-
Somalia yamteua mkuu mpya wa jeshi kuchukua nafasi ya Jenerali Rage
Jan 30, 2026 02:49Baraza la Mawaziri la Somalia limemteua Brigedia Jenerali Ibrahim Mohamed Mohamud kuwa Kamanda mpya wa Jeshi la Taifa la Somalia (SNA). Hii ni kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu wa Somalia iliyosomwa na msemaji wa serikali, Abdinasir Ahmed Bashir.
-
Je, Tel Aviv inalenga kuizingira kimkakati Misri katika Bahari Nyekundu?
Jan 29, 2026 03:24Misri, katika kujibu kuongezeka kwa ushawishi na uingiliaji wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Pembe ya Afrika, imeimarisha uwepo wake wa kijeshi nchini Somalia.
-
Somalia yakamata msaada wa chakula uliorejeshwa kwa WFP baada ya kutoelewana na Marekani
Jan 28, 2026 04:27Serikali ya Somalia imesema kuwa msaada wa chakula uliotolewa kwenye ghala wakati wa shughuli za upanuzi wa bandari katika mji mkuu, Mogadishu, umerejeshwa kwa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), kufuatia ripoti kwamba maafisa wa eneo hilo wamekamata msaada wa chakula uliotolewa na nchi wafadhili.
-
Serikali ya Somalia imechukua hatua gani katika kukabiliana na kujitenga kwa Somaliland?
Jan 21, 2026 07:58Kufuatia kuongezeka harakati za watu wanaotaka kujitenga huko Somaliland baada ya kutambuliwa rasmi na utawala wa Kizayuni wa Israel, serikali ya Somalia imechukua hatua mpya za kukabiliana na harakati hizo katika eneo hilo.
-
Rais wa Somalia atoa wito kwa Somaliland kushiriki katika mazungumzo
Jan 18, 2026 12:35Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amewatolea wito maafisa wa Somaliland kushiriki katika mazungumzo na serikali yake; akisema kuwa yuko tayari kuafikiana katika masuala yote isipokuwa "umoja wa nchi."
-
Magaidi 30 wa al-Shabaab wauawa na vikosi vya Somalia, Uganda na AU
Jan 16, 2026 02:13Vikosi vya Somalia, Uganda na Umoja wa Afrika (AU) jana Alhamisi viliwaangamiza zaidi ya wanamgambo 30 wa al-Shabaab, na kujeruhi wengine kadhaa wakati wa operesheni ya pamoja huko kusini mwa Somalia.
-
Jeshi la Somalia laangamiza magaidi 17 wa al-Shabaab
Jan 14, 2026 06:26Wizara ya Ulinzi wa Somalia imesema kwamba, Jeshi la Kitaifa la nchi hiyo limewaua magaidi 17 wa al-Shabaab katika operesheni ya anga iliiyofanyika kusini mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Somalia: Israel kuwahamishia kwa nguvu Wapalestina Somaliland ni kinyume cha sheria za kimataifa
Jan 11, 2026 06:56Waziri wa Ulinzi wa Somalia, Ahmed Moalim Fiqi, ameishutumu Israel kwa kupanga kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina wa Ukanda wa Gaza na kuwapeleka katika eneo lililojitenga la Somaliland, akiukashifu mpango huo alioutaja kuwa ni "ukiukaji mkubwa" wa sheria za kimataifa.
-
Somalia yakanusha madai ya Marekani ya kutwaa chakula cha WFP
Jan 09, 2026 02:23Somalia jana Alhamisi ilikanusha madai ya Marekani kwamba maafisa wa eneo hilo wametwaa bidhaa za chakula kutoka katika ghala la shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), huku Washington ikisimamisha misaada kwa Mogadishu kusubiri uchunguzi.
-
Somalia yapokezwa uenyekiti wa kiduru wa Baraza la Usalama la UN
Jan 03, 2026 06:03Somalia jana Ijumaa ilichukua urais wa zamu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kipindi cha mwezi huu wa Januari, ikiwa ni mara ya kwanza kwa nchi hiyo kushikilia wadhifa huo tangu ilipohudumu mara ya mwisho katika baraza hilo mwaka 1971-72.