-
Ajali za barabarani zaua watu 25 Tanzania ndani ya saa 24
Jun 11, 2022 06:48Watu watano wamepoteza maisha na wengine tisa wamejeruhiwa baada ya basi dogo aina ya Coaster waliyokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka nchini Tanzania.
-
Jumanne tarehe 26 Aprili 2022
Apr 25, 2022 22:09Leo ni Jumanne tarehe 24 mwezi mtukufu wa Ramadhani 1443 Hijria sawa na tarehe 26 Aprili mwaka 2022.
-
Rais Samia anadi fursa za uwekezaji na utalii nchini Tanzania katika ziara yake Marekani
Apr 16, 2022 08:40Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana alikuwa na mazungumzo na Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Haris, kwa lengo la kufufua sekta ya utalii nchini Tanzania na kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo mbili.
-
Sensa Tanzania: Rais Samia atangaza tarehe ya kuhesabiwa Watanzania
Apr 08, 2022 08:36Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniza, Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi nembo ya sensa na kutangaza kuwa siku ya sensa ya watu na makazi nchini humo itakuwa Jumanne Agosti 23, mwaka huu 2022.
-
Benki za Kiislamu Tanzania zakumbatiwa na wasiokuwa Waislamu
Apr 06, 2022 21:27Benki za Kiislamu nchini Tanzania zimeendelea kupata umaarufu na kupongezwa kwa huduma zao, na sasa zinawavutia kwa wingi hata wateja wasiokuwa Waislamu nchini humo.
-
Rais Samia avitaka vyama vya kisiasa Tanzania kushiriki katika kuleta maendeleo ya taifa
Apr 05, 2022 07:17Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amehudhuria Mkutano wa Kitaifa wa Maridhiano, Haki na Amani ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD).
-
Uhaba wa mafuta ya petroli wawalazimisha Wakenya kwenda Tanzania kuyatafuta
Apr 02, 2022 08:33Uhaba wa mafuta ya petroli katika Kaunti ya Kwale, Pwani ya Kenya umewalazimisha madereva kusafiri hadi katika nchi jirani ya Tanzania kupitia mpaka wa Lungalunga ili kutafuta bidhaa hiyo muhimu, huku wafanyabiashara wakipandisha bei kutokana na uhaba mkubwa wa bidhaa hiyo nchini Kenya.
-
Kongamano la Idhaa za Kiswahili lamalizika Tanzania, waandishi waaswa kutochanganya Kiswahili na Kiingereza
Mar 21, 2022 08:47Kongamano la kimataifa la Idhaa za Kiswahili limemalizika mjini Arusha Tanzania, kwa washiriki, hasa waandishi wa habari, kukumbushwa umuhimu wa kutekeleza jukumu lao la kuzungumza lugha fasaha ya Kiswahili ili wananchi wanaowasikiliza waweze kujifunza kutoka kwao.
-
Tanzania yakaribisha pendekezo la Iran la kutoa elimu na mafunzo ya ujuzi kwa wanawake wa nchi hiyo
Mar 20, 2022 06:27Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu wa Tanzania amekaribisha pendekezo lililotolewa na Makamu wa Rais wa Iran katika Masuala ya Wanawake na Familia la kuwapatia mafunzo ya ujuzi wanawake na wasichana wa Tanzania.
-
Mahakama Tanzania yamuachia huru Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe
Mar 04, 2022 08:54Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania, Freeman Mbowe na wenzake watatu, leo Ijumaa wamefutiwa mashtaka yote yaliyokuwa yakiwakabili katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.