-
Tume ya Uchaguzi Tunisia: Rais Saied hakushauriana nasi kuhusu kura ya maoni au uchaguzi
Dec 16, 2021 13:10Adel Brinsi ambaye ni mjumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi nchini Tunisia, amesema kuwa Rais Kais Saied wa nchi hiyo hakushauriana na mamlaka hiyo kuhusu suala la kuitisha kura ya maoni ya marekebisho ya Katiba au uchaguzi ujao wa Bunge uliopangwa kufanyika Disemba 17 mwaka ujao.
-
Rais wa Tunisia: Bunge linaendelea kusitishwa hadi uchaguzi mpya utakapoandaliwa
Dec 13, 2021 23:53Rais wa Tunisia Kais Saied alitangaza jioni ya Jumatatu jana kwamba Bunge la nchi hiyo litaendelea kusitishwa hadi uchaguzi mpya utakapoandaliwa, akiyashutumu makundi ya kisiasa kuwa yamesaliti nchi na kupora fedha za umma.
-
Mabrouk: Tunisia sasa iko nje ya klabu ya mataifa ya kidemokrasia
Dec 11, 2021 04:39Waziri wa zamani wa Tunisia ameseaa kuwa nchi hiyo imeachana na klabu ya nchi za kidemokrasia baada ya rais wa nchi hiyo kutwaa mamlaka yote ya utendaji mapema mwaka huu, na kusababisha mzozo mkubwa wa kisiasa nchini humo.
-
Kuendelea mgogoro wa kisiasa Tunisia
Dec 03, 2021 01:03Licha ya mgogoro wa kisiasa wa Tunisia kuendela kwa miezi kadhaa sambamba na kufanyika juhudi za kujaribu kuumaliza, lakini juhudi hizo zimeshindwa kuzaa matunda.
-
Financial Times: Fungate ya Rais Kais Saied wa Tunisia inaelekea ukingoni
Nov 16, 2021 03:39Gazeti la Financial Time la Uingereza limeripoti kuwa wataalamu wanasema fungate ya Rais wa Tunisia itamalizika hivi karibuni kutokana na mashaka ya kushindwa kwake kupata suluhisho la haraka la mgogoro wa kiuchumi unaoisumbua nchi hiyo licha ya kuwa na uungaji mkono wa kiasi fulani kwa sasa.
-
Serikali ya Tunisia yaamuru kukamatwa rais wa zamani wa nchi hiyo kutokana na misimamo yake
Nov 05, 2021 07:50Maafisa wa serikali ya Tunisia wametoa amri ya kukamatwa rais wa zamani wa nchi hiyo Moncef Marzouki kutokana na misimamo yake inayopinga maamuzi yaliyochukuliwa na kiongozi wa sasa wa nchi hiyo, Kais Saied.
-
Moncef Marzouki: Saeid auzuliwe na kushtakiwa kwa kuangamiza utawala wa Sheria Tunisia
Oct 28, 2021 06:34Rais wa zamani wa Tunisia amewataka wananchi wa nchi hiyo wafanye maandamano ya kupinga maamuzi ya rais wa sasa wa nchi hiyo, Kais Saied, kumuondoa madarakani na kumfikisha mahakamani kwa tuhuma za kuangamiza serikali, mapinduzi ya wananchi na utawala wa sheria.
-
Rais wa Tunisia aahidi kuanzisha mazungumzo ya kitaifa nchini
Oct 22, 2021 06:05Rais Kais Saied wa Tunisia amesema kuwa karibuni ataanzisha mazungumzo ya kitaifa kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho katiba na mfumo wa kisiasa wa nchi hiyo.
-
Kuapishwa Waziri Mkuu mpya wa Tunisia
Oct 12, 2021 23:00Hatimaye baada ya vuta nikuvute ya kisiasa ya majuma kadhaa nchini Tunisia, serikali mpya ya nchi hiyo imeapishwa ikiongozwa na mwanamama Najla Bouden Romdhane.
-
Maelfu ya watu waandamana nchini Tunisia kutaka Rais Kais Saied ajiuzulu
Oct 10, 2021 23:01Maelfu ya watu wamemiminika kwenye mitaa ya mji mkuu wa Tunisia, Tunis katika maandamano mapya ya kumtaka rais wa nchi hiyo Kais Saied ajiuzulu.