-
Albino kuandamana Tanzania kulaani jinai wanazofanyiwa
Apr 28, 2019 13:28Chama cha Watu Wenye Ulemavu wa Ngozi (Albino) nchini Tanzania kimeazimia kufanya maandamano ya kulaani jinai wanazofanyiwa ikiwemo ufukuaji wa makaburi ya watu wenye ulemavu huo na kuondoka na viungo vyao. Uovu huo uko zaidi mkoani Mbeya. Ammar Dachi na maelezo zaidi kutoka Dar es Salaam, Tanzania...
-
Kimbunga cha Kenneth kufika kusini mwa Tanzania usiku wa leo, tahadhari zachukuliwa + Sauti
Apr 25, 2019 12:12Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA) imetangaza kuwa, kimbunga Kenneth kimeongezeka kasi na kinatarajiwa kufika pwani ya kusini ya Tanzania na kaskazini mwa Msumbiji kuanzia usiku wa leo. Hadi sasa wameshapokelewa watu takribani mia sita katika eneo la hifadhi. AMARI DACHI na taarifa zaidi akiripoti kutoka Dar es Salaam
-
Mvua, mafuriko na maporomoko ya ardhi yaua makumi ya watu Tanzania na Uganda
Apr 24, 2019 03:29Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika nchi za Afrika Mashariki zimesababisha vifo vya makumi ya watu katika nchi za Uganda na Tanzania.
-
Serikali ya Tanzania: Hatujazuia kuchapishwa ripoti ya IMF, bado tunafanya majadiliano nao
Apr 23, 2019 09:50Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema kuwa bado inaendelea kufanya majadiliano na Shirika la Fedha Duniani (IMF) kuhusiana na ripoti ya hivi karibuni ya shirika hilo kuulenga uchumi wa nchi hiyo.
-
SAUTI, Ripoti ya matukio ya Kiislamu, madrasa zatakiwa kuwa na mtaala mmoja, Mufti wa Tanzania asema; Uislamu haukatazi uzazi wa mpango
Apr 19, 2019 13:51Ripoti ya matukio ya Kiislamu iliyoandaliwa na mwandishi wetu wa visiwani Zanzibar, Harith Subeit. Inaanza kuangazia macho sisitizo la uwepo wa mitaala ya kufundishia kwa ajili ya madrasa zote visiwani Zanzibar.
-
IMF: Uchumi wa Tanzania utadhoofika kutokana na sera za serikali
Apr 19, 2019 03:38Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) umetahadharisha kuwa, uchumi wa Tanzania utadhoofika iwapo sera za sasa na sheria mpya zitaendelea kutekelezwa.
-
Fatma Karume: Bunge la Tanzania lilizingatia maana gani ya neno ‘Dhaifu’ la profesa Assad?
Apr 15, 2019 08:58Mwanasheria maarufu nchini Tanzania Fatma Karume amekosoa hoja ya Spika wa Bunge la nchi hiyo aliyesema kuwa bunge hilo halitofanya kazi na CAG na kwamba badala yake litafanya kazi na ofisi yake na kuongeza kuwa, katika katiba ya nchi hiyo mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hakuna mahala panaposema kwamba ‘kuna ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).’
-
CAG wa Tanzania: Tutaendelea kutumia neno 'Dhaifu' katika ripoti zetu
Apr 10, 2019 12:05Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanania, Profesa Mussa Assad amesema kuwa, wataendelea kutumia neno 'dhaifu' katika maeneo tofauti ya ukaguzi wao kulingana na taratibu za kazi hiyo zilivyo na kwamba hata ripoti aliyoiwasilisha leo pia ina neno dhaifu.
-
Wasomi Tanzania: Bunge limewasaliti wananchi kwa kutoshirikiana na CAG
Apr 03, 2019 11:47Baada ya Bunge kuazimia kutoshirikiana na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali nchini Tanzania, mhadhiri msaidizi wa Chuo Kikuu cha Tumaini jijini Dar es salaam (TUDARCO) Danford Kitwana amesema kitendo hicho cha bunge ni kuwasaliti wananchi wake.
-
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Tanzania alionya Bunge
Apr 03, 2019 10:26Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Tanzania, Profesa Mussa Juma Assad ametahadharisha kuhusu matokeo mabaya ya hatua ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kupasisha azimio la kutofanya kazi naye.