-
Vikwazo vyenye wigo mpana vya Wamagharibi dhidi ya Russia
Feb 25, 2022 10:03Baada ya Russia kuchukua uamuzi wa kuishambuulia kijeshi Ukraine, kambi ya magharibi imeonyesha radiamali katika fremu ya kuiwekea vikwazo Moscow ambapo kabla ya hapo madola hayo yalikuwa yameahidi kuchukua uamuzi huo.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa: Hatua za kichochezi za NATO zimeifanya hali katika eneo iwe tata
Feb 25, 2022 09:39Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehrah amesema, hatua za kichochezi zilizochukuliwa na shirika la kijeshi la NATO kwa uongozi wa Marekani zimetatanisha hali ya mambo katika eneo; na si hasha zikaifanya iwe tata zaidi.
-
Serikali ya Iran: Vita si suluhisho la mgogoro wowote ule
Feb 25, 2022 03:26Msemaji wa serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, vita si suluhisho la tatizo lolote lile. Amesema hayo ikiwa ni kutangaza msimamo wa serikali ya Iran kuhusu vita baina ya Russia na Ukraine huko mashariki mwa Ulaya.
-
Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran: Mgogoro wa Ukraine umesababishwa na uchochezi wa NATO
Feb 24, 2022 11:39Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran ametuma ujumbe katika mtandao wa kijamii wa Twitter akisisitiza kuwa chanzo cha mgogoro wa Ukraine ni hatua za kichochezi za Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO).
-
Oparesheni ya kijeshi ya Russia nchini Ukraine, sababu na matokeo yake
Feb 24, 2022 07:30Rais Vladimir Putin wa Russia mapema Alhamisi amehutubia taifa katika televisheni na kutangaza kuwa, vikosi vya nchi yake vimeanza oparesheni maalumu ya kijeshi katika eneo la Donbass ambalo limetangaza kujitenga na Ukraine. Punde baada ya kutangaza oparesheni hiyo ya kijeshi, Putin ametaka kusitishwe 'muundo wa kijeshi' Ukraine na kuitaka nchi hiyo iweke chini silaha zake.
-
Iran: Uingiliaji wa US, NATO umeshadidisha mgogoro wa Ukraine
Feb 22, 2022 23:12Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekosoa vikali chokochoko za Marekani na shirika la kijeshi la NATO katika mgogoro wa Ukraine na kusisitiza kuwa, uingiliaji huo umeshadidisha taharuki mashariki mwa nchi hiyo jirani na Russia.
-
Putin, Macron na Zelensky wajadili mgogoro wa eneo la mashariki ya Ukraine
Feb 21, 2022 04:35Ikulu ya rais wa Ufaransa ya Élysée imetangaza kuwa, baada ya kuzungumza na Rais Vladimir Putin wa Russia, rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron amezungumza kwa njia ya simu pia na mwenzake wa Ukraine Volodymyr Zelensky kumjulisha kuhusu mazungumzo yao.
-
Putin asisitiza, Russia haina nia ya kuingia vitani na Ukraine
Feb 16, 2022 23:18Rais Vladimir Putin wa Rassia aliuambia mkutano wa waandishi wa habari siku ya Jumanne baada ya kukutana na Kansela wa Ujerumani, Olaf Scholz, huko Kremlin kwamba ametoa wito kwa nchi za Magharibi kujiepusha kupeleka silaha za kivita kwenye mipaka ya Russia na kwamba zinapaswa kusitisha upanuzi wa shirika la NATO upande wa Mashariki.
-
Russia: Hatutaki vita barani Ulaya wala Ukraine
Feb 16, 2022 03:40Rais wa Russia amesema kuwa nchi yake haitaki kutokee vita barani Ulaya wala nchini Ukraine na ni kwa sababu hiyo ndio maana imetoa pendekezo la kudhaminiwa usalama wa eneo hilo.
-
Zelensky adai: Russia itaishambulia Ukraine siku ya Jumatano
Feb 14, 2022 23:31Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amedai kuwa Russia itatekeleza shambulio dhidi ya Kiev siku ya Jumatano.