-
DRC yawapandisha kizimbani wanajeshi wake kwa kutoroka vita; inawatuhumu pia kwa ubakaji
Feb 10, 2025 03:52Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza kuwa wanajeshi wasiopungua 75 wanatazamiwa kufikishwa mahakamani leo Jumatatu wakikabiliwa na shtaka la kuwakimbia wapiganaji wa kundi la waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda katika jimbo la Kivu ya Mashariki.
-
Bunge la Afrika Mashariki lasimamisha vikao vyake kwa muda usiojulikana kwa sababu za kifedha
Feb 10, 2025 03:30Bunge la nchi za Afrika Mashariki, EALA limetangaza kuwa limesimamisha vikao vyake kwa muda usiojulikana kutokana na changamoto za kifedha, zilizosababishwa na baadhi ya nchi wanachama kushindwa kulipa michango yao ya fedha.
-
Libya yagundua makaburi mawili ya halaiki yenye miili ipatayo 50 ya wahajiri na wakimbizi
Feb 10, 2025 03:29Mamlaka za Libya zimegundua miili ipatayo 50 kwenye makaburi mawili ya halaiki katika jangwa la kusini mashariki mwa nchi hiyo, katika maafa ya karibuni zaidi yaliyohusisha watu wanaotaka kufika Ulaya kupitia nchi hiyo ya Afrika Kaskazini.
-
Vyombo vya habari Kenya vyazungumzia athari za ushindi wa Odinga kama mkuu wa Kamisheni ya AU
Feb 09, 2025 23:13Vyombo vya habari vya Kenya vimechapisha ripoti kuhusu athari za matokeo ya ushindi wa mgombea wa nchi hiyo, Raila Odinga, katika uchaguzi wa nafasi ya Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, unaotarajiwa kufanyika wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Afrika mjini Addis Ababa wiki ijayo, katika siasa za ndani nchini Kenya.
-
Wanasheria Tunisia: Kesi ya Instalingo ni njama ya Kisiasa ya kuwamaliza wapinzani wa serikali
Feb 09, 2025 23:12Maamuzi yaliyotolewa na mahakama ya Tunisia katika kesi inayojulikama kama "Instalingo" yanaendelea kuibua hisia hasi kutoka kwa mawakili, wanaharakati wa kutetea haki za binadamu na timu ya utetezi kwa washtakiwa, ambao wanayataja maamuzi hayo kuwa yasiyo na mantiki wala msingi wa kisheria, na kwamba lengo lake ni kuwafutilia mbali wapinzani wa kisiasa wa serikali ya Tunis.
-
Mali: Tunawasaka wanamgambo wenye silaha waliouwa watu zaidi ya 25
Feb 09, 2025 23:11Jeshi la Mali limeahidi kuwasaka "magaidi" waliohusika na shambulio la kikatili dhidi ya msafara mkubwa uliokuwa ukielekea kwenye mgodi wa dhahabu nchini humo.
-
Suluhisho la kikanda ndiyo njia bora ya kumaliza mgogoro wa Kongo DR
Feb 09, 2025 07:17Wakuu wa nchi wanachama katika jumuiya mbili za kikanda za Mashariki na Kusini mwa Afrika, jana Jumamosi, wafanya mkutano wa aina yake katika mji mkuu wa Tanzania, Dar es Salaam wakijaribu kutafuta suluhisho la kumaliza mgogoro wa mashariki mwa Kongo DR.
-
Ethiopia yaahidi kutumia fursa za biashara huria kutoa fursa zaidi barani Afrika
Feb 09, 2025 07:09Waziri wa Biashara na Ushirikiano wa Kikanda wa Ethiopia amesema kuwa, nchi yake ina nia thabiti ya kuhakikisha kunakuwepo utekelezaji madhubuti wa makubaliano ya Eneo Huria la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA) ili kutoa fursa kubwa za soko la ndani ya bara pana na kubwa la hilo.
-
Bunge la Libya lalaani njama za Wazayuni za kuwahamisha watu wa Ghaza
Feb 09, 2025 07:07Bunge la Libya limelaani na kupinga njama za Marekani na Israel za kutaka kuwahamisha wananchi wa Ghaza na kuwapeleka sehemu nyingine nje ya ardhi zao za jadi za Palestina.
-
Waafrika Kusini 'weupe' wakataa 'ofa' ya kuwa wakimbizi Marekani
Feb 09, 2025 03:42Raia wa Afrika Kusini wenye asili ya Uholanzi na nchi nyingine za Ulaya wamepuuzilia mbali mwito wa Rais Donald Trump, wa kwenda kuwa wakimbizi nchini Marekani, kwa madai ya kubaguliwa nchini Afrika Kusini.