-
Kuendelea “mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa” mhimili wa siasa za uingiliaji mambo wa Marekani dhidi ya Venezuela
Aug 18, 2020 21:56Katika hali ambayo hadi sasa siasa za “mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa” za Marekani dhidi ya Venezuela zimefeli na kugonga mwamba, Robert Charles O’Brein, mshauri wa usalama wa taifa wa White House amesisitiza kuwa, mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa utakuwa mhimili wa harakati za Washington dhidi ya Venezuela.
-
Sisitizo la kuongezwa ushirikiano wa Iran na Venezuela na ghadhabu za Washington kwa hilo
Aug 11, 2020 22:01Katika miaka ya hivi karibuni Iran na Venezuela zimeandamwa na vikwazo vya kiuchumi na kisiasa vya Marekani na viongozi wa White House wamefanya juhudi kubwa kutumia nyenzo mbalimbali ili wazifanye nchi mbili hizi zisalimu amri na kufuata siasa za Washington.
-
Kuendelea ushirikiano wa Iran na Venezuela licha ya vitisho vya Marekani
Aug 06, 2020 01:57Ushirikiano wa kibiashara na kisiasa wa Iran na Venezuela unaendelea kuimarika licha ya kuwepo vitisho na vikwazo vya Marekani. Kutumwa meli za mafuta za Iran nchini Venezuela mwezi uliopita ilikuwa hatua ya kwanza katika uwanja huo na sasa Iran imechukua hatua nyingine ya kufungua duka kubwa la bidhaa zake katika mki mkuu wa nchi hiyo, Caracas.
-
Tishio jipya la Donald Trump dhidi ya Venezuela
Jul 12, 2020 08:05Katika hali ambayo siasa za chuki na hasama za Marekani dhidi ya Venezuela hadi sasa zimeshindwa na kugonga mwamba, Rais Donald Trump kwa mara nyingine tena ametoa matamshi ya vitisho kwa kusema: Kuna mambo yatatokea kuhusiana na Venezuela.
-
Vikwazo vipya vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Venezuela na jibu kali la Rais Maduro
Jul 01, 2020 05:53Tangu mgogoro wa kisiasa wa Venezuela uliposhadidi, Umoja wa Ulaya umekuwa pamoja na Marekani dhidi ya Rais Nicolas Maduro wa nchi hiyo.
-
Meli ya chakula ya Iran yafika kwenye eneo la majini la Venezuela licha ya vikwazo vya Marekani
Jun 22, 2020 03:17Meli ya Iran yenye chakula kwa ajili ya wananchi wa Venezuela imefika kwenye eneo la majini la nchi hiyo ya Amerika ya Latini licha ya Marekani kuiwekea vikwazo nchi hiyo na kuifungia njia zote. Hadi tunapokea habari hii, meli hiyo ilikuwa imekaribia kufika kwenye bandari ya Guaira.
-
Ndege ya Iran iliyobeba msaada wa COVID-19 yawasili Venezuela
Jun 09, 2020 03:34Serikali ya Venezuela imesema ndege ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iliyobeba msaada wa dharura kwa ajili ya waathirika wa ugonjwa wa COVID-19 iliwasili nchini humo jana Jumatatu.
-
Kiongozi Muadhamu awashukuru wafanyakazi wa meli za mafuta za Iran zilizotumwa Venezuela
Jun 08, 2020 23:10Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma ujumbe kufuatia harakati ya Kijihadi ya makamanda na wafanyakazi wa meli za mafuta za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambazo zilibeba shehena za bidhaa za petroli na kuzifikisha nchini Venezuela.
-
Marekani na mwendelezo wa vikwazo vya mafuta dhidi ya Venezuela
Jun 03, 2020 21:59Marekani imeapa kuzidisha vikwazo na kuishinikiza zaidi serikali ya Venezuela licha ya kufeli siasa zake za vikwazo dhidi ya nchi hiyo. Katika uwanja huu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo amesema Washington imeyawekea vikwazo makampuni mengine manne ya mafuta ya Venezuela na ameitaka jamii ya kimataifa izidishe mashinikizo dhidi ya serikali ya Caracas hadi itakapoondolewa madarakani.
-
Cuba na Venezuala zalaani ukatili wa polisi wa Marekani dhidi ya watu weusi
May 30, 2020 23:52Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Cuba na Venezula wamelaani vikali ukatili wa polisi wa Marekani dhidi ya Wamarekani weusi pamoja na ujumbe wa kuchochea utumiaji mabavu alioutoa Rais Donald Trump.