russia amethibitisha kufanyika shambulio la anga kwenye viunga vya bandari ya Odessa nchini Ukraine na kuongeza kwamba ni vituo na kambi za kijeshi ndizo zililengwa katika shambulio hilo.
-
Waziri Mkuu wa Hungary: Vikwazo dhidi ya Russia vimefeli
Jul 24, 2022 03:03Waziri Mkuu wa Hungary amekiri kuwa vikwazo shadidi vya Wamagharibi dhidi ya Russia vimefeli na kugonga mwamba, na kusisitiza kwamba serikali za nchi za Ulaya zinaporomoka.
-
Kusainiwa mkataba wa mauzo ya nafaka kutoka Ukraine, mwanzo wa kutatua mgogoro wa chakula duniani
Jul 23, 2022 06:42Jana Ijumaa, Ukraine, Uturuki na Umoja wa Mataifa zilitia saini makubaliano ya kutatua mgogoro wa nafaka duniani. Mkataba huo ulitiwa saini kati ya Oleksandr Kubrakov, Waziri wa Miundombinu wa Ukraine, Kholusi Akar Waziri wa Ulinzi wa Uturuki, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na Waziri wa Ulinzi wa Russia Sergei Shoigu.
-
Mgogoro wa chakula ulimwenguni kupungua baada ya Russia, Ukraine kusaini mapatano ya nafaka
Jul 23, 2022 02:23Russia na Ukraine zimesaini mapatano pamoja na Umoja wa Mataifa na Uturuki kuhusu kuanza tena usafirishaji wa nafaka huku kukiwa na matumaini kuwa makubaliano hayo yatapunguza shida ya chakula ulimwenguni.
-
Russia yaanza ujenzi wa kituo cha kwanza cha nyuklia nchini Misri
Jul 22, 2022 03:21Shirika la Taifa la Nishati ya Nyuklia la Russia ROSATOM limeanza awamu ya kwanza ya ujenzi wa kituo cha kwanza cha nyuklia nchini Misri.
-
Russia yatishia kusimamisha uuzaji wa mafuta yake nje ya nchi
Jul 21, 2022 07:09Russia imetishia kuwa itaacha kuuza mafuta yake ghafi nje ya nchi hiyo iwapo nchi za Magharibi zitatekeleza mpango wao wa kuweka kibano katika bei ya mauzo ya bidhaa hiyo.
-
Mustakabali mwema katika Muungano wa China, Russia na Iran
Jul 21, 2022 03:10Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Russia amesema China, Russia na Iran zitaunda muungano mkubwa katika mustakabali wa dunia.
-
Rais wa zamani wa Russia aonya kuhusu 'Siku ya Kiyama'
Jul 18, 2022 03:06Rais wa zamani wa Russia ameionya vikali Ukraine na kusema kuwa, iwapo Kiev itathubutu kulishambulia eneo la Crimea, basi Kiyama kitawafikia wao pamoja na washirika wao kwa wakati mmoja.
-
Marandi: Makubaliano ya Marekani na Iran ni hatua erevu ya kuzuia mgogoro wa nishati
Jul 17, 2022 07:21Mohammad Marandi, mchambuzi mwandamizi wa masuala ya kisiasa na mitaala kuhusu Marekani amesema makubaliano kati ya Marekani na Iran ni hatua erevu ambayo kama itachukuliwa itazuia kutokea mgogoro wa nishati katika nchi za Magharibi.
-
Kuendelea mpambano wa Magharibi mkabala wa Russia; mara hii vikwazo vya dhahabu
Jul 16, 2022 23:25Nchi za Magharibi zinaendelea kustafidi na wenzo wa mashinikizo kwa Russia kupitia njia mbalimbali kama kuiwekea nchi hiyo vifurushi vya vikwazo vipya kufuatia hatua yake ya kuanzisha vita dhidi ya Ukraine; ambapo Umoja wa Ulaya umetangaza kuwa uuzaji nje wa dhahabu kutoka Russia utajumuishwa katika kalibu ya vikwazo vipya vya umoja huo.