-
Meja Jenerali Salami: Mashinikizo ya maadui hayawezi kuipigisha magoti Iran
Sep 12, 2019 22:08Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) amesema kuwa, taifa la Iran limedhihirisha kuwa lina nguvu kuliko vikwazo na katu haliwezi kupigishwa magoti na mashinikizo ya maadui.
-
Iran: Hatufanyi mazungumzo na Marekani iwapo wanaendeleza ugaidi wa kiuchumi
Sep 11, 2019 02:59Mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema ni jambo lisilowezekana kwa Jamhuri ya Kiislamu kufanya mazungumzo na Marekani madhali serikali ya Washington inaendeleza ugaidi wa kiuchumi na kuliwekea vikwazo taifa hili.
-
Ukosoaji wa Russia kwa nafasi haribifu ya Magharibi katika Ghuba ya Uajemi
Sep 10, 2019 22:01Baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kutangaza kuiondoa nchi hiyo katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) mnamo tarehe 8 Mei mwaka uliopita, alianza kutekeleza mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Iran.
-
Misri yataka kuondolewa vikwazo vya Marekani dhidi ya Sudan
Sep 10, 2019 02:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri ametaka kuondolewa vikwazo vya Marekani dhidi ya Sudan, akisisitiza kuwa serikali mpya ya kiraia ya Khartoum inahitaji uungaji mkono wa jamii ya kimataifa na sio kuendelea kuwekewa vikwazo na kutengwa.
-
Hatua mpya za Marekani dhidi ya JCPOA; kupinga mpango wa Ufaransa na kutangaza vikwazo vipya dhidi ya Iran
Sep 05, 2019 21:55Rais Donald Trump wa Marekani alisikika mara kadha wa kadha akiyakosoa vikali makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, na hatimaye mnamo tarehe 8 Mei, 2018 akatangaza rasmi kujitoa nchi yake katika makubaliano hayo. Kilichofuata baada ya hapo, ilikuwa ni kutekelezwa na serikali ya Trump katika awamu mbili tofauti vikwazo vikali dhidi ya Iran sambamba na kupinga mpango wowote wa kuyalinda makubaliano hayo ya nyuklia.
-
Vikwazo vipya vya Marekani na woga wa Washington kuhusu nguvu za makombora za Iran
Aug 29, 2019 23:12Katika kipindi hiki cha utawala wa Donald Trump, Marekani imeliwekea taifa la Iran vikwazo vikubwa mno baada ya Washington kujitoa bila sababu katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Wito wa Umoja wa Mataifa kwa Marekani wa kutimiza wajibu wake wa kidiplomasia kuhusiana na Zarif
Aug 08, 2019 22:38Kuwekewa vikwazo Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif na serikali ya Trump kumetafsiriwa na wengi kama ishara ya kuemewa na kuzidiwa nguvu Marekani na diplomasia imara na amilifu ya Tehran. Na kitendo hicho kimeibua hisia kali na ukosoaji mkubwa dhidi ya Washington duniani.
-
Taathira hasi za siasa za serikali ya Marekani dhidi ya Iran kwa uhusiano kati ya Washington na waitifaki wake wa Ulaya
Aug 08, 2019 22:15Mkuu wa zamani wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) amesisitiza kuwa siasa zinazotekelezwa na serikali ya nchi hiyo dhidi ya Iran zimekuwa na taathira hasi kwa uhusiano kati ya Washington na waitifaki wake wa Ulaya.
-
Larijani: Zarif ni nembo ya uchapakazi na diplomasia makini ya Iran
Aug 05, 2019 22:06Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amemtaja Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa ni nembo ya uchapakazi na diplomasia makini ya Iran.
-
Dakta Zarif: Nimewekewa vikwazo baada ya kukataa pendekezo la kukutana na Trump
Aug 05, 2019 07:20Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria safari yake ya mwezi uliopita huko New York na kusema kuwa, "niliambiwa nitawekewa vikwazo katika kipindi cha wiki mbili zijazo isipokuwa kama nitakubali kukutana na Rais Donald Trump wa Marekani."