-
Kenya yalaumiwa kwa kupuuza ripoti ya dhulma kwa watoto
Aug 16, 2025 07:47Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International, limemshtumu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya Kipchumba Murkomen kwa kupuuza uchunguzi uliofanywa na shirika moja kuhusu ulanguzi wa watoto nchini humo.
-
AU yataka ulimwengu utumie ramani ya dunia inayoakisi ukubwa halisi wa bara la Afrika
Aug 16, 2025 01:38Umoja wa Afrika (AU) umeunga mkono kampeni inayolenga kukomesha matumizi ya ramani ya dunia ya karne ya 16 ya Mercator, inayotumiwa na serikali na mashirika ya kimataifa, na badala yake kutumia ramani inayowakilisha kwa usahihi zaidi ukubwa wa bara la Afrika.
-
Wanigeria wafanya matembezi ya amani ya Arubaini ya Imam Hussein (as) na kutangaza mshikamano na Gaza
Aug 15, 2025 22:52Maelfu ya waombolezaji wa Nigeria wamekamilisha matembezi ya kinembo ya siku mbili ya kumbukumbu ya Arubaini ya Imam Hussein (as) na kutangaza himaya na uungaji mkono wao kwa Wapalestina.
-
Anayedaiwa kuwa jasusi wa Ufaransa akamatwa kwa madai ya njama ya mapinduzi ya Mali
Aug 15, 2025 22:51Watawala wa kijeshi wa Mali wametangaza kuwa wamemkamata raia mmoja wa Ufaransa kwa tuhuma za kufanya ujasusi wa nchi yake katika jaribio la kuliyumbisha taifa hilo la Afrika.
-
Zaidi ya watu milioni nne wanakabiliwa na baa la njaa Somalia
Aug 15, 2025 07:21Idadi ya watu wanaokabiliwa na baa la njaa nchini Somalia inazidi kuongezeka katika nchi hiyo inayokabiliwa na ukosefu wa amani kutokana na harakati za kundi la kigaidi la al-Shabab.
-
MSF: Kipindupindu 'kibaya' kuwahi kutokea ndani ya miaka mingi kimeua watu 40 Darfur, Sudan
Aug 15, 2025 03:59Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limeripoti kuwa, watu wasiopungua 40 wamefariki dunia katika eneo la Darfur, Sudan katika kipindi cha wiki moja, huku nchi hiyo ikikabiliana kudhibiti mripuko mkubwa zaidi wa kipindupindu kuwahi kushuhudiwa nchini humo katika kipindi cha miaka mingi.
-
Kadhaa wajeruhiwa, biashara za mamilioni zachomwa moto katika machafuko ya Embu, Kenya
Aug 15, 2025 02:11Kikosi maalumu cha wapelelezi kimetumwa mjini Siakago, Kaunti ya Embu nchini Kenya kufuatia wimbi la machafuko ambavyo yamesababisha wakazi kadhaa kujeruhiwa na mali zenye thamani ya mamilioni ya shilingi kuharibiwa.
-
Upinzani Uganda wafungua kesi mahakamani kupinga raia kushtakiwa kwenye mahakama ya kijeshi
Aug 14, 2025 22:57Chama kikuu cha upinzani nchini Uganda cha Jukwaa la Umoja wa Kitaifa (National Unity Platform) NUP, kimefungua kesi katika Mahakama ya Katiba ya kutaka sheria mpya iliyorudisha haki ya mahakama za kijeshi kusikiliza kesi za raia ifutwe.
-
UN yasema kunyimwa dhamana Besigye na mahakama ya Uganda kunatia hofu kubwa
Aug 14, 2025 09:36Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, (OHCHR), imesema mwenendo wa Mahakama Kuu ya Uganda wa kumnyima dhamana mara kwa mara kiongozi mkongwe wa upinzani nchini humo Kizza Besigye pamoja na msaidizi wake Obeid Lutale katika kesi inayowakabili ni jambo linalotia hofu kubwa.
-
Watu 25 wafukiwa na kifusi Tanzania wakati shughuli za ukarabati mgodi
Aug 14, 2025 03:23Watu 25 wamefukiwa na kifusi katika mgodi mdogo wa dhahabu unaomilikiwa na Kikundi cha Wachapakazi, uliopo Kijiji cha Mwongozo, Kata ya Mwenge, Halmashauri ya Shinyanga, mkoani Shinyanga nchini Tanzania, baada ya mgodi huo kutitia wakati wa zoezi la ukarabati wa maduara.