-
Viongozi wa nchi za kigeni waanza kuwasili Nairobi kwa mazishi ya Raila Odinga
Oct 17, 2025 08:29Matayarishao ya maziko ya mwanasiasa mashuhuri wa Kenya Raila Odinga, aliyefariki dunia juzi Jumatano akiwa na umri wa miaka 80 alipokuwa anatibiwa nchini India, yanaendelea na tayari viongozi wa nchi za kigeni wameanza kuwasili mjini Nairobi kushiriki kwenye maziko hayo yanayotarajiwa kufanyika kashokutwa Jumapili jimboni kwake Bondo.
-
Kanali Randrianirina aapishwa kuwa rais mpya wa Madagacar, SADC yaunda timu
Oct 17, 2025 08:29Kanali wa kijeshi, Michael Randrianirina, ameapishwa leo Ijumaa kuwa rais wa Madagascar katika mji mkuu, Antananarivo huku umuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ikimteua Rais wa zamani wa Malawi Joyce Banda kuongoza ujumbe wa kutafuta ukweli nchini Madagascar kufuatia matukio ya hivi karibuni ya kisiasa na kiusalama nchini humo.
-
Majeshi ya Nigeria yaua makumi ya waasi katika operesheni za nchi nzima
Oct 17, 2025 08:29Jeshi la Nigeria limetoa taarifa na kutangaza kuwa makumi ya waasi wameuawa na wengine 62 kukamatwa na vikosi vya serikali katika operesheni za nchi nzima kwenye kipindi cha wiki mbili zilizopita.
-
Mripuko wa homa ya Bonde la Ufa waua watu 33 Senegal, Mauritania
Oct 17, 2025 03:47Watu wasiopungua 33 wamefariki dunia kutokana na homa ya Bonde la Ufa nchini Senegal na Mauritania tangu kuzuka kwa mripuko wa homa hiyo nadra mwishoni mwa Septemba, afisa wa Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC) alisema hayo jana Alkhamisi.
-
Rais Rajoelina athibitisha kuikimbia Madagascar
Oct 16, 2025 22:46Rais wa Madagascar aliyeondolewa madarakani Andry Rajoelina amethibitisha kwa mara ya kwanza kwamba aliikimbia nchi hiyo kati ya Oktoba 11 na 12.
-
AU yaisimamishia uanachama Madagascar kufuatia mapinduzi ya kijeshi
Oct 16, 2025 02:54Umoja wa Afrika umetengaza kuisimamishia unachama Madagascar "hadi utaratibu wa kikatiba utakaporejeshwa" baada ya mapinduzi yaliyomuondoa madarakani Rais Andry Rajoelina.
-
Shirika la Mashad: Watu 146 wameuawa El-Fasher, Sudan
Oct 16, 2025 02:16Shirika la kutetea haki za binadamu la Mashad limerekodi vifo vya raia 146, wakiwemo watoto 41 katika siku za hivi karibuni katika mji El-Fasher magharibi mwa Sudan.
-
Mwanasiasa mkongwe Raila Odinga aombolezwa; Rais Ruto atangaza siku saba za maombolezo
Oct 15, 2025 22:57Rais William Ruto ametangaza kipindi cha maombolezo ya kitaifa kwa muda wa siku saba kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Amollo Odinga.
-
DRC, M23 zasaini makubaliano ya kubuni utaratibu wa usitishaji mapigano
Oct 15, 2025 08:12Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kundi la waasi la M23 wametia saini makubaliano mjini Doha ya kuanzisha utaratibu wa ufuatiliaji na uhakiki wa usitishaji mapigano, chini ya upatanishi wa Qatar.
-
Waziri Mkuu wa zamani na mkongwe wa siasa za Kenya Raila Odinga afariki dunia akiwa matibabuni India
Oct 15, 2025 04:27Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga amefariki dunia leo asubuhi huko Koothattukulam, wilayani Ernakulam nchini India, baada ya kupata mshtuko wa moyo wakati anafanya matembezi yake ya kila asubuhi.