-
Iran: Marekani ikijitoa katika JCPOA, tutaanzisha tena shughuli za nyuklia kwa kiwango cha kisasa zaidi
Apr 23, 2018 00:09Waziri wa Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, chaguo kuu la Iran endapo Marekani itajitoa katika makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA ni kuanzisha tena shughuli za nyuklia za taifa hili zenye malengo ya amani lakini kwa kiwango cha juu na cha kisasa zaidi.
-
Trump aendelea kukosolewa, bunge la Ujerumani lalaani shambulizi la Marekani dhidi ya Syria
Apr 21, 2018 23:16Kinyume na serikali ya Ujerumani, bunge la nchi hiyo limelaani shambulizi la Marekani, Ufaransa na Uingereza dhidi ya Syria na kulitaja kuwa ni kukiuka sheria na mikataba ya kimataifa.
-
Kukiri Ujerumani nafasi muhimu ya Russia ulimwenguni
Apr 02, 2018 09:32Heiko Maas, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, amesema kuwa nchi yake inakaribisha mazungumzo na Russia kwa ajili ya kukomesha mgogoro uliojitokeza hivi sasa baina ya Moscow na nchi za Magharibi zikiongozwa na Uingereza.
-
Ujerumani yasisitizia umuhimu wa kufanya mazungumzo na Russia
Apr 01, 2018 12:44Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani amesisitiza kuwa kuna umuhimu wa kufanya mazungumzo na Russia.
-
Timuatimua ya wanadiplomasia kati ya Russia na madola ya Magharibi yaendelea, Ujerumani yakaribisha mazungumzo
Mar 31, 2018 03:01Huku hali ya kutimua wanadiplomasia kati ya madola ya Magharibi na Russia ikiendelea, serikali ya Ujerumani imesema kuwa inakaribisha mazungumzo na Moscow.
-
Kiongozi wa eneo la Catalani atiwa mbaroni Ujerumani
Mar 25, 2018 09:50Kiongozi wa zamani wa eneo la Catalani linalotaka kujitenga na Uhispania, Carles Puigdemont ametiwa mbaroni leo na polisi nchini Ujerumani kufuatia waranti wa kimataifa uliotolewa na Uhispania.
-
Sisitizo la viongozi wa Uingereza, Ujerumani na Ufaransa la kufungamana na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA
Mar 23, 2018 03:27Viongozi wa Uingereza, Ujerumani na Ufaransa walikutana jana Alkhamisi pambizoni mwa mkutano wa viongozi wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels Ubelgiji ambapo pamoja na mambo mengine walizungumzia suala la makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA).
-
Msikiti mwingine washambuliwa kwa bomu nchini Ujerumani
Mar 20, 2018 12:23Msikiti mmoja katika mji wa Ulm, kusini mwa Ujerumani umeshambuliwa kwa bomu na watu wasiojulikana, chini ya wiki mbili baada ya msikiti mwingine kuteketezwa kwa moto katika mji mkuu wa nchi hiyo ya Ulaya, Berlin.
-
Iran haifanyi mazungumzo tena kuhusu mapatano ya nyuklia ya JCPOA
Mar 16, 2018 03:20Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesisitiza kuwa katu haitakubali kufanyika mazungumzo mapya kuhusu mapatano ya nyuklia baina yake na mdola sita makubwa duniani.
-
Wenye chuki dhidi ya Uislamu wachoma moto msikiti nchini Ujerumani
Mar 11, 2018 12:58Katika kile kinachoonekana ni muendelezo wa matukio ya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu barani Ulaya, wavamizi wasiojulikana wameuteketeza moto msikiti mmoja katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin.