-
Nigeria imewezaje kusambaratisha mahesabu ya mapinduzi nchini Benin?
Dec 09, 2025 23:05Uingiliaji wa haraka wa Nigeria kwa ombi la serikali ya Benin, ulifelisha jaribio la mapinduzi na kuzuia kuenea kwa ukosefu wa utulivu katika Afrika Magharibi.
-
ICC imemhukumu kiongozi wa Janjaweed wa Darfur kifungo cha miaka 20 jela
Dec 09, 2025 08:05Majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) leo Jumanne wamemhukumu kiongozi wa wanamgambo wa Janjaweed katika jimbo la Darfur Sudan kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya kufanya ukatili katika jimbo la Darfur.
-
Kikosi kipya cha polisi wa Kenya chawasili Haiti kukabiliana na magenge ya uhalifu
Dec 09, 2025 07:59Hiki ni kikosi cha tano cha polisi wa Kenya kufika huko Haiti kisiwa kilichokumbwa na ghasia tangu kuanza kuhudumu kwa misheni ya polisi inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa. Kenya ina polisi zaidi ya 700 nchini humo.
-
Nchi za eneo la Sahel zatishia kusimamisha ndege za Nigeria iwapo anga ya nchi hizo itakiukwa
Dec 09, 2025 07:58Shirikisho la Nchi za Sahel barani Afrika linalojumuisha Mali, Niger na Burkina Faso (AES) limetangaza kuwa litazizuia ndege zote zinazokiuka anga yashirikisho hilo kufuatia ripoti za ukiukaji wa sheria uliofanywa na Nigeria.
-
Mwanaharakati: Nchi za Afrika ziige mfano wa Kenya wa kuchunguza jinai za jeshi la Uingereza
Dec 09, 2025 03:58Uchunguzi wa bunge la Kenya kuhusu makosa na ukiukaji uliofanywa na Kikosi cha Mafunzo cha Jeshi la Uingereza nchini Kenya (BATUK) umeibua wito wa muda mrefu wa kuhoji mienendo ya majeshi ya kigeni barani Afrika.
-
Rais wa DRC aituhumu Rwanda kwa kukiuka makubaliano ya 'amani' yaliyofikiwa Marekani
Dec 09, 2025 03:56Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Félix Tshisekedi, ameituhumu Rwanda kwa kukiuka makubaliano ya 'amani' yaliyosimamiwa na Marekani na kutiwa saini wiki iliyopita mjini Washington DC.
-
Mlipuko wa kipindupindu DRC umeua watu 1,888, wakiwemo watoto 340
Dec 09, 2025 03:54Mlipuko wa kipindupindu mwaka huu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) umeleta madhara makubwa, ukiwa na jumla ya wagonjwa 64,427 tangu mwanzo wa mwaka huu 2025, na kusababisha vifo 1,888. Watoto waliougua ni 14,818 na waliofariki dunia ni 340, na hivyo kufanya huu kuwa mlipuko mbaya zaidi katika kipindi cha miaka 25 nchini humo. Hayo ni kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF linaeleza.
-
Idadi ya waliokufa kutokana na hujuma ya RSF Kusini mwa Kordofan, Sudan, yafikia 114
Dec 08, 2025 23:10Mamlaka za Sudan katika jimbo la Kordofan Kusini zimethibitisha maafa makubwa: shambulio la ndege isiyo na rubani la waasi wa RSF lililotokea Alhamisi, Desemba 4, hadi sasa limeua watu 114 na kujeruhi 71. Miongoni mwa waliokufa wamo watoto 63 na idadi hiyo ingali inaongezeka.
-
Tinubu: Jeshi la Nigeria ‘lililinda’ Benin kufuatia jaribio la mapinduzi
Dec 08, 2025 23:09Rais wa Nigeria, Bola Tinubu, amesema vikosi vya ulinzi vya nchi yake vilisaidia kulinda taifa jirani la Benin baada ya jaribio la mapinduzi ya kijeshi Jumapili.
-
Ukosefu mkubwa maji unazidi kusambaa kusini mwa Somalia
Dec 08, 2025 23:08Vyanzo muhimu vya maji kusini mwa Somalia vinakauka kwa kasi huku ukame ukiongezeka, na kusababisha uhaba mkubwa kwa mamia ya maelfu ya watu.