-
Wanamuqawama wa Yemen wavurumisha makombora 4 ya Zilzal-1 kwenye ngome za askari wa Saudia
Jul 26, 2019 23:42Jeshi na kamati za wananchi nchini Yemen limevurumisha makombora manne aina ya Zilzal-1 kwenye ngome za vibaraka wa muungano vamizi wa Saudia katika mikoa ya Aseer na Najran kusini mwa Saudia.
-
Mshauri wa Amiri Jeshi Mkuu wa Iran atoa onyo kwa Marekani na Uingereza
Jul 24, 2019 13:25Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya ulinzi ametoa onyo kwa Uingereza kuhusiana na nia yake ya kujiingiza kwenye eneo la Lango Bahari la Hormuz na kwa Marekani kuhusu nia yake ya kutaka kuanzisha vita vya kijeshi na akaeleza kwamba: Kauli iliyotolewa na Saudi Arabia na Imarati kuhusu kuhitimishwa vita vya Yemen inadhihirisha kushindwa kwao katika vita hivyo.
-
2019, mwaka wa kunyongwa watu zaidi nchini Saudi Arabia
Jul 12, 2019 01:27Vyombo vya habari vimeripoti kuwa kesi za kunyongwa watu nchini Saudi Arabia zimeongezeka mara mbili katika nusu ya kwanza ya mwaka huu wa 2019.
-
Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa ataka Saudi Arabia iwekewe vikwazo, mauaji ya Khashoggi
Jul 03, 2019 08:27Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia jinai za mauaji ametaka Saudi Arabia iwekewe vikwazo kutokana na mauaji ya mwandishi habari mkosoaji wa utawala wa nchi hiyo.
-
Kwa nini Imarati imeamua kupunguza idadi ya wanajeshi wake huko Yemen?
Jun 29, 2019 23:46Baadhi ya duru za habari zimeripoti kuwa, Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) umepunguza idadi ya askari wake waliokuwa katika mji wa Aden huko kusini mwa Yemen.
-
Waziri Mkuu wa Palestina: Wapalestina wanataka uhuru na si sadaka
Jun 25, 2019 22:27Waziri Mkuu wa Palestina amesema kuwa mhandisi na mtayarishaji wa mpango wa Kimarekani wa eti amani ya Mashariki ya Kati wa Muamala wa Karne unaosimamiwa na mkwe wa Rais Donald Trump, Jared Kushner na wenzake hawaelewi kuwa Wapalestina hawataki sadaka bali wanadai haki zao za kuwa huru na kukomeshwa uvamizi wa Israel na udhibiti wa dola hilo haramu wa maisha na uchumi wao.
-
HRW: Saudi Arabia inapanga kumnyonga mtafiti Hassan al Maliki
Jun 24, 2019 00:53Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rigths Watch limetangaza kuwa utawala wa Saudi Arabia unakusudia kumhukumu na kumnyonga msomi na mtafiti maarufu Hassan Farhan al Maliki.
-
Jeshi la Yemen laua askari 8 wa Saudia, latungua drone nyingine ya Riyadh
Jun 23, 2019 22:27Jeshi la Yemen na vikosi vya kujitolea vya wananchi wa nchi hiyo vimejibu mashambulizi ya muungano vamizi unaoongozwa na utawala wa Aal-Saud, kwa kuua wanajeshi wanane wa Saudia katika mkoa wa Najran, kusini magharibi mwa Saudi Arabia mpakani na Yemen.
-
Yemen yatekeleza shambulizi jingine la ulipizaji kisasi katika uwanja wa ndege wa Abha, Saudia
Jun 17, 2019 08:23Vikosi vya Yemen vimetekeleza shambulizi jingine la ulipizaji kisasi kwa kuulenga uwanja wa ndege wa Abha, katika mkoa wa Asir kusini mwa Saudi Arabia. Shambulizi hilo limetekelezwa ikiwa ni katika kulipiza kisasi mauaji ya wananchi wasio na hatia wa Yemen ambao wameuawa nchini humo katika mashambulizi ya Saudia na waitifaki wake katika kipindi cha miaka minne sasa.
-
Nafasi haribifu ya Saudia na Imarati katika kuzidisha mgogoro wa Sudan
Jun 17, 2019 07:04Mgogoro wa kisiasa wa Sudan umeshika mkondo mpya hususan baada ya mauaji ya raia zaidi ya mia moja waliokuwa wamekusanyika mbele ya makao makuu ya jeshi la nchi hiyo mjini Khartoum mapema mwezi huu.