-
UN yataka kufunguliwa kesi ya jinai zinazofanywa dhidi ya Waislamu Myanmar
Oct 24, 2019 23:21Maafisa wawili wa Umoja wa Mataifa wametoa wito wa kufunguliwa kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ili kushughulikia jinai zinazofanywa na jeshi la Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya katika jimbo la Rakhine nchini humo.
-
India yazidisha hatua kali za usalama kabla ya kuhitimishwa kesi ya Msikiti wa Babri
Oct 15, 2019 00:35Serikali ya India imezidisha hatua kali za usalama katika mji wa Ayodhya, jimbo la Uttar Pradesh huko kaskazini mwa nchi hiyo kabla ya kutolewa uamuzi muhimu sana wa Mahaka Kuu ya nchi hiyo juu ya mzozo wa eneo la Msikiti wa Babri linalogombaniwa baina ya Waislamu na Wahindu.
-
Waislamu Tanzania wajiandaa kufanya Maulidi ya Mtume Muhammad SAW kwa hamasa kubwa zaidi mwaka huu + Sauti
Oct 07, 2019 06:03Viongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) wametoa ufafanuzi kuhusu maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa yanavyoendelea jijini Mwanza na wamejipanga kufanya shughuli mbalimbali za kijamii kuelekea maadhimisho hayo ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad SAW. Ammar Dachi na taarifa zaidi kutoka Dar es Salaam...
-
Zarif: Iwapo Marekani inataka mazungumzo na Iran lazima itekeleze ahadi zake
Sep 29, 2019 03:46Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Iran haitaacha mustakabali wa uchumi na wananchi wake utegemee mkutano wa kimaonyesho na Rais Donald Trump wa Marekani. Ameongeza kuwa, kama ambavyo Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alivyosema, 'iwapo Mareknai inataka kufanya mazungumzo na Iran, ni lazima kwanza itekeleze ahadi zake na isitishe vikwazo.'
-
Hujuma dhidi ya Waislamu zimeongeza nchini Marekani katika kipindi cha uongozi wa Trump
Sep 18, 2019 03:18Baraza la Uhusiano wa Kiislamu la Marekani limetangaza kuwa, hujuma na mashambulio dhidi ya Waislamu nchini humo yameongezeka mno katika kipindi cha uongozi wa Rais Donald Trump.
-
Independent: India inafanya mikakati ya kuwapokonya uraia mamilioni ya Waislamu
Aug 19, 2019 22:05Gazeti la Independent linalochapishwa nchini Uingereza limefichua kwamba, serikali ya India inapanga mikakati ya kuwapokonya uraia watu wasiopungua milioni nne aghlabu yao wakiwa ni Waislamu na kuwatambua kuwa ni wahajiri wa kigeni.
-
Familia ya binti Msomali-Muingereza aliyegharikishwa yataka haki
Aug 13, 2019 02:59Familia ya binti Msomali mwenye uraia wa Uingereza aliyegharikishwa imetaka haki na uadilifu baada ya kubainika kuwa alipoteza maisha kwa njia ya kutatanisha.
-
Ujumbe wa Kiongozi Muadhamu kwa Mahujaji; kujibari na washirikina fursa kwa ajili ya mataifa madhulumu ya Waislamu
Aug 11, 2019 06:22Marasimu ya kujibari na kujiweka mbalii na washirikina yalifanyika jana Jumamosi katika jangwa la Arafa kwa kusomwa ujumbe wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa Mahujaji wa Nyumba Tukufu ya Mwenyezi Mungu na Waislamu wote.
-
Kupigwa marufuku shughuli za Harakati ya Kiislamu ya Nigeria na taathira zake
Jul 29, 2019 05:32Wakati Waislamu wa Nigeria wakiendeleza jitihada za kuhakikisha kwamba kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo, Sheikh Ibrahim Zakzaky anaachiwa huru, Rais wa nchi hiyo amepiga marufuku shughuli zote za harakati hiyo.
-
Baraza la Kiislamu nchini Ujerumani lalalamikia miamala mibaya ya polisi dhidi ya Waislamu
Jun 06, 2019 22:37Baraza Kuu la Waislamu nchini Ujerumani limekosoa mimala ya ukandamizaji ya maafisa wa polisi wa nchi hiyo kuwalenga Waislamu.