-
Israel yakiri: Tulisababisha uharibifu mdogo kwa Iran kuliko ilivyodhaniwa hapo awali
Dec 12, 2025 23:03Israel imekiri kuwa ilisababisha uharibifu wa kiwango kidogo kwa Iran wakati wa vita vya siku 12 mwezi Juni mwaka huu kuliko ilivyofikiriwa awali.
-
Ripoti: US inaishinikiza Israel iuondoe mlima wa kifusi uliozagaa Ghaza baada ya miaka 2 ya vita
Dec 12, 2025 06:40Marekani imeitaka Israel ibebe jukumu la kuondoa vifusi vikubwa vilivyotapakaa kwenye kila pembe ya Ukanda wa Ghaza baada ya zaidi ya miaka miwili ya vita vya kinyama na mauaji ya kimbari iliyofanya dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo, pamoja na uharibifu mkubwa uliosababishwa na mashambulizi yake ya anga na matingatinga ya kivita. Hayo yameelezwa na toleo la Alkhamisi la gazeti la kizayuni la Yedioth Ahronoth.
-
Umoja wa Mataifa: Hali ya kibinadamu Gaza ni mbaya
Dec 11, 2025 23:10Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu kuongezeka kwa janga la kibinadamu katika Ukanda wa Gaza kutokana na mvua na baridi kali huko Palestina.
-
OIC: Ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni Ukingo wa Magharibi ni ukiukaji wa sheria za kimataifa
Dec 11, 2025 23:09Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imelaani mpango mpya wa Wazayuni wa kujenga nyumba 764 katika Ukingo wa Magharibi, ikiitaja hatua hiyo kuwa ni ukiukaji wazi wa sheria za kimataifa na azimio za Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, hasa Azimio nambari 2334.
-
Hamas: Israel inakiuka majukumu ya awamu ya 1 ya makubaliano ya kusitisha mapigano
Dec 11, 2025 08:44Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeilaani vikali Israel kwa kutotimiza wajibu wake katika makubaliano ya kusitisha mapigano huko Gaza, wakati harakati hiyo ya Palestina imetekeleza majukumu yake yote kwa mujibu wa awamu ya kwanza ya makubaliano hayo.
-
Tangu ulipotangazwa usitishaji vita Ghaza, Israel imewaua shahidi Wapalestina wasiopugua 386
Dec 11, 2025 03:42Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Habari ya Ukanda wa Ghaza ametangaza kuwa jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel halijaheshimu wala kufungamana na makubaliano ya kusitisha mapigano na itifaki ya masuala ya kibinadamu iliyoainishwa kwenye makubaliano hayo.
-
Ansarullah: Wazayuni wawafanyia ukatili hata wanawake wajawazito
Dec 11, 2025 00:06Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen, ametoa hotuba kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake na kugusia jinsi utawala wa Kizayuni wa Israel unavyoua kikatili maelfu ya wanawake Waislamu nchini Palestina wakiwemo wanawake wajawazito, wazee na watoto na kusema kuwa, Wazayuni hawawaonei huruma hata wanawake wajawazito na vitoto vichanga vilivyomo tumboni.
-
Shida na umasikini; urithi ambao utawala wa kizayuni umewaachia watu wake kutokana na vita vya Ghaza
Dec 10, 2025 04:24Matokeo ya uchunguzi uliofanywa na shirika moja la Kizayuni la utoaji huduma na misaada ya kibinadamu yanaonyesha kuwa, vita vya Ghaza vimewatumbukiza Wazayuni wengi zaidi kwenye lindi la umasikini; na zaidi ya robo ya familia, sasa zinakabiliwa na uhaba wa chakula.
-
Msemaji wa UNRWA: Kinachoendelea Gaza hakijawahi kushuhudiwa tangu wakati wa Vita vya Pili vya Dunia
Dec 10, 2025 02:47Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) amesema kwamba "kinachoendelea huko Gaza hakijawahi kushuhudiwa tangu wakati wa Vita vya Pili vya Dunia."
-
UNIFIL yapinga madai ya Israel kuhusu silaha za Hizbullah
Dec 09, 2025 23:12Kamanda wa Kikosi cha Mpito cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon (UNIFIL) amesema kuwa ujumbe wa kulinda amani wa kimataifa haujapata ushahidi wowote kuhusu Harakati ya Hizbullah kujenga upya uwezo wake wa kijeshi, akikanusha madai ya Israel yaliyotumika kama kisingizio cha kushambulia kusini mwa Lebanon.