-
Araghchi asisitiza: Iran ina haki ya kumiliki mzunguko kamili wa fueli ya nyuklia
May 03, 2025 03:27Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema, kurudia kila mara kauli za uwongo hakubadilishi ukweli wa kimsingi na akaeleza bayana kwamba, Iran, ikiwa ni miongoni mwa nchi zilizotia saini mkataba wa NPT, ina haki ya kumiliki mzunguko kamili wa fueli ya nyuklia.
-
Iran yalaani jinai za kivita za Marekani nchini Yemen
May 02, 2025 23:13Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei amelaani vikali wimbi la mashambulizi ya jeshi la Marekani katika muda wa saa 24 zilizopita katika maeneo mbalimbali ya majimbo ya Sana'a, Saada, na Al-Jawf nchini Yemen, yakilenga miundombinu na maeneo ya makazi ya Yemen.
-
Seddiqi: Teknolojia ya nyuklia ni mtaji wa taifa/kuna udharura wa kuwaheshimu walimu na wafanyakazi
May 02, 2025 07:44Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo ya hapa mjini Tehran ameashria mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja ya nyuklia kati ya Iran na Marekani yaliyoanza wiki kadhaa zilizopita na kusema: Timu ya mazungumzo ya Iran ina uzoefu mkubwa; na katika mazungumzo hayo inatetea kwa nguvu na irada kamili haki ya Iran ya kumiliki teknolojia ya amani ya nyuklia ambayo ni mtaji wa taifa.
-
Araghchi: Iran imeazimia kikweli kufikia makubaliano yenye uwiano
May 02, 2025 07:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi amesema kuwa Iran hivi sasa imeazimia kikwelikweli kufikia makubaliano ya haki na yenye uwiano kuliko wakati mwingine wowote.
-
Mkuu wa Kamati ya Bunge ya Usalama wa Taifa Iran ajibu vitisho vya Waziri wa Ulinzi wa Marekani
May 02, 2025 04:09Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu amejibu vitisho vya Waziri wa Ulinzi wa Marekani akisema kuwa, Wamarekani wenyewe ndio watakaolipa gharama ya mienendo yao inayokinzana.
-
Baqaei atangaza mabadiliko katika ratiba ya mazungumzo ya Iran na Marekani
May 02, 2025 03:54Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza kubadilishwa tarehe ya duru ijayo ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja ya Iran na Marekani ambayo yalipangwa kufanyika Jumamosi ya tarehe 4 Mei huko Roma, mji mkuu wa Italia.
-
Iran yaunga mkono 'mazungumzo ya jadi' na mataifa ya Ghuba ya Uajemi
May 01, 2025 23:22Mkuu wa Baraza la Kistratijia la Mahusiano ya Kigeni la Iran amesisitiza haja ya kufanyika mazungumzo ya dhati na jadi kati ya Iran na nchi za Ghuba ya Uajemi, akiyaeleza mazungumzo hayo kama msingi wa utulivu katika eneo.
-
Ismail Baqaei: Vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran vimegonga mwamba
May 01, 2025 10:03Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria uraibu wa Marekani wa kuwekea vikwazo mataifa mengine na kubainisha kwamba, vikwazo vya Washington dhidi ya Tehran vimeshindwa na kutokuwa na natija.
-
Iran yaitaka ICJ kukomesha mauaji ya kimbari ya Gaza, kuruhusiwa misaada ya kibinadamu
May 01, 2025 03:46Tehran imelaani mashambulizi ya Israel kwenye Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan ikiyataja kuwa ni mfano wa wazi wa mauaji ya kimbari na kutoa wito kwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) na jamii ya kimataifa kuchukua hatua ya kuwajibika kukomesha ukatili huo.
-
Majibu ya Tehran kwa Shutuma za Uongo za Ufaransa Kuhusu Mpango wa Nyuklia wa Amani wa Iran
Apr 30, 2025 22:48Mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeed Iravani, amewatumia barua Rais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, akielezea kuwa madai ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa kwamba Iran iko "katika hatua ya mwisho" ya kuzalisha silaha za nyuklia ni yasiyo na msingi na kisiasa ni hatua isiyo ya uwajibikaji. Iran haijawahi kuwa na nia ya kutafuta silaha za nyuklia na haijabadilisha sera yake ya ulinzi.