-
Kuendelea mashambulizi na jinai za Wazayuni kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi
Feb 25, 2025 02:28wanajeshi wa utawala wa Kizayuni kwa mara nyingine tena wameshambulia maeneo mbalimbali katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Afrika Kusini: Usitishaji vita Gaza sharti ulete amani ya kudumu
Feb 21, 2025 02:50Rais wa Afrika Kusini amesema usitishaji wa mapigano katika Ukanda wa Gaza unapasa kuleta uadilifu na amani ya kudumu katika eneo hilo.
-
Matakwa ya mashirika ya haki za binadamu ya kutopatiwa Israel vipuri vya ndege za kivita za F-35
Feb 21, 2025 02:23Muungano wa Kimataifa wa mashirika 232 ya kutetea haki za binadamu umezitaka nchi mbalimbali zinazohusika katika uundaji za ndege za kivita aina ya F-35 kuacha kuipatia Israel vipuri vya ndege hizo.
-
Errea nayo yabatilisha mkataba wake na Shirikisho la Soka la utawala wa Kizayuni
Feb 20, 2025 07:38Kampuni nyingine ya udhamini wa vifaa vya michezo ya Ulaya imefuta mkataba wake na Shirikisho la Soka la utawala wa Kizayuni wa Israel na hivyo kutoa pigo jingine kwa utawala huo haramu.
-
Kuendelea kushtakiwa jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina
Feb 20, 2025 02:34Gideon Sa’ar Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa utawala vamizi wa Israel ameshtakiwa kwa kutenda jinai za kivita katika Ukanda wa Gaza.
-
Ripoti: Marekani na Ufaransa zinataka askari mamluki wapelekwe kusini mwa Lebanon
Feb 19, 2025 06:54Marekani na Ufaransa zimeripotiwa kuwa zimependekeza mamluki wanaoitwa wakandarasi binafsi wapelekwe kusini mwa Lebanon katika jitihada za kuushawishi utawala wa Kizayuni wa Israel uondoe kikamilifu majeshi yake nchini humo.
-
Jumuiya ya mateka wa Palestina: Mateka 58 wamekufa shahidi katika muda wa miezi sita iliyopita
Feb 18, 2025 13:43Mkuu wa Jumuiya ya mateka wa Palestina amesema, kuna hatari nyingi zinatishia maisha ya mateka wa Kipalestina, na kwamba katika kipindi cha miezi sita iliyopita, mateka 58 wamekufa shahidi wakiwa ndani ya jela za utawala wa Kizayuni.
-
Jeshi la Israel laendelea kukalia maeneo ya ardhi ya Lebanon licha ya muhula wa kuondoka kumalizika
Feb 18, 2025 13:42Muhula wa mwisho uliokuwa umetolewa kwa askari wote wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kuondoka kusini mwa Lebanon chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa kati ya utawala huo na harakati ya Hizbullah ulimalizika leo Jumanne, huku Israel ikitangaza kuwa itaendelea kubaki katika "maeneo matano ya kimkakati" ya ardhi ya nchi hiyo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Ulimwengu wa Kiislamu uchukue msimamo thabiti kuiunga mkono Palestina
Feb 17, 2025 07:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekumbusha kuhusu uungaji mkono ulioonyeshwa na nchi za Kiarabu na Kiislamu kwa hatua ya maana iliyochukuliwa na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC ya kukabiliana na mpango wa pamoja wa Marekani na utawala wa Kizayuni unaolenga kuifuta Palestina, na akabainisha kwamba: "Ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kuiunga mkono Palestina kwa msimamo thabiti."
-
AU yataka Israel ishtakiwe kwa mauaji ya kimbari ya Ghaza na kutoshirikiana wala kuanzisha uhusiano nayo
Feb 17, 2025 07:09Wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika AU wametoa wito, mwishoni mwa mkutano wa 38 wa kilele uliofanyika mjini Addis Ababa, wa kusitishwa ushirikiano na kutoanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel.