-
Iran: Saudia haiwezi kuficha rekodi yake ya ugaidi kwa kuichafua Jamhuri ya Kiislamu
Mar 20, 2018 12:30Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekanusha vikali madai mapya yaliyotolewa na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia kwamba Tehran imewaficha wakuu wa magenge ya kigaidi na kusisitiza kuwa, Riyadh haiwezi kuficha wala kupotosha historia na rekodi yake ya kuunga mkono na kufadhili ugaidi, kwa kueneza urongo na propaganda dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Syria yaitaka UN kuchukua hatua dhidi ya waungaji mkono ugaidi
Feb 22, 2018 00:59Serikali ya Syria imeuandikia barua Umoja wa Mataifa ikizungumzia ongezeko la mauaji ya kigaidi yanayofanywa dhidi ya raia wa Damascus na vitongoji vyake na kuutaka umoja huo kuchukua hatua dhidi ya nchi zinazoyasaidia na kuyafadhili makundi ya kigaidi.
-
Serikali ya Misri yamuweka mpinzani wa al Sisi katika orodha ya magaidi!
Feb 20, 2018 23:42Serikali ya Misri imemuweka kiongozi wa chama cha upinzani cha "Misri Imara" na wanachama wengine 15 wa chama hicho katika orodha ya magaidi.
-
Undumakuwili wa Wamarekani kuhusu ugaidi; bahari ya damu Stoneman Douglas, ni ufyatuaji risasi au ni ugaidi?
Feb 17, 2018 02:33The Anti-Defamation League ambayo ni taasisi ya kulinda haki za raia wa Marekani imesema kuwa, kijana katili aliyefanya mauaji ya kutisha katika shule ya Stoneman Douglas huko Parkland, Florida alikuwa mwanachama wa genge moja la Wazungu wenye misimamo mikali.
-
Haniyeh: Hatua ya Marekani ya kuliweka jina langu katika orodha nyeusi ni fakhari kwangu
Feb 02, 2018 11:37Ismail Haniyeh, Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema kuwa, uamuzi wa Marekani ya kuliweka jina lake katika orodha nyeusi, ni ishara ya fakhari kwake.
-
Makundi ya kitakfiri yahudumia malengo ya utawala wa Kizayuni
Jan 27, 2018 00:44Duru za habari zimefichua sura mpya na pana zaidi ya ushirikiano wa utawala wa Kizayuni wa Israel na makundi ya kitakfiri na kigaidi huko Syria na kutangaza kwamba, utawala huo umeunda kundi la kigaidi kwa ajili ya kuusaidia utawala huo katika maeneo unayoyakalia kwa mabavu ya Golan.
-
Hassan Nasrullah: Inasikitisha kuona bado kuna nchi zinaendeleza uhusiano na Israel
Jan 20, 2018 01:12Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah nchini Lebanon sambamba na kuzitaka nchi zote za dunia kujiepusha kufanya uhusiano na utawala katili wa Israel, ameonyesha masikitiko kwamba bado kuna nchi zinaendeleza uhusiano na utawala huo.
-
Juhudi za Ulaya kuzidisha uingiliaji wa kijeshi barani Afrika
Jan 19, 2018 09:51Ikiwa ni katika mkondo wa kudumisha uingiliaji wa nchi za Magharibi barani Afrika, serikali za Italia na Uingereza zimeazimia kuimarisha uwepo wao wa kijeshi katika baadhi ya nchi za bara hilo.
-
Maulamaa wa Pakistan watoa fatua ya kuharamisha kujiripua
Jan 17, 2018 00:47Mamia ya maulamaa wa Kiislamu nchini Pakistan wametoa fatua ya kuharamisha mashambulizi ya kujitoa muhanga, katika hali ambayo nchi hiyo inaendelea kukabiliwa na hujuma za magenge ya kigaidi.
-
Larijani: Iran na Pakistan zimesimama kidete kukabiliana na matatizo ya ugaidi kwa busara
Jan 16, 2018 01:05Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Iran na Pakistan zikitumia busara na werevu zimeweza kusimama kidete na kukabiliana vyema na matatizo mbalimbali yanayosababishwa na ugaidi.