• Wahalifu wanaotafuta damu ya watoto 1000 kufanya kafara Gabon wamekuwa janga + Sauti

    Wahalifu wanaotafuta damu ya watoto 1000 kufanya kafara Gabon wamekuwa janga + Sauti

    Jan 28, 2020 02:30

    Wazazi katika mji mkuu wa Gabon, Libreville, Jumatatu, Januari 27, 2020 hawakuwaruhusu watoto wao kwenda skuli licha ya serikali kuweka ulinzi mkali katika skuli zote za mji huo mkuu. Wazazi hao wanasema kuwa hatua hiyo pekee haiwezi kuwazuia wahalifu wanaotafuta damu za watoto elfu moja kama kafara ya kuwabakisha madarakani. Mossi Mwasi na maelezo zaidi kutoka Brazzaville.

  • Chama cha FDC chailaumu vikali serikali ya Uganda + Sauti

    Chama cha FDC chailaumu vikali serikali ya Uganda + Sauti

    Jan 20, 2020 16:18

    Kwa mara nyingine tena, mwanasiasa mkongwe katika chama cha FDC nchini Uganda, Daktari Kizza Besigye ameikosoa vikali serikali ya Rais Yoweri Museveni kutokana na ubabe na ukandamizaji unaofanywa na vyombo vya dola dhidi ya wapinzani. Kigozi Ismail na maelezo zaidi kutoka Kampala.

  • Wakazi wa kaskazini mwa Bujumbura waendelea kuteseka kwa madhara ya mafuriko + Sauti

    Wakazi wa kaskazini mwa Bujumbura waendelea kuteseka kwa madhara ya mafuriko + Sauti

    Jan 07, 2020 08:31

    Waathiriwa wa mafuriko katika baadhi ya maeneo ya kaskazini mwa Bujumbura waliopiga kambi katika madarasa ya shule wametakiwa kuondoka ili kuruhusu sehemu ya pili ya mwaka wa shule kuanza. Hata hivyo raia hao wanalalamika kutokuwa na sehemu ya kwenda. Hali hiyo imepelekea baadhi ya shule katika eneo hilo kuakhirisha kufungua muhula mpya wa masomo. Hamida Issa na maelezo zaidi kutoka Bujumbura…

  • Waislamu Zanzibar wahimizwa kujifunza elimu ya ndoa ili kuepuka talaka holela + Sauti

    Waislamu Zanzibar wahimizwa kujifunza elimu ya ndoa ili kuepuka talaka holela + Sauti

    Dec 27, 2019 15:50

    Waislamu visiwani Zanzibar hasa vijana wametakiwa kulipa umuhimu suala la elimu ya ndoa ili kupunguza wimbi la talaka za kiholela ambazo kimsingi zinahesabiwa ni sehemu moja ya kukanyaga haki za watoto. Hayo na mengineyo yamo kwenye ripoti ya kila wiki ya matukio ya Kiislamu, Afrika Mashariki, kama inavyoletwa kwenu na mwandishi wetu wa Zanzibar, Harith Subeit.

  • Hali ya utulivu yarejea Bangui, Jamhuri ya Afrika ya Kati baada ya mapigano + Sauti

    Hali ya utulivu yarejea Bangui, Jamhuri ya Afrika ya Kati baada ya mapigano + Sauti

    Dec 27, 2019 15:48

    Hali ya utulivu imerejea katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui baada ya siku mbili za mapigano baina ya makundi mawili hasimu. Mapigano hayo yamesababisha zaidi ya watu 30 kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa. Mossi Mwasi na maelezo zaidi…

  • Uganda yapongezwa na WHO kwa kukazania afya ya jamii + Sauti

    Uganda yapongezwa na WHO kwa kukazania afya ya jamii + Sauti

    Dec 27, 2019 15:45

    Serikali ya Uganda imepongezwa kwa kusimamia na kukazania vyema afya katika jamii kuanzia mashinani. Pongezi hizo zimetolewa na Shirika la Afya Duniani, WHO. Kigozi Ismail na maelezo zaidi kutoka Kampala…

  • Waziri wa zamani wa DRC ataka Rwanda ivamiwe na kugeuzwa mkoa ili mashariki mwa DRC kuwe salama + Sauti

    Waziri wa zamani wa DRC ataka Rwanda ivamiwe na kugeuzwa mkoa ili mashariki mwa DRC kuwe salama + Sauti

    Dec 25, 2019 10:44

    Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Adolphe Muzito amesema kuwa, njia pekee ya kumaliza uasi mashariki mwa nchi hiyo ni kuivamia nchi jirani ya Rwanda na kuigeuza kuwa mkoa wa DRC. Mossi Mwasi na maelezo zaidi.

  • Mashinikizo ya wananchi yailazimisha serikali DRC kufuta sherehe za kukabidhiwa madaraka Tshisekedi + Sauti

    Mashinikizo ya wananchi yailazimisha serikali DRC kufuta sherehe za kukabidhiwa madaraka Tshisekedi + Sauti

    Dec 23, 2019 09:59

    Serikali ya jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imelazimika kufutilia mbali sherehe za kupokezana madaraka kwa njia ya amani baina ya rais mstaafu wa nchi hiyo Joseph Kabila na rais wa hivi sasa Felix Tshisekedi. Hii in baada ya wananchi na asasi za kiraia kulalamikia gharama kubwa za hafla hizo zilizotazamiwa kufanyika tarehe 24 Januari mwakani. Mwandishi wetu Mossi mwazi na maelezo zaidi.

  • Mkuu wa Mkoa wa Tabora afuta mapumziko ya Mwaka Mpya; watu wakalime pamba + Sauti

    Mkuu wa Mkoa wa Tabora afuta mapumziko ya Mwaka Mpya; watu wakalime pamba + Sauti

    Dec 15, 2019 16:20

    Nchini Tanzania, Mkuu wa mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, ameagiza kuakhirishwa likizo ya A-Mass na mwaka mpya kwa maafisa wa kilimo na maafisa wote katika kipindi hiki cha mvua, ili watoke waende vijijini wakawahimize wananchi kulima pamba kwa ubora unaotakiwa. Ammar Dachi na maelezo zaidi kutoka Dar es Salaam, Tanzania

  • ACT-Wazalendo yalalamika kufanyiwa hujuma visiwani Zanzibar + Sauti

    ACT-Wazalendo yalalamika kufanyiwa hujuma visiwani Zanzibar + Sauti

    Dec 02, 2019 17:01

    Viongozi wa chama cha ACT Wazalendo visiwani Zanzibar wametahadharisha kuhusu madhara yanayoweza kutokea kutokana na kile wanachoamini ni hujuma za makusudi zinazoendeshwa dhidi ya viongozi wa chama hicho visiwani Unguja na Pemba. Harith Subeit na maelezo zaidi kutoka Zanzibar.