-
WHO: Wagonjwa wa kipindupidu Sudan wafikia 113,500; chanjo yaendelea kutolewa
Sep 23, 2025 08:23Shirika la Afya Duniani leo Jumanne limetangaza kuwa mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu umewaathiri watu zaidi ya 113,600 na kuuwa zaidi ya 3,000 kote nchini humo tangu Julai mwaka jana.
-
Taasisi ya misaada Sudan: Shambulio la RSF limeua watu 75 Darfur
Sep 19, 2025 23:07Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF vimewaua watu 75 katika shambulio la ndege zisizo na rubani lililolenga msikiti mmoja katika kambi ya watu waliolazimika kuyahama makazi yao kwenye jimbo la Darfur nchini Sudan. Hayo yameelezwa na taasisi ya utoaji misaada inayoendesha eneo hilo inayojulikana kama Chumba cha Mjibizo wa Dharura (Emergency Response Room).
-
Zaidi ya 1,000 waaga dunia katika maporomoko ya ardhi Darfur, Sudan
Sep 02, 2025 03:33Kwa akali watu 1,000 wamepoteza maisha katika maporomoko ya ardhi yaliyoharibu kijiji kizima katika eneo la Milima ya Marra magharibi mwa Sudan.
-
Kamanda wa wanamgambo wa RSF aapishwa kuwa Mkuu wa serikali sambamba huko Sudan
Sep 01, 2025 04:15Mohammed Hamdan Dagalo kamanda wa wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) jana aliapishwa kuwa kiongozi wa serikali sambamba nchini Sudan.
-
Raia 5 wa familia moja wauawa katika shambulio la droni la RSF huko Kordofan ya Kaskazini
Aug 31, 2025 03:53Jeshi la Sudan limetangaza kuwa raia watano kutoka kwa familia moja, wakiwemo binti wawili, wameuawa katika shambulio la ndege isiyo na rubani lililotekelezwa na Kikosi cha Wanamgambo waMsaada wa Haraka (RSF) katika Jimbo la Kordofan Kaskazini, kusini mwa Sudan.
-
Katibu Mkuu wa UN alaani mashambulizi yasiyokoma ya RSF dhidi ya mji wa El Fasher, Sudan
Aug 30, 2025 02:23Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani vikali mashambulizi yanayofanywa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, RSF dhidi ya mji wa El Fasher, kaskazini mwa jimbo la Darfur nchini Sudan huko akitoa indhari juu ya maafa makubwa ya kibinadamu na ukiukaji wa sheria za kimataifa unaofanywa katika mji huo.
-
UNICEF yaonya: Watoto wamenasa kwenye janga la kutisha El Fasher, Sudan
Aug 28, 2025 22:53Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limeonya juu ya janga kubwa la kuogofya linalowawajihi watoto walionasa mjini El-Fasher, makao makuu ya jimbo la Darfur Kaskazini, magharibi mwa Sudan.
-
Raia 13 wauawa na wanamgambo wa RSF huko Darfur, Sudan
Aug 25, 2025 07:04Raia wasiopungua 13 wa Sudan wameripotiwa kuuawa na wapiganaji wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) huko Darfur Kaskazini.
-
Sudan yaripoti wagonjwa wapya wa kipindupindu 1,575, vifo 22
Aug 20, 2025 03:00Wizara ya Afya ya Sudan imetangaza kuwa wagonjwa 1,575 wapya wa kipindupindu na vifo 22 vimesajiliwa kote nchini humo katika muda wa wiki moja iliyopita.
-
Watu 21 waaga dunia kwa kipindupindu nchini Sudan katika muda wa wiki moja
Aug 06, 2025 03:22Wizara ya Afya ya Sudan jana ilitangaza kuwa raia wa nchi hiyo wasiopungua 21 wameaga dunia katika muda wa wiki moja baada ya kuugua kipindupindu huku maambukizo mapya yakiripotiwa kufikia 2,345.