-
Brigedia Jenerali Ali Jahanshahi: Iran imejiandaa kukabiliana na aina yoyote ile ya vitisho
Dec 14, 2025 07:10Brigedia Jenerali Ali Jahanshahi, Kamanda wa vikosi vya nchi kavu vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, vikosi vya ulinzi vikiwa na zana kamili, silaha na uwezo viko tayari kukabiliana na tishio lolote la adui kwa kusikiliza amri ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Pezeshkian: BRICS inatoa fursa ya ushirikiano imara zaidi wa wanachama
Dec 14, 2025 02:53Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ameashiria nafasi na uwezo wa kundi la BRICS na kulieleza kama jukwaa muhimu la kuimarisha maingiliano na uhusiano wa kiuchumi na kisiasa miongoni mwa nchi wanachama.
-
Khatibzadeh: Uhusiano wa Iran na China mkamilishaji wa mfumo mpya wa kimataifa
Dec 13, 2025 11:41Saeed Khatibzadeh, Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran na Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kisiasa na Kimataifa ameutaja uhusiano wa Iran na China uliojengeka juu ya msingi wa chaguo la maslahi ya pamoja.
-
Iran, Russia zasisitiza kutekeleza mkataba wa ushirikiano wa kimkakati katika mazungumzo ya Pezeshkian na Putin
Dec 13, 2025 02:34Rais Masoud Pezeshkian jana Ijumaa alikutana na kuzungumza na Rais Vladimir Putin wa Russia pambizoni mwa Mkutano wa Kimataifa wa Amani na Uaminifu uliofanyika huko Ashgabat mji mkuu wa Turkmenistan na kusisitiza kuhusu azma thabiti ya Iran ya kutekeleza makubaliano kuhusu ushirikiano wa kina wa kimkakati kati yake na Russia.
-
Iran yalaani mwenendo wa madola makubwa wa kuitunukia Israel 'haki maalumu' ya kufanyia uchokozi
Dec 12, 2025 11:03Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, sera za mataifa makubwa katika Asia Magharibi zimetengeneza "haki maalumu kwa ajili ya utawala wa Kizayuni," hali ambayo imeiwezesha Israel kufanya uchokozi wa kijeshi katika eneo zima, ikiwa ni pamoja na dhidi ya Iran, bila kukabiliwa na mjibizo wa maana kimataifa kwa uchokozi wake huo.
-
Rais Pezeshkian:Iran na Kazakhstan ziimarishe uhusiano ili kukabiliana na Marekani
Dec 12, 2025 03:04Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kuwa Iran na Kazakhstan zinapaswa kuimarisha uhusiano wa karibu ili kukabiliana na ubeberu Marekani.
-
Imamu Khamenei: Watu wa Iran wamesambaratisha njama adui za kubadilisha utambulisho wao wa kidini na kihistoria
Dec 11, 2025 12:59Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inapiga hatua na kusonga mbele licha ya kukabiliwa na mapungufu mengi.
-
Mtazamo wa Iran kuhusu vitendo vya Marekani dhidi ya Venezuela: Uzushi hatari unaotishia amani na usalama wa dunia
Dec 11, 2025 08:45Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amevitaja vitendo vya Marekani dhidi ya Venezuela kuwa ni uzushi hatari unaotishia amani na usalama wa dunia.
-
Israel yakiri: Iran ilikuwa na uwezo wa kumlenga kwa hujuma za mtandao kila Muisraeli katika Vita vya Siku 12
Dec 11, 2025 07:12Mkuu wa idara ya usalama wa kimtandao ya utawala wa kizayuni wa Israel (INCD) amesema, operesheni za kimtandao za Iran za wakati wa vita vya siku 12 mnamo mwezi Juni zilikuwa na wigo mpana kutosha kumfikia kila raia wa Israel na kwamba Tehran ilikuwa ikipanga na kufanya mashambulizi ya makombora dhidi ya maeneo yaliyolengwa kama vile Taasisi ya Weizmann kwa kudukua kwanza kamera za usalama za maeneo hayo.
-
Pezeshkian: Hatua ya Marekani dhidi ya Venezuela ni uzushi hatari unaotishia amani ya dunia
Dec 11, 2025 03:35Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amekosoa na kulaani waziwazi vitendo haramu vya Marekani katika eneo la Karibi, akisema: "Kitendo cha serikali ya Marekani cha kutuma meli za kivita huko Karibi na pwani ya Venezuela, kwa visingizio vya uwongo, ni haramu, ukiukaji wa sheria za kimataifa na ni uzushi hatari unaotishia amani na usalama wa dunia."