-
Kukiri Israel juu ya kutekeleza ufutaji kizazi katika Ukanda wa Gaza
Dec 04, 2024 02:45Waziri wa zamani wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel Moshe Yaalon amesisitiza kwa mara nyingiine tena kwamba, utawala huo unafanya "maangamizi ya kizazi" kaskazini ya Ukanda wa Gaza, akimshutumu Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kwa kuielekeza Israel kwenye "uharibifu."
-
Libya yataka kufutwa uanachama wa utawala wa Israel katika Umoja wa Mataifa
Dec 03, 2024 12:15Libya imetaka kufutwa uanachama wa utawala wa Kizayuni katika Umoja wa Mataifa na kuhuishwa sura ya saba ya Hati ya Baraza la Usalama dhidi ya utawala huo unaotekeleza mauaji ya kimbari.
-
HAMAS: Mateka Wazayuni 33 wameuawa kutokana na "ukichwangumu wa mhalifu wa kivita Netanyahu"
Dec 03, 2024 03:36Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, mateka Wazayuni 33 wanaoshikiliwa na harakati hiyo katika Ukanda wa Ghaza wameuawa tangu utawala ghasibu wa Israel ulipoanzisha vita vinavyoendelea kwa takriban miezi 14 sasa dhidi ya eneo hilo uliloliwekea mzingiro.
-
Mienendo ya kindumakuwili ya Ulaya kuhusu waranti ya kukamatwa watawala wa Israel
Nov 29, 2024 15:27Hatua ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ya kutoa waranti ya kukamatwa Benjamin Netanyahu na Yoav Gallant, Waziri Mkuu na waziri wa zamani wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel imeakisiwa pakubwa kimataifa kwa kutilia maanani umuhimu wake na pia kutokana na kutochukuliwa hatua kama hiyo huko nyuma dhidi ya viongozi wa utawala huo ghasibu.
-
Israel yakiuka makubaliano ya kusitisha vita Lebanon, yaendelea kuua Wapalestina Ghaza
Nov 29, 2024 11:42Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limefanya mashambulizi mapya dhidi ya Lebanon kinyume na makubaliano ya kusitisha mapigano liliyofikia na harakati ya Muqawama ya Hizbullah; na wakati huohuo limeshadidisha mashambulizi yake ya kinyama ya anga katika Ukanda wa Ghaza.
-
Magaidi wa kitakfiri 400 waangamizwa Syria
Nov 29, 2024 07:14Kituo cha Russia cha Hmeimim cha Maridhiano ya Kitaifa nchini Syria kimetangaza kuwa magaidi wa kitakfiri wa 400 wa kundi la Jabhatu-Nusra wameangamizwa baada ya kushambulia makao makuu ya jeshi la Syria huko Idlib na Aleppo.
-
UK: Tutamtia mbaroni Netanyahu akikanyaga ardhi ya Uingereeza
Nov 29, 2024 02:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza amedai kuwa nchi yake inaheshimu uamumizi wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC wa kutiwa mbaroni waziri mkuu wa Israel, Banjamin Netanyahu na kusisitiza kuwa, kama Netanyahu atakanyaga ardhi ya Uingereza, basi London itamtia mbaroni.
-
Gazeti la Kiebrania: Utawala wa Kizayuni umepata hasara nyingi katika vita na Hizbullah
Nov 28, 2024 03:30Kufuatia kutangazwa usitishaji vita kusini mwa Lebanon, vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa vita hivyo vimeutia hasara nyingi na kuusababishia uharibifu mkubwa utawala huo wa Kizayuni.
-
61% ya Wazayuni: Netanyahu amegonga mwamba, Israel haijashinda vita dhidi ya Hizbullah
Nov 27, 2024 12:41Kwa mujibu wa uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa na jeshi la utawala haramu wa Israel ndani ya jamii ya Wazayuni, asilimia 61 miongoni mwao wanaamini kuwa utawala huo haujapata ushindi katika vita dhidi ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Licha ya kutolewa waranti wa kumkamata, Gallant apanga safari ya kutembelea Marekani
Nov 26, 2024 06:42Waziri wa zamani wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel Yoav Gallant anapanga kusafiri kuelekea Marekani licha ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kutoa hati ya kumkamata kwa kuhusika na jinai za kivita katika Ukanda wa Ghaza.