-
Chama cha Nahdha Tunisia chataka kuhitimishwa ukandamizaji dhidi ya waandamanaji
Jan 15, 2022 23:15Chama cha Nahdha cha Tunisia kimetoa taarifa kikitaka kuhitimishwa vitendo vya utumiaji mabavu na ukandamizaji unaofanywa na vikosi vya usalama dhidi ya maandamano ya amani ya wananchi wa nchi hiyo.
-
Rais wa Tunisia akosolewa kwa kuandaa bajeti bila kumshirikisha yeyote
Jan 15, 2022 07:39Muungano wa Wafanyakazi Tunisia (UGTT) umemkosoa vikali Rais Kais Saied wa nchi hiyo, kwa kutwaa mamlaka yote ya nchi, na kuandaa bajeti ya nchi yeye binafsi pasi na kuzishirikisha taasisi nyingine husika.
-
Maandamano dhidi ya serikali nchini Tunisia katika maadhimisho ya mapinduzi ya Januari 14
Jan 15, 2022 07:11Sambamba na kumbukumbu ya mwaka wa 11 wa harakati ya wananchi wa Tunisia iliyopelekea kupinduliwa serikali ya dikteta wa zamani wa nchi hiyo, Zine El Abidine Ben Ali, Tunisia jana Ijumaa ilishuhidia maandamano makubwa ya kupinga utendaji wa kiongozi wa sasa wa nchji hiyo, Kais Saied.
-
Chama cha Ennahda Tunisia chatoa wito wa maandamano makubwa Ijumaa ijayo
Jan 11, 2022 10:40Chama cha Ennahda chenye mfungamano na Harakati ya Ikhwanul Muslimini cha Tunisia kimetoa taarifa kikiwatolea wito wananchi kushiriki kwa wingi katika maandamano yatakayofanyika nchini humo Ijumaa tarehe 14 mwezi huu wa Januari.
-
Spika wa Bunge, Mawaziri Wakuu wa zamani wa Tunisia kupandishwa kizimbani
Jan 07, 2022 23:19Spika wa bunge lililovunjwa la Tunisia na Mawaziri Wakuu wa zamani wa nchi hiyo watafikishwa kizimbani kwa tuhuma za kukiuka sheria za kampeni za kisiasa na kutobainisha vyanzo vya fedha zao wakati wa kampeni za uchaguzi.
-
Spika wa bunge lililovunjwa na waziri mkuu wa zamani wa Tunisia wafunguliwa mashtaka
Jan 06, 2022 04:26Spika wa Bunge lililovunjwa na waziri mkuu wa zamani wa Tunisia watafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kukiuka sheria za uendeshaji kampeni za kisiasa na kutobainisha wazi vyanzo vya fedha walizotumia katika kampeni za uchaguzi.
-
Miito yatolewa Tunisia kwa ajili ya kuachiwa huru Naibu Mkuu wa Annahdha
Jan 02, 2022 23:05Miito imeendelea kutolewa nchini Tunisia ili kuachiwa huru mwanasiasa aliyeko kizuini, Noureddine Bhiri, ambaye pia ni Naibu Mkuu wa chama kikubwa zaidi cha kisiasa huko Tunisia cha Annahdha.
-
Afisa mwandamizi wa Annahdha 'atekwa nyara' na maafisa usalama Tunisia
Jan 01, 2022 09:04Harakati ya Annahdha nchini Tunisia imesema kuwa, afisa mwandamizi wa chama hicho cha kisiasa ametiwa mbaroni na maafisa usalama wa nchi hiyo.
-
Indhari kuhusu kurejea udikteta huko Tunisia
Dec 30, 2021 08:06Rached Ghannouchi Spika wa Bunge lililosimamishwa la Tunisia amezitaja hatua na maamuzi yanayochukuliwa na Rais wa nchi hiyo, Kais Saied kuwa ni sawa ni kuhuisha tajiriba iliyofeli na kueleza kuwa, Tunisia inaelekea katika mkondo wa kurejea kwenye udikteta na kutengwa.
-
Kongamano la kumuenzi Qassem Soleimani na Abu Mahdi al-Mohandes lafanyika Tunisia
Dec 30, 2021 04:47Kundi la vyama vya siasa na asasi za kiraia nchini Tunisia zimefanya kongamano kwa mnasaba wa mwaka wa pili wa kuuawa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) na Abu Mahdi al-Muhandis, Naibu Mkuu wa Kikosi cha Kujitolea cha Wananchi wa Iraq cha Hashd al Sha'abi.