-
Iran yaonya: Israel itajitanua zaidi Asia Magharibi iwapo haitadhibitiwa
Aug 18, 2025 07:34Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baqaei amesema Israel ni tishio kwa usalama na uthabiti wa Asia Magharibi kutokana na mwenendo wake wake kupenda kujitanua, akionya kuwa eneo hili la kistratejia linaweza kukabiliwa na vita visivyoisha ikiwa utawala huo hautazuiwa.
-
Kwa nini Ulaya sasa inatafuta kuamilisha utaratibu wa Snapback baada ya miaka mingi ya kutokuchukua hatua?
Aug 18, 2025 04:53Wakati nchi tatu za Ulaya zinajaribu kutumia utaratibu wa Snapback dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, mbali na Iran yenyewe, Russia na China pia zinapinga utumiaji wa utaratibu huo au urejeshaji otomatiki wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa, na kuutaja kuwa kinyume cha sheria.
-
Iran yalaani uamuzi wa Israel wa kuwafurusha Wapalestina Jiji la Gaza
Aug 18, 2025 03:15Iran imelaani vikali uamuzi wa Israel wa kuwalazimisha Wapalestina kuhama makazi yao na kuelekea kusini mwa Gaza na kusisiitiza kuwa, jamii ya kimataifa na nchi za Kiislamu zina wajibu wa kukabiliana na uhalifu huo wa kutisha wa kivita.
-
Larijani: Israel imedhoofika kutoka na wimbi la makombora ya Iran
Aug 17, 2025 23:59Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC), Ali Larijani amesema kuwa, wimbi la mashambulio ya makombora ya Iran lilimfanya adui Mzayuni akate tamaa kikamilifu wakati wa vita vya siku 12 vya Israel ilivyoitwisha Jamhuri ya Kiislamu.
-
Kwa nini msimamo wa Umoja wa Nchi za Kiislamu dhidi ya mpango wa "Israel Kubwa" ni hatua ya kukabiliana na kujitanua kwa utawala wa Kizayuni?
Aug 17, 2025 23:24Katika radiamali ambayo haijawahi kushuhudiwa tena huko nyuma, nchi 31 za Kiislamu zimetoa taarifa ya pamoja zikilaani mpango wa Benjamin Netanyahu wa kuunda "Israeli Kubwa" na huku zikitahadharisha kuhusu hatari ya sera hiyo ya kupenda kujitanua, zimeutaja mpango huo kuwa tishio kwa usalama wa eneo, ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa na hatua ya kuchochea ghasia na ukosefu wa amani katika eneo la Asia Magharibi.
-
Magaidi kadhaa waangamizwa katika operesheni ya IRGC kusini mashariki mwa Iran
Aug 17, 2025 08:48Vikosi vya usalama vya Iran vimesambaratisha mtandao mkubwa wa magaidi wakufurishaji na kuua kadhaa miongoni mwao, mbali na kunasa silaha na mabomu kadhaa katika mkoa wa kusini mashariki wa Sistan na Baluchestan.
-
Iran yamjia juu Makamu wa Rais wa ICJ kwa kuikingia kifua Israel
Aug 17, 2025 08:24Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amemkosoa vikali Julia Sebutinde, Makamu wa Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kutokana na uungaji mkono wake wa wazi kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Balozi wa Iran awashukuru viongozi wa serikali na kidini wa Iraq kwa kufanikisha maadhimisho ya Arbaeen
Aug 17, 2025 07:14Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Iraq ametoa shukurani zake za dhati kwa mamlaka kuu, serikali, wananchi, viongozi wa makabila na vikosi vya usalama vya Iraq kwa kuandaa kwa mafanikio maadhimisho ya Arbaeen ya Imam Hussein (as) na kulitaja suala hilo kuwa mfano usio na mbadala, wa wema na ukarimu wa Wairaki.
-
IRGC: Taifa liko tayari kuvunja safu yoyote ya adui
Aug 17, 2025 04:09Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesisitiza kuwa taifa la Iran liko tayari kusimama kidete kukabiliana na maadui wa Jamhuri ya Kiislamu na kuwalazimisha wasalimu amri kama lilivyofanya katika makabiliano yaliyopita.
-
Qalibaf: Muda wa kumdhibiti mbwa kichaa wa Kizayuni unayoyoma
Aug 15, 2025 23:27Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, Gaza ndiyo "ngome ya mwisho" ya Waislamu, na kusisitiza haja ya kuungwa mkono Palestina haraka iwezekanavyo, kabla ya ardhi nyingine katika eneo kushambuliwa na kuporwa na utawala ghasibu wa Israel.