-
AU: Tuko tayari kusimamia mazungumzo ya kukwamua mgogoro wa kisiasa Somalia
Apr 22, 2021 22:02Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika limesema liko tayari kuandaa na kusimamia mazungumzo ya kukwamua mgogoro wa kisiasa unaoikabili Somalia.
-
Nigeria yatuma makumi ya askari polisi wake nchini Somalia
Apr 19, 2021 03:17Kikosi cha askari polisi 144 wa Nigeria kimewasili nchini Somalia, kwenda kupiga jeki jitihada za kurejesha uthabiti katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Jeshi la Somalia lachukua udhibiti wa ngome za magaidi wa al-Shabab
Apr 08, 2021 08:42Jeshi la Somalia (SNA) limetangaza kuchukua udhibiti wa kambi kadhaa za kundi la kigaidi la al-Shabab huko Galgaduud, katikati mwa Somalia.
-
Viongozi wa Somalia washindwa kukubaliana juu ya ajenda ya mkutano muhimu wa uchaguzi
Apr 05, 2021 08:24Viongozi wa Somalia wameshindwa kufikia makubaliano juu ya ajenda kuu ya mkutano muhimu wa uchaguzi, suala ambalo limedhihirisha tena ufa uliopo kati ya makundi ya kisiasa ya Somalia.
-
Magaidi 76 wa al-Shabaab wauawa na jeshi la Somalia
Apr 04, 2021 06:32Jeshi la Somalia limesema kuwa limeangamiza makumi ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab katika operesheni ya kiusalama kusini mwa Somalia.
-
Askari wa Somalia wazima hujuma za al-Shabaab dhidi ya kambi za jeshi
Apr 03, 2021 05:12Jeshi la Taifa la Somalia limetangaza kuwa, askari wa nchi hiyo wamefanikiwa kuzima mashambulio ya kundi la kigaidi la al-Shabaab yaliyolenga kambi mbili za kijeshi kusini mwa nchi.
-
Katibu Mkuu wa UN ana wasiwasi kuhusu mkwamo wa kisiasa Somalia
Mar 26, 2021 03:22Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mkwamo wa kisiasa unaondelea nchini Somalia kuhusu uchaguzi mkuu licha ya kufanyika duru kadhaa za majadiliano miongoni mwa wadau wa kisiasa nchini humo katika ngazi zote ni suala linalomtia wasiwasi mkubwa.
-
Raia kadhaa wauawa na kujeruhiwa katika shambulio la kombora mjini Mogadishu, Somalia
Mar 25, 2021 22:26Raia wasiopungua watatu wameuawa na wengine watano wamejeruhiwa baada ya makombora kadhaa kulenga ofisi kuu za vikosi vya Umoja wa Mataifa na vya Umoja wa Afrika vinavyolinda amani nchini Somalia (AMISOM) zilizoko katika mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu.
-
Alkhamisi, 25 Machi, 2021
Mar 24, 2021 21:56Leo ni Alkhamisi tarehe 11 ya mwezi Shaaban 1442 Hijria mweafaka na tarehe 25 Machi 2021 Miladia.
-
Somalia yazindua kampeni ya kitaifa ya utoaji chanjo ya Corona
Mar 17, 2021 01:10Rais Mohamed Abdullahi Farmaajo wa Somalia hapo jana alipokea chanjo ya Corona ya shirika la AstraZeneca la Uingereza, kuashiria kuanza kwa kampeni ya kitaifa ya utoaji wa chanjo ya Corona katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.