-
Iran: Hatutosita kutoa majibu makali na ya haraka kwa jinai za Israel
Aug 01, 2024 03:12Balozi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, Tehran italinda vilivyo haki zake kwa mujibu wa kifungu cha 51 cha hati ya Umoja wa Mataifa na haitosita kutoa majibu makali na ya haraka kwa jinai za utawala wa Kizayuni.
-
Kan'ani: Kutoguswa nchi mbalimbali na jinai za Israel kunachochea ugaidi wa dola hilo pandikizi
Aug 01, 2024 03:11Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa mara nyingine tena amelaani jinai iliyofanywa na Israel ya kumuua shahidi Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya HAMAS hapa Tehran na kusisitiza kuwa, kimya na dharau inayooneshwa na nchi na mashirika ya kimataifa mbele ya jinai za kutisha za utawala wa Kizayuni ni sawa na kuchochea ugaidi wa kiserikali unaofanywa na dola hilo pandikizi.
-
Kiongozi wa Mapinduzi kuongoza Sala ya Maiti ya kumsalia Shahidi Haniya, Iran yamuomboleza kwa siku tatu
Jul 31, 2024 23:49Ofisi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu imetangaza kuwa, Ayatullah Khamenei leo asubuhi ataongoza Sala ya Maiti ya kumsalia Shahidi Ismail Haniya, Mwanjihadi mkubwa wa Muqawama wa Palestina, itakayosaliwa katika Chuo Kikuu cha Tehran.
-
Msimamo wa pamoja wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na Rais Masoud Pezeshkian kuhusu uungaji mkono kwa taifa la Palestina
Jul 31, 2024 22:56Ayatullah Ali Khamenei Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na Daktari Masoud Pezeshkian, Rais mpya wa Iran siku ya Jumanne katika vikao vyao na marehemu Ismail Haniyeh, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamas na Ziad al-Nakhaleh, Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina walisisitiza kwamba suala la kuiunga mkono Palestina ni msimamo imara na wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Huyu ndiye Ismail Haniyeh, Kiongozi Mkuu wa Kisiasa wa HAMAS aliyeuawa shahidi Tehran
Jul 31, 2024 08:31Jumanne usku ya tarehe 30 Julai 2024, Ismail Haniyeh Kiongozi wa Tawi la Kisiasa la Harakati ya HAMAS ameuawa shahidi akiwa na mlinzi wake mmoja hapa Tehran. Ufuatao hapa chini ni wasifu kwa muhtasari wa maisha yake.
-
IRGC: Israel isubiri jibu kali la kuumiza kwa kumuua kigaidi Haniyah
Jul 31, 2024 07:27Kamanda wa Kikosi cha Anga za Mbali cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) ameuonya vikali utawala wa Kizayuni wa Israel na kuutaka ujiandae kwa matokeo mabaya na majibu makali ya kuumiza kwa kumuua kigaidi Ismail Haniyah, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS).
-
Kiongozi Muadhamu: Utawala wa Kizayuni umejiandalia uwanja wa kuadhibiwa vikali
Jul 31, 2024 07:15Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe maalumu baada ya kuuawa shahidi Mkuu wa Tawi la Kisiasa la HAMAS akisisitiza kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umejiandalia uwanja wa kuadhibiwa vikali.
-
Rais Pezeshkian: Iran itawafanya wavamizi magaidi kujutia kitendo chao cha uoga
Jul 31, 2024 04:43Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Iran itawafanya wavamizi wa magaidi kujutia kitendo chao cha uoga.
-
Iran: Damu ya shahidi Ismail Haniya haitapotea bure
Jul 31, 2024 03:57Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran ametoa mkono wa pole kufuatia kuuawa shahidi Ismail Haniya Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) na kueleza kwamba, hapana shaka kuwa, damu ya mujahidi huyo haitapotea bure.
-
Ismail Haniyeh ameuawa shahidi katika hujuma ya kigaidi mjini Tehran
Jul 31, 2024 00:23Idara ya Uhusiano wa Umma ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) imetangaza kuwa mkuu wa Idara ya Siasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) Ismail Haniyeh na mmoja wa walinzi wake wameuawa shahidi baada ya kushambuliwa makazi yao mjini Tehran.