-
Chama cha Ennahda Tunisia chatoa wito wa maandamano makubwa Ijumaa ijayo
Jan 11, 2022 10:40Chama cha Ennahda chenye mfungamano na Harakati ya Ikhwanul Muslimini cha Tunisia kimetoa taarifa kikiwatolea wito wananchi kushiriki kwa wingi katika maandamano yatakayofanyika nchini humo Ijumaa tarehe 14 mwezi huu wa Januari.
-
Spika wa Bunge, Mawaziri Wakuu wa zamani wa Tunisia kupandishwa kizimbani
Jan 07, 2022 23:19Spika wa bunge lililovunjwa la Tunisia na Mawaziri Wakuu wa zamani wa nchi hiyo watafikishwa kizimbani kwa tuhuma za kukiuka sheria za kampeni za kisiasa na kutobainisha vyanzo vya fedha zao wakati wa kampeni za uchaguzi.
-
Spika wa bunge lililovunjwa na waziri mkuu wa zamani wa Tunisia wafunguliwa mashtaka
Jan 06, 2022 04:26Spika wa Bunge lililovunjwa na waziri mkuu wa zamani wa Tunisia watafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kukiuka sheria za uendeshaji kampeni za kisiasa na kutobainisha wazi vyanzo vya fedha walizotumia katika kampeni za uchaguzi.
-
Miito yatolewa Tunisia kwa ajili ya kuachiwa huru Naibu Mkuu wa Annahdha
Jan 02, 2022 23:05Miito imeendelea kutolewa nchini Tunisia ili kuachiwa huru mwanasiasa aliyeko kizuini, Noureddine Bhiri, ambaye pia ni Naibu Mkuu wa chama kikubwa zaidi cha kisiasa huko Tunisia cha Annahdha.
-
Afisa mwandamizi wa Annahdha 'atekwa nyara' na maafisa usalama Tunisia
Jan 01, 2022 09:04Harakati ya Annahdha nchini Tunisia imesema kuwa, afisa mwandamizi wa chama hicho cha kisiasa ametiwa mbaroni na maafisa usalama wa nchi hiyo.
-
Indhari kuhusu kurejea udikteta huko Tunisia
Dec 30, 2021 08:06Rached Ghannouchi Spika wa Bunge lililosimamishwa la Tunisia amezitaja hatua na maamuzi yanayochukuliwa na Rais wa nchi hiyo, Kais Saied kuwa ni sawa ni kuhuisha tajiriba iliyofeli na kueleza kuwa, Tunisia inaelekea katika mkondo wa kurejea kwenye udikteta na kutengwa.
-
Kongamano la kumuenzi Qassem Soleimani na Abu Mahdi al-Mohandes lafanyika Tunisia
Dec 30, 2021 04:47Kundi la vyama vya siasa na asasi za kiraia nchini Tunisia zimefanya kongamano kwa mnasaba wa mwaka wa pili wa kuuawa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) na Abu Mahdi al-Muhandis, Naibu Mkuu wa Kikosi cha Kujitolea cha Wananchi wa Iraq cha Hashd al Sha'abi.
-
Marzouki ajibu mapigo, asema hukumu dhidi yake haina maana, imetolewa na rais asiye halali
Dec 23, 2021 23:20Rais wa zamani wa Tunisia Moncef Marzouki amesema kuwa tuhuma zote zinazomkabili zimepindua uhakika wa mambo na zinamhusu Rais Kais Saied mwenyewe. Al Marzouki ametoa matamshi hayo akizungumzia hukumu ya awali iliyotolewa dhidi yake na mahakama nchini Tunisia bila ya kuwepo mahakamani, na kumhukumu kifungo cha miaka 4 jela.
-
Rais wa zamani wa Tunisia ahukumiwa kifungo cha miaka minne jela kwa kumpinga rais
Dec 23, 2021 03:42Mahakama ya Tunisia imemhukumu rais wa zamani wa nchi hiyo Mohamed Moncef Marzouki kifungo cha miaka minne jela.
-
Mwanasheria wa Tunisia awasilisha mashtaka ya "uhaini mkubwa" dhidi ya Kais Saied, Al Sisi na mrithi wa utawala wa Imarati
Dec 22, 2021 23:21Mwanasheria wa Tunisia ametangaza kuwa amefungua kesi mahakamani dhidi ya baadhi ya maafisa wa serikali ya Tunisia na baadi ya viongozi wa Kiarabu kwa tuhuma za "uhaini mkubwa".