-
Rais wa Iran atoa mkono wa Idi kwa viongozi na wananchi wa mataifa ya Kiislamu
Mar 30, 2025 23:51Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewatumia salamu za mkono wa Idi na kuwapongeza viongozi na wananchi wa mataifa ya Kiislamu kwa mnasaba wa kuadhimisha na kushereheka Idul-Fitri, siku ya sherehe na furaha kubwa kwa Waislamu.
-
Kwa nini Trump hastahamili kuwepo kwa wahamiaji Waislamu huko Marekani?
Jan 27, 2025 23:23Moja ya amri tisa za Donald Trump katika siku ya kwanza ya uongozi wake ni kupitiwa upya sheria ya kurejesha marufuku ya Waislamu kuingia Marekani, suala ambalo iwapo litaidhinishwa na kutekelezwa, litakuwa na madhara makubwa kwa wahamiaji Waislamu nchini Marekani na hata waombaji visa Waislamu.
-
Mashirika ya haki yaonya; Trump atarejesha marufuku dhidi ya Waislamu
Jan 23, 2025 04:07Mashirika ya kutetea haki za kiraia nchini Marekani yameonya kuwa, amri ya utendaji iliyosainiwa na Rais Donald Trump siku ya Jumatatu inaweka msingi wa kurejesha marufuku ya wasafiri kutoka nchi zenye Waislamu na Waarabu wengi kuingia Marekani.
-
Qalibaf: Iran imesimama imara kuwatetea Waislamu duniani
Jan 17, 2025 23:12Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema: Iran siku zote inasisima imara na imeonyesha kuwa ni nchi pekee inayowatetea Waislamu wote bila ya kujali madhehebu zao na imetoa maelfu ya mashahidi katika njia hii.
-
Hadi ifikapo 2050 Waislamu watakuwa khumsi moja ya watu wote barani Ulaya
Jan 10, 2025 23:27Tovuti ya habari ya Globe Eye News imeripoti kuwa idadi ya Waislamu barani Ulaya itazidi kuongezeka katika kipindi cha miaka ijayo.
-
Mahakama Kuu ya India yabatilisha hukumu ya kuzifunga Madrasa 17,000 za Waislamu
Nov 09, 2024 03:05Baada ya uhakiki na uchunguzi uliochukua muda wa miezi kadhaa, Mahakama Kuu ya India hatimaye imetoa uamuzi wa kubakishwa Madrasa 17,000 za Waislamu zilizotaka kufungwa katika jimbo kubwa zaidi la nchi hiyo la Uttar Pradesh.
-
Rais Pezeshkian: Umoja utawafanya Waislamu kuwa na nguvu kubwa
Oct 31, 2024 22:57Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya umoja baina ya nchi za Kiislamu na kusema: Iwapo tutaweza kufikia umoja katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii, tunaweza kuwa nguvu kubwa katika eneo la Asia Magharibi, na katika hali hii Marekani haiwezi kutuwekea vikwazo.
-
Rais wa Iran asisitizia umuhimu wa umoja wa Waislamu
Oct 11, 2024 07:48Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesisitiza haja ya umma wa Kiislamu kuwa na umoja na mshikamano na kubainisha kwamba, migawanyiko kati ya Waislamu itawanufaisha maadui pekee.
-
Rais wa Iran: Jinai za Israel ni matokeo ya ukosefu wa umoja wa Waislamu
Sep 19, 2024 11:19Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, adui analeta mgawanyiko na mifarakano kati yetu na kubainisha kwamba, Waisraeli milioni 2 au 3 wanawaangamiza Waislamu, wanaua wanawake na watoto, wazee na vijana na wagonjwa, wanapiga mabomu hospitali na misikiti na sisi tumekaa tu na kutazama, kwa sababu hatuna umoja na ndio maana Israel inathubutu kufanya jinai hizi.
-
Qalibaf: Madai ya uwongo ya nchi za Magharibi yanakwamisha mazungumzo yenye tija
Sep 15, 2024 23:23Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa hakutakuwepo mazungumzo yoyote yenye tija maadamu nchi za Ulaya na nyingine za Magharibi zinataka kuandaa mazingira kwa ajili ya mashinikizo zaidi kwa kutoa madai ya uwongo.