-
Jeshi la Iran laapa kulinda usalama na uhuru wa nchi
Mar 31, 2024 03:03Vikosi vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimetangaza azma ya kuendeleza juhudi za kiwango cha juu ili kufikia malengo ya Mapinduzi ya Kiislamu na kulinda usalama na uhuru wa taifa.
-
Viongozi wa harakati za Palaestina za Hamas na Jihad Islami wakutana Tehran
Mar 30, 2024 07:43Ismail Haniyah, mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amekutana mjini Tehran na Katibu Mkuu wa Harakati ya Palestina ya Jihad Islami Ziyad al-Nakhaleh.
-
Sisitizo la Pakistna la kuhitajia mno gesi ya Iran
Mar 29, 2024 23:01Musadik Masood Malik, Waziri wa Mafuta wa Pakistan amesema kuwa nchi yake inahitajia mno gesi ya Iran na kwamba msimamo wa Islamabad uko wazi kuwa, kukamilishwa mradi wa kupelekwa gesi ya Iran nchini Pakistan ni jambo la dharura.
-
Iran: Majanga ya Gaza ni maabara ya kupima haki za binadamu
Mar 29, 2024 22:59Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, majanga chungu nzima yaliyowapa watu wa Ukanda wa Gaza katika kipindi cha miezi 6 iliyopita ni maabara ya kupima ni kwa kiwango gani nchi na jamii ya kimataifa zinavyoheshimu haki za binadamu.
-
Meja Jenerali Bagheri: Jibu la Israel kwa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa ni mauaji ya watu wasio na hatia
Mar 29, 2024 22:58Mkuu wa Majeshi ya Iran amesema kuwa, jibu la utawala wa Kizayuni wa Israel kwa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa ni kuwaua tu watu wasio na hatia, wakiwemo wanawake na watoto, kuharibu hospitali na kusababisha njaa.
-
Ayatullah Khatami: Siku ya Quds itakuwa tofauti kabisa mwaka huu
Mar 29, 2024 08:42Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa hapa Tehran hii leo ameashiria jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kusema kuwa, hadithi ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu, itakuwa hadithi tofauti kabisa kutokana na hamasa na wingi wa watu watakaoshiriki matembezi ya siku hiyo.
-
Spika Qalibaf: Ulimwengu wote wa Kiislamu una wajibu wa kuunga mkono Muqawama wa taifa la Palestina
Mar 29, 2024 04:31Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amepongeza istikama na kusimama imara kusio na mfano kwa Muqawama na wananchi wa Palestina dhidi ya utawala ghasibu wa Israel na akasema, Ulimwengu mzima wa Kiislamu una wajibu wa kuliunga mkono taifa la Palestina katika vita visivyo na mlingano na utawala huo wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
-
Kiongozi Mkuu: Ghaza ndiyo mshindi mkuu kwenye medani ya vita na utawala wa Israel mwangamizaji wa kizazi
Mar 29, 2024 00:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema vikosi vya Muqawama na watu wa Ghaza ndio washindi kwenye medani ya vita na utawala wa Israel mwangamizaji wa kizazi na akasisitiza kwa kusema: kilele cha kuheshimika na kusimama imara watu wa Ghaza na Palestina na kushindwa utawala wa Kizayuni katika vita hivyo vya miezi sita ni tukio na jambo lenye rehma za Mwenyezi Mungu.
-
Iran: Walimwengu wana wajibu wa kuubebesha dhima utawala wa Kizayuni
Mar 28, 2024 23:09Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameitaka jamii ya kimataifa ichukue hatua na kuubebesha dhima utawala wa Kizayuni, baada ya Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Masuala ya Palestina kufanya tathmini ambayo imezitaja jinai za utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Gaza kuwa ni mauaji ya kimbari.
-
Msisitizo wa Iran juu ya haki yake katika medani ya gesi ya Arash
Mar 28, 2024 02:20Naibu Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Masuala ya Sheria, Mohammed Dehghan, amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitafumbia jicho kwa hali yoyote ile haki zake katika medani ya pamoja ya gesi ya Arash na haitaruhusu upande wowote kukiuka sheria za kimataifa katika suala hili.