-
Qatar kuiburuza Saudia mahakamani kwa tuhuma za kuingiza siasa katika ibada ya Hijah
Jul 03, 2018 23:54Serikali ya Qatar na katika mfululizo wa kufuatilia masuala ya kisheria na kimataifa dhidi ya nchi za Saudi Arabia, Imarati, Bahrain na Misri, imetangaza kwamba imefungua mashitaka dhidi ya Riyadh kutokana na serikali ya nchi hiyo kuingiza siasa katika ibada ya Hijjah.
-
Kusimamishwa uuzaji silaha za Ubelgiji kwa Saudi Arabia
Jul 01, 2018 22:01Kufuatia hatua ya Saudi Arabia na washirika wake ya kuendelea kuishambulia kijeshi Yemen, Baraza la Kiserikali la Ubelgiji, limetoa amri ya kusimamishwa uuzaji silaha wa nchi hiyo kwa Riyadh.
-
Marekani, Israel, Saudia zinapanga njama za kuudhuri uchumi wa Iran
Jul 01, 2018 09:18Marekani, Utawala wa Kizayuni wa Israel na Saudi Arabia zinapanga njama za kuzuia na kusitisha mkondo wa ustawi wa uchumi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran lakini hazitafanikiwa.
-
Malaysia yasimamisha ushirikiano wake wa kijeshi na Saudia katika vita dhidi ya Yemen
Jun 28, 2018 08:52Waziri wa Ulinzi wa Malaysia amesema kuwa, nchi yake imesimamisha ushirikiano wake wa kijeshi na Saudi Arabia katika vita dhidi ya Yemen.
-
Human Rights Watch yafurahishwa na kuingizwa Saudia katika orodha nyeusi ya kuvunja haki za binadamu
Jun 27, 2018 03:27Shirika la kimataifa la Human Rights Watch limepokea kwa furaha hatua ya kuingizwa jina la Saudi Arabia katika orodha nyeusi ya wavunjaji wa haki za watoto wadogo na kusema kuwa hiyo ni hatua muhimu.
-
"Saudia iliipa hongo timu ya taifa ya Misri ikubali kuifunga kombe la dunia" - Mwandishi
Jun 27, 2018 03:25Mwandishi mmoja wa Misri amelalamika kuwa serikali ya nchi yake ilipokea rushwa na hongo kutoka kwa Saudi Arabia na kuilazimisha timu ya taifa ya nchi hiyo ikubali kufungwa na Saudia katika mashindano ya fainali za kombe la dunia yanayoendelea nchini Russia hivi sasa.
-
Njia ya reli ya kuiunganisha Israel na Saudi Arabia iko mbioni kujengwa
Jun 24, 2018 22:25Kanali ya Pili ya televisheni ya Israel imetangaza habari ya kukubaliana Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benajmain Netanyahu na Waziri wa Barabara na Uchukuzi wa utawala huo, Yisrael Katz, kuhusu kuanza ujenzi wa njia ya reli ya kuiunganisha Saudi Arabia na ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Shakhsia tofauti wafanya maandamano London kupinga uungaji mkono wa UK kwa Saudia Yemen
Jun 23, 2018 20:43Kundi la wawakilishi wa bunge, wahadhiri wa vyuo vikuu na watu wenye vipawa tofauti nchini Uingereza, wamefanya maandamano mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo wakilaani uungaji mkono wa serikali ya London kwa uvamizi wa Saudia nchini Yemen.
-
Qatar yataka Saudia na Imarati zitimuliwe Baraza la Haki za Binaadamu
Jun 23, 2018 09:42Baada ya kupita mwaka mmoja tangu kukatwa mahusiano ya nchi za Kiarabu na Qatar na kadhalika kuiwekea vikwazo na mzingiro wa kila upande nchi hiyo, serikali ya Doha imetaka uanachama wa Saudia na Imarati katika Baraza la Haki za Binaadamu usimamishwe.
-
Syria: Riyadh ingali inawazuia raia wetu kwenda kufanya Hija
Jun 23, 2018 02:55Serikali ya Syria imeukosoa vikali utawala wa Aal-Saud kwa kuingiza siasa katika amali tukufu ya Hija, ambapo Riyadh imewazuia raia wa Syria kwenda kutekeleza ibada hiyo kwa mwaka wa saba mfululizo.