-
Lukashenko: Belarus itaungana na Russia katika vita vya Ukraine ikishambuliwa
Feb 16, 2023 23:19Rais Alexander Lukashenko wa Belarus ameonya kuwa, iwapo nchi hiyo itashambuliwa, basi haitakuwa na budi kuungana na Russia katika vita dhidi ya Ukraine.
-
Katibu Mkuu wa UN: Dunia inaelekea katika vita vikubwa zaidi
Feb 07, 2023 02:56Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametahadharisha kwamba, hatua zozote za kuchochea mgogoro wa Russia na Ukraine huenda zikaitumbukiza dunia katika vita vipana na vikubwa zaidi.
-
Russia: Tutatumia silaha zozote iwapo Ukraine itaishambulia Crimea
Feb 05, 2023 06:54Russia imetoa onyo kali na kusisitiza kuwa, shambulio lolote la Ukraine dhidi ya eneo la Crimea litaiepelekea Moscow kutumia 'silaha za aina yoyote' kujibu mapigo na kujilinda.
-
Onyo la Russia kwa Netanyahu kuhusu msaada wa silaha kwa Ukraine
Feb 03, 2023 22:44Russia imeuonya vikali utawala haramu wa Israel baada ya Waziri Mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu kutangaza Jumatano usiku kwamba anachunguza suala la kutuma msaada wa kijeshi wa utawala huo nchini Ukraine.
-
Radiamali ya Iran kwa vitendo vya uhasama vya utawala wa Kizayuni na msimamo wa kichochezi wa Ukraine
Feb 03, 2023 04:47Amir Saeed Irwani, Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa, siku ya Jumatano, akizungumzia shambulio la kigaidi kwenye kiwanda cha Wizara ya Ulinzi huko Isfahan, amesema katika barua kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na pia kwa mwenyekiti wa kiduru wa Baraza la Usalama kwamba uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa utawala wa Kizayuni umehusika na tukio hilo la kigaidi.
-
Rais wa Argentina: Nchi za Amerika ya Latini hazitaipatia silaha Ukraine
Jan 29, 2023 04:13Rais wa Argentina amesema kuwa nchi za Amerika ya Latini, kinyume na nchi za Magharibi, hazina mpango wa kuipatia Ukraine silaha kwa kisingizio cha vita vinavyoendelea nchini humo.
-
Israel yaufyata baada ya onyo la Russia, yakataa ombi la US la kuipa Ukraine makombora
Jan 26, 2023 23:18Utawala haramu wa Israel umepinga ombi la Marekani la kuutaka uipe Ukraine makombora na silaha nyinginezo, baada ya Russia kuonya vikali dhidi ya kupewa Kiev misaada ya kijeshi na zana za vita.
-
Uungaji mkono wa Marekani kwa mashambulizi ya Ukraine dhidi ya Crimea; jitihada za kujaribu kuchochea vita
Jan 21, 2023 22:54Sabrina Singh, Naibu Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) ameeleza kuwa, eti Marekani inakitambua kisiwa cha Crimea kuwa sehemu ya ardhi ya Ukraine na kwamba inaunga mkono oparesheni za Kyiv za kukikomboa kisiwa hicho.
-
Balozi: Marekani inashajiisha vitendo vya kigaidi dhidi ya Russia
Jan 19, 2023 07:01Balozi wa Russia nchini Marekani ameonya vikali dhidi ya mashambulizi tarajiwa ya Ukraine katika Peninsula ya Crimea na kusisitiza kuwa, Moscow itajibu mapigo baada ya Washington kudokeza kuwa huenda Kiev ikatumia silaha za Magharibi kulishambulia eneo hilo.
-
Russia yadhibiti mji wa kistratajia wa Soledar, Donbass
Jan 14, 2023 00:20Wizara ya Ulinzi wa Russia imesema vikosi vya jeshi la nchi hiyo vimefanikiwa kudhibiti kikamilifu mji wa kistratajia wa Soledar, ulioko katika eneo la Donbass. Eneo la Donbass lenye raia wenye asili ya Russia liko mashariki mwa Ukraine na tangu 2014 Warusi walianzisha jamhuri mbili, Donetsk na Luhansk, na kuunda serikali zilizojitenga na serikali ya Ukraine.