-
Jeshi la Yemen limetekeleza operesheni 13 za makombora dhidi ya Israel ndani ya siku 10
Dec 30, 2024 04:22Msemaji wa Jeshi la Yemen amesema kwamba vitengo vya makombora vya nchi hiyo vimeendesha angalau operesheni 13 dhidi ya ngome za utawala wa Kizayuni wa Israel katika siku 10 zilizopita. Operesheni hizo zinatekelezwa kulipiza kisasi kwa niaba ya Wapalestina katika Gaza ambao wanakabiliwa na mauaji ya kimbari vya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hamas yaonya kuhusu sera za Israel za kujitanua
Dec 30, 2024 04:21Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imeonya kuhusu sera ya kujitanua ya utawala haramu wa Israel nchini Syria kufuatia kuanguka kwa Rais wa zamani wa nchi hiyo, Bashar al-Assad.
-
Ripoti: Watawala wa kigaidi Syria wanafanya maangamizi ya kizazi katika mji wa Kikristo
Dec 29, 2024 23:43Shirika moja la kutetea haki za binadamu linasema Wakristo wametishwa na kundi la wanamgambo wa Hay'at Tahrir al-Sham (HTS) kuuhama mji wa Maaloula, kusini magharibi mwa Syria, katika kile kinachotajwa kuwa ni kitendo cha maangamizi ya kizazi.
-
Vikosi vya Yemen vyaangusha ndege ya kivita isiyo na rubani ya Marekani MQ-9 Reaper
Dec 29, 2024 23:38Vikosi vya Jeshi la Yemen vimetangaza kuangusha ndege ya kivita isiyo na rubani ya Marekani, aina ya MQ-9 Reaper, katika anga ya mkoa wa Al-Bayda.
-
Mtoto mchanga wa tano afariki dunia Ghaza kutokana na baridi kali na kukosekana kwa vifaa
Dec 29, 2024 09:32Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ametoa indhari kuhusu vifo vya watoto Wapalestina vinavyoongezeka kutokana na baridi kali na kukosekana kwa vifaa vya kutosha.
-
Ahadi ya Al-Joulani ya kushirikisha Wasyria wote katika uendeshaji nchi imethibiti kuwa ni uongo
Dec 29, 2024 07:32Kwa kuanza kwa wimbi la timuatimua ya maafisa wa jamii ya Maalawi katika wizara za serikali ya Syria, imethibiti kuwa ahadi alizokuwa ametoa Abu Muhammad Al-Jolani za kutotengwa tabaka lolote la jamii ya Wasyria katika uendeshaji nchi ni za uongo.
-
Baada ya Israel kuichoma moto hospitali kuu ya kaskazini ya Ghaza, yamkamata mkurugenzi na wafanyakazi wake
Dec 28, 2024 10:42Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa askari wa jeshi la utawala w Kizayuni wa Israel wamemkamata Hussam Abu Safiya, Mkurugenzi wa Hospitali ya Kamal Adwan kaskazini mwa Ghaza, na wafanyakazi wengine mapema leo, siku moja baada ya askari wa jeshi hilo kuichoma moto hospitali hiyo, ambayo ndicho kituo kikuu pekee cha afya katika eneo hilo.
-
Serikali ya Al-Joulani yatoa agizo la siri: Picha zozote za mauaji na uporaji zisisambazwe
Dec 28, 2024 09:19Kufuatia kusambazwa picha na video za mauaji na uporaji unaofanywa na wanachama wa Tahrir al-Sham nchini Syria, utawala mpya wa Al-Joulani umetoa agizo la siri la kupiga marufuku usambazaji wa picha na video hizo.
-
Ripota Maalumu wa UN afichua nafasi ya Ujerumani na Marekani katika mauaji ya kimbari ya Israel huko Gaza
Dec 28, 2024 04:01Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu na Kupambana na Ugaidi amesema: Marekani na Ujerumani zinadhamini asilimia 99 ya silaha za utawala wa Kizayuni wa Israel na inawezekana kuchukuliwa hatua za kisheria dhidi ya nchi hizo.
-
Mamilioni ya Wayemeni walaani jinai za Wazayuni dhidi ya taasisi za kiraia
Dec 27, 2024 23:37Mamilioni ya wananchi wa Yemen walimiminika mabarabarani jana Ijumaa huko Sana'a na mikoa mingine, kulaani hujuma na jinai za Wazayuni wanaoshambulia maeneo na taasisi za kiraia katika mji mkuu, Sana'a na mkoani Hudaydah.