-
Kampuni ya silaha ya Israel ya Elbit imeingiza mapato makubwa wakati wa mauaji ya kimbari ya Gaza
Nov 19, 2025 09:00Kampuni ya Israel inayoongoza kwa utengenezaji wa silaha, Elbit Systems, imetangaza ongezeko kubwa la faida iliyopatikana katika muda wa robo mwaka kufuatia miezi kadhaa ya ushiriki wa kampuni hiyo katika mauaji ya halaiki ya Israel huko Gaza kupitia utoaji silaha, zana za kijeshi na mifumo ya ufuatiliaji, huku ikipata mikataba mipya barani Ulaya.
-
Watu 15 wauawa katika hujuma ya anga ya Israel katika kambi ya wakimbizi wa Kipalestina huko Lebanon
Nov 19, 2025 03:28Utawala wa Israel umefanya mashambulizi ya anga na kuuwa watu wasiopungua 15 kwenye kambi kubwa zaidi ya wakimbizi wa Kipalestina kusini mwa Lebanon.
-
'Siku ya fedheha’: Afisa wa zamani wa haki za binadamu wa UN akosoa azimio la UNSC kuhusu Gaza
Nov 19, 2025 03:26Afisa wa ngazi ya juu wa zamani wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amelaani hatua ya Baraza la Usalama la umoja huo ya kupitishaa azimio linalounga mkono mpango wa Marekani wa kuanzisha kikosi cha kimataifa cha kurejesha utulivu katika Ukanda wa Gaza uliozingirwa, akiitaja kura hiyo kuwa ni "siku ya fedheha" kwa chombo hicho cha dunia.
-
Umoja wa Mataifa: Wayemen milioni 17 wanakabiliwa na njaa kali
Nov 18, 2025 07:19Umoja wa Mataifa umetangaza katika ripoti yake ya hivi punde kwamba raia milioni 17 wa Yemen wanakabiliwa na njaa kali, na idadi hii inatarajiwa kuongezeka.
-
Ukata na umaskini wa Wazayuni umeongezeka kwa theluthi nzima baada ya Oktoba 7
Nov 17, 2025 22:53Mfumuko wa bei na gharama ya maisha zinazidi kupanda huko Israel. Huku hali ikiwa hivyo ripoti rasmi ya Taasisi ya Bima ya Israel inaoneesha kwamba umaskini umeongezeka kwa zaidi ya theluthi moja kwa wakazi wa utawala huo baada ya Operesheni ya Kimbunga cha Al Aqsa ya Oktoba 7, 2023.
-
Kwa nini Hamas na makundi ya muqawama ya Palestina yanapinga azimio lililopendekezwa na Marekani?
Nov 17, 2025 07:22Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetangaza katika taarifa yake kwamba makundi na harakati za Palestina zimewasilisha waraka kuhusu rasimu ya azimio la Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kusisitiza kuwa wamepinga vikali azimio hilo lililopendekezwa na Marekani kupitia waraka huo.
-
Mchambuzi: Utawala wa sasa wa Syria utaifanya nchi igawanyike vipande vipande
Nov 17, 2025 07:19Mtafiti wa mahusiano ya kimataifa Yasser Al-Khatib amesema, hali ya mambo nchini Syria ni ngumu na tata mno kutokana na udhaifu wa watawala wake wa sasa, ambao unawasukuma watawala hao kutafuta msaada kutoka nje ya nchi, huku Wasyria wakighariki kwenye dimbwi la mgawanyiko wa nchi unaosababishwa na maslahi yanayokinzana ya nchi zinazoingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo.
-
Makundi ya Wapalestina: Hatutaki uwepo wa majeshi ya kigeni Ukanda wa Gaza
Nov 16, 2025 23:36Makundi na harakati za Palestina zimetangaza kuwa zinapinga uwepo wowote wa kijeshi wa kigeni au kambi za kimataifa ndani ya Ukanda wa Gaza, zikisisitiza kwamba suala hilo linawakilisha ukiukwaji wa moja kwa moja mamlaka ya kujitawala ya Wapalestina.
-
Safari inayotia shaka ya ndege kutoka Ghaza, ni mwanzo wa awamu mpya ya kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina?
Nov 16, 2025 22:53Zaidi ya Wapalestina 150 wakazi wa Ukanda wa Ghaza wamehamishwa kwa ndege kutoka eneo hilo la Palestina na kupelekwa Afrika Kusini kwa namna inayotia shaka, huku mamlaka za Afrika Kusini zikieleza kwamba hazikuwa zikijua chochote na kwamba uchunguzi juu ya suala hilo ungali unaendelea.
-
Rais wa Venezuela: Uadilifu ni sharti la kupatikana amani ya kweli Gaza
Nov 16, 2025 03:38Rais wa Venezuela amesisitiza uungaji mkono kamili kwa haki za watu wa Palestina na haja ya kutekelezwa haki dhidi ya jinai na vitendo vya mauaji ya kimbari.