-
Magaidi 120 wauawa kusini magharibi mwa Niger
Feb 22, 2020 03:53Wizara ya Ulinzi ya Niger imetangaza habari ya kuuawa magaidi 120 na kutekwa magari na vifaa vyao vya kutengenezea mabomu katika operesheni maalumu iliyofanywa na wanajeshi wa nchi hiyo katika eneo la kusini magharibi mwa nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.
-
Makundi yenye silaha yaendelea kumwaga damu Nigeria
Feb 18, 2020 04:35Watu waliojizatiti kwa silaha wameshambulia jimbo la Delta kusini mwa Nigeria na kuua watu 10. Mashuhuda wanasema waliotekeleza ukatili huo walikuwa wamevalia magwanda ya kijeshi.
-
Jeshi la Syria: Tutang'oa mizizi ya ugaidi wa ukufurishaji
Feb 17, 2020 22:09Jeshi la Syria sambamba na kuashiria kukombolewa makumi ya vijiji na miji ya kaskazini magharibi mwa nchi hiyo, limesisitiza kuendeleza mapambano yake kwa ajili ya kuung'oa ugaidi wa ukufurishaji.
-
Wakazi wa mkoa wa al Hasakah Syria waanzisha mapambano ya kuwafukuza wanajeshi wa Marekani
Feb 13, 2020 23:10Gavana wa mkoa wa al Hasakah nchini Syria amezitaja hatua za mapambano zilizochukuliwa na raia wa vijiji kadhaa vya mkoa huo dhidi ya wanajeshi wa Marekani kuwa ni kuanza kwa mapambano ya wananchi ya kuwafukuza wanajeshi vamizi wa Marekani huko Syria.
-
Rais wa Mali: Serikali iko tayari kuzungumza na makundi ya kigaidi
Feb 11, 2020 08:42Rais Ibrahim Boubacar Keita wa Mali amesema serikali yake iko tayari kukutana na kufanya mazungumzo na makundi ya kigaidi kwa shabaha ya kumaliza jinamizi la ugaidi ambalo mbali na kuchochea mapigano ya kikabila, pia limeifanya nchi hiyo ishindwe kutawalika na kustawi.
-
Rouhani: Vikwazo vya madawa vya Marekani dhidi ya taifa la Iran ni kitendo cha kigaidi
Feb 06, 2020 04:06Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran vinakiuka sheria na kanuni za kimataifa na maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kuongeza kuwa, vikwazo hivyo ni hatua ya kigaidi.
-
Syria: Ugaidi wa kiuchumi ni mwendelezo wa ugaidi wa kifizikia
Jan 30, 2020 09:59Mwakilishi wa Kudumu wa Syria katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa ugaidi wa kiuchumi ni mwendelezo wa hatua zilizo dhidi ya ubinaadamu za kuyatumia makundi ya kigaidi.
-
Matokeo hasi ya chokochoko za Marekani Asia Magharibi
Jan 23, 2020 23:22Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa hatua na chokochoko za kijeshi zinazofanywa na Marekani katika eneo la Asia Magharibi, ndio chanzo cha machafuko ndani ya eneo hilo na ameongeza kuwa, uthibitisho wa mwisho wa jambo hilo ni kumuua kigaidi Luteni Qassem Soleimani katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Baghadad, Iraq.
-
Ugaidi, vikwazo na mauaji ya kigaidi, stratijia tatu za Magharibi dhidi ya kambi ya muqawama
Jan 19, 2020 07:27Wizara ya Fedha ya Uingereza katika hatua yake ya uhasama, imeliweka kikamilifu jina la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon katika orodha yake ya taasisi ambazo kwa mtazamo wa London ni za kigaidi.
-
Rais Rouhani wa Iran: Wamarekani wahitimishe hatua zao ghalati
Jan 10, 2020 08:33Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa anataraji kwamba Wamarekani watahitimisha hatua zao ghalati, lakini iwapo watatekeleza hatua nyingine iliyo dhidi ya maslahi ya Iran, basi watapata jibu kali mkabala.