-
Spika wa Bunge, Mawaziri Wakuu wa zamani wa Tunisia kupandishwa kizimbani
Jan 08, 2022 02:49Spika wa bunge lililovunjwa la Tunisia na Mawaziri Wakuu wa zamani wa nchi hiyo watafikishwa kizimbani kwa tuhuma za kukiuka sheria za kampeni za kisiasa na kutobainisha vyanzo vya fedha zao wakati wa kampeni za uchaguzi.
-
Spika wa bunge lililovunjwa na waziri mkuu wa zamani wa Tunisia wafunguliwa mashtaka
Jan 06, 2022 07:56Spika wa Bunge lililovunjwa na waziri mkuu wa zamani wa Tunisia watafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kukiuka sheria za uendeshaji kampeni za kisiasa na kutobainisha wazi vyanzo vya fedha walizotumia katika kampeni za uchaguzi.
-
Miito yatolewa Tunisia kwa ajili ya kuachiwa huru Naibu Mkuu wa Annahdha
Jan 03, 2022 02:35Miito imeendelea kutolewa nchini Tunisia ili kuachiwa huru mwanasiasa aliyeko kizuini, Noureddine Bhiri, ambaye pia ni Naibu Mkuu wa chama kikubwa zaidi cha kisiasa huko Tunisia cha Annahdha.
-
Afisa mwandamizi wa Annahdha 'atekwa nyara' na maafisa usalama Tunisia
Jan 01, 2022 12:34Harakati ya Annahdha nchini Tunisia imesema kuwa, afisa mwandamizi wa chama hicho cha kisiasa ametiwa mbaroni na maafisa usalama wa nchi hiyo.
-
Indhari kuhusu kurejea udikteta huko Tunisia
Dec 30, 2021 11:36Rached Ghannouchi Spika wa Bunge lililosimamishwa la Tunisia amezitaja hatua na maamuzi yanayochukuliwa na Rais wa nchi hiyo, Kais Saied kuwa ni sawa ni kuhuisha tajiriba iliyofeli na kueleza kuwa, Tunisia inaelekea katika mkondo wa kurejea kwenye udikteta na kutengwa.
-
Kongamano la kumuenzi Qassem Soleimani na Abu Mahdi al-Mohandes lafanyika Tunisia
Dec 30, 2021 08:17Kundi la vyama vya siasa na asasi za kiraia nchini Tunisia zimefanya kongamano kwa mnasaba wa mwaka wa pili wa kuuawa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) na Abu Mahdi al-Muhandis, Naibu Mkuu wa Kikosi cha Kujitolea cha Wananchi wa Iraq cha Hashd al Sha'abi.
-
Marzouki ajibu mapigo, asema hukumu dhidi yake haina maana, imetolewa na rais asiye halali
Dec 24, 2021 02:50Rais wa zamani wa Tunisia Moncef Marzouki amesema kuwa tuhuma zote zinazomkabili zimepindua uhakika wa mambo na zinamhusu Rais Kais Saied mwenyewe. Al Marzouki ametoa matamshi hayo akizungumzia hukumu ya awali iliyotolewa dhidi yake na mahakama nchini Tunisia bila ya kuwepo mahakamani, na kumhukumu kifungo cha miaka 4 jela.
-
Rais wa zamani wa Tunisia ahukumiwa kifungo cha miaka minne jela kwa kumpinga rais
Dec 23, 2021 07:12Mahakama ya Tunisia imemhukumu rais wa zamani wa nchi hiyo Mohamed Moncef Marzouki kifungo cha miaka minne jela.
-
Mwanasheria wa Tunisia awasilisha mashtaka ya "uhaini mkubwa" dhidi ya Kais Saied, Al Sisi na mrithi wa utawala wa Imarati
Dec 23, 2021 02:51Mwanasheria wa Tunisia ametangaza kuwa amefungua kesi mahakamani dhidi ya baadhi ya maafisa wa serikali ya Tunisia na baadi ya viongozi wa Kiarabu kwa tuhuma za "uhaini mkubwa".
-
Tume ya Uchaguzi Tunisia: Rais Saied hakushauriana nasi kuhusu kura ya maoni au uchaguzi
Dec 16, 2021 16:40Adel Brinsi ambaye ni mjumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi nchini Tunisia, amesema kuwa Rais Kais Saied wa nchi hiyo hakushauriana na mamlaka hiyo kuhusu suala la kuitisha kura ya maoni ya marekebisho ya Katiba au uchaguzi ujao wa Bunge uliopangwa kufanyika Disemba 17 mwaka ujao.