-
'Kuua raia mjini Kabul kumeonyesha udhaifu wa kiintelijensia wa Marekani'
Sep 20, 2021 11:22Mchambuzi wa zamani wa masuala ya usalama katika wizara ya ulinzi ya Marekani, Pentagon amesema, kukiri makamanda wa jeshi la Marekani kwamba walifanya shambulio kimakosa katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul na kuua raia wa nchi hiyo kumeonyesha udhaifu wa kiintelijensia wa Washington.
-
Mfumo wa kupiga kura kwa njia ya elektroniki nchini Russia wahujumiwa na wadukuzi
Sep 18, 2021 08:12Mwenyekiti wa Kamisheni ya Ulinzi wa Haki ya Kujitawala ya Baraza la Seneti la Russia ametangaza kuwa, mfumo wa kupiga kura kwa njia ya elektroniki nchini humo umehujumiwa na wadukuzi kutoka nchi za Magharibi.
-
Watu 19 wauawa katika shambulizi jipya la wabeba silaha Niger
Jul 30, 2021 12:39Raia 19 wameuawa kwenye shambulizi linaloaminika kuwa la kigaidi katika mpaka wa Niger na Mali.
-
Zaidi ya walowezi 400 wavamia Msikiti Mtakatifu wa al-Aqswa
Jul 18, 2021 11:23Makumi ya walowezi wa Kizayuni wameuvamia tena Msikiti wa al-Aqswa huko Palestina wakisaidiwa na askari wa jeshi la utawala haramu wa Israel na kuuvunjia heshima msikiti huo ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu.
-
Ubalozi wa Marekani Baghdad washambuliwa kwa droni
Jul 06, 2021 08:16Baadhi ya duru za habari za Iraq zimetangaza habari ya kujiri shambulio la anga katika eneo la Kijani huko Baghdad na karibu na jengo la ubalozi wa Marekani.
-
Shambulio la bomu laua, kujeruhi watu 20 Mogadishu, Somalia
Apr 29, 2021 02:25Watu wasiopungua saba wameuawa huku wengine zaidi ya 11 wakijeruhiwa baada ya gari lililokuwa limesheheni mabomu kuripuka nje ya makao makuu ya polisi katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
Kimya cha IAEA baada ya uharibifu uliofanywa katika taasisi ya nyuklia ya Iran
Apr 15, 2021 02:25Hujuma ya uharibifu iliyofanywa na Israel katika taasisi ya nishati ya nyuklia ya Natanz nchini Iran siku ya Jumapili iliyopita, kwa mara nyingine tena imeleta udharura wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kama taasisi kuu zaidi ya kimataifa inayosimamia shughuli za nyuklia dunia, kutoa jibu na kueleza wazi msimamo wake.
-
Iran kuwaanika wahusika wa shambulio dhidi ya meli yake ya mizigo
Mar 14, 2021 07:58Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inafuatilia suala la kuwatambua watu waliohusika na shambulio la kigaidi dhidi ya meli ya mafuta ya nchi hii katika maji ya kimataifa na karibuni hivi itawaanika.
-
Russia: Mashambulio ya Marekani Syria ni ukiukaji wa kanuni na sheria za kimataifa
Feb 26, 2021 13:14Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imelaani mashambulizi ya usiku wa kuamikia leo ya Marekani huko Syria na kuyataja kuwa ni kinyume na kanuni na sheria za kimataifa.
-
Maajenti 12 wa usalama wauawa katika shambulio la bomu Somalia
Feb 08, 2021 12:11Mkuu wa Idara ya Intelijensia ya Somalia pamoja na maajenti 11 wa kitengo hicho cha usalama wameuawa katika mripuko wa bomu la kutegwa kando ya barabara katika jimbo la Galmudug, katikati ya nchi.