-
Wagonjwa wapya 14 wa COVID-19 wabainika nchini Tanzania
Apr 13, 2020 03:41Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto wa Tanzania, Ummy Mwalimu amesema kuwa, watu 14 ambao wote ni raia wa Tanzania wamepatikana na ugonjwa wa corona na kufanya idadi ya watu walioambukizwa ugonjwa wa COVID-19 nchini humo kufikia 46.
-
Hatimaye corona yailazimisha Tanzania kupiga marufu safari za ndege, Marekani yaongoza kwa vifo na maambukizi
Apr 12, 2020 23:16Hatimaye serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepiga marufuku safari zote za ndege za abiria za kimataifa ikiwa ni siku chache tu baada ya Rais John Pombe Magufuli wa nchi hiyo kusisitizia msimamo wake wa kutofunga mipaka ya Tanzania akisema kuwa kufunga mipaka hiyo kutaziletea madhara makubwa nchi jirani kama za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Magufuli: Mlipuko wa corona hautafanya uchaguzi mkuu wa Tanzania uakhirishwe
Mar 26, 2020 08:47Rais John Magufuli wa Tanzania amesema uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu hautaakhirishwa licha ya kuwepo kwa mlipuko wa virusi vya corona.
-
Watu 27 waliochukuliwa sampuli ya vipimo vya Corona Tanzania, wako salama
Mar 19, 2020 13:02Watu 27 ambao walichukuliwa sampuli za vipimo vya afya ili kuwachunguza iwapo wameambukizwa virusi vya Corona Covid-19, wapo salama.
-
Mmarekani na Mjerumani waongeza idadi ya walioingia na corona nchini Tanzania
Mar 18, 2020 09:29Idadi ya watu walio na ugonjwa wa COVID-19 imeongezeka nchini Tanzania baada ya vipimo vya raia wawili wa Marekani na Ujerumani kuthibitika kuwa wameambukizwa kirusi cha corona.
-
Tanzania; Mufti afunga madrasa zote, hali ya mgonjwa wa kwanza wa corona inaendelea vizuri
Mar 18, 2020 09:17Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amewaagiza walimu wa madrasa kufunga madrasa zote nchini humo hadi utakapotangazwa utaratibu mpya.
-
SAUTI, Serikali ya Tanzania yafunga shule zote kuanzia za msingi na secondari kuzuia maambukizi ya virusi hatari vya Corona
Mar 17, 2020 13:47Serikali ya Tanzania imesema shule zote za awali, msingi na sekondari zitafungwa kwa siku 30 kuanzia leo Jumanne Machi 17, ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya virusi vya corona (CODIV-19) ndani ya nchi hiyo.
-
Serikali ya Tanzania yafunga shule, matamasha na michezo kwa hofu ya corona
Mar 17, 2020 11:26Serikali ya Tanzania imesema shule zote za awali, msingi na sekondari zitafungwa kwa siku 30 kuanzia leo Jumanne Machi 17, 2020 ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya virusi vya corona (CODIV-19)
-
Tanzania yathibitisha kuwepo mgonjwa wa corona nchini humo
Mar 16, 2020 10:51Serikali ya Tanzania imetangaza kuwepo mgonjwa wa COVID-19 maarufu kama virusi vya corona ambaye aliingia nchini humo jana Jumapili.
-
Jeshi la Polisi Tanzania: Hatujawapiga wabunge wa upinzani
Mar 14, 2020 10:07Jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam limetupilia mbali madai ya kuwapiga wabunge wa chama cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na kusisitiza kuwa, hilo sio jukumu lake.