Asia Magharibi
  • Kuhani wa Kiyahudi asema: Netanyahu ni kafiri

    Kuhani wa Kiyahudi asema: Netanyahu ni kafiri

    Nov 28, 2023 09:47

    Kuhani mmoja wa Kiyahudi ameeleza bayana kuwa waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu ni kafiri na akasisitiza kwamba kwa mujibu wa Taurati, ni haramu kuikalia kwa mabavu ardhi ya Palestina.

  • Makubaliano ya kusitisha vita  Gaza yarefushwa kwa siku 2 zaidi

    Makubaliano ya kusitisha vita Gaza yarefushwa kwa siku 2 zaidi

    Nov 28, 2023 03:42

    Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Qatar na Harakati ya Hamas zimetangaza kuwa, makubaliano ya usitishaji vita huko Gaza yameongezwa muda kwa siku mbili zaidi, kwa msingi wa masharti yale yale ya awali.

  • Jinai za kutisha za Wazayuni; waiba mpaka viungo vya miili ya wananchi wa Gaza

    Jinai za kutisha za Wazayuni; waiba mpaka viungo vya miili ya wananchi wa Gaza

    Nov 27, 2023 23:57

    Dunia imeshuhudia jinai za kuogofya mno zisizoelezeka kwa maneno, baada ya utawala wa Kizayuni wa Israel kulazimika kusimamisha vita huko Gaza bila ya kufanikisha lengo lake hata moja. Jinai ni kubwa kiasi kwamba Wazayuni wameiba miili ya watu, wameiba binadamu bali wameiba mpaka viungo vya miili ya Wapalestina waliowaua shahidi kwenye jinai yao hiyo ya kutisha.

  • Al Jazeera: Vita vya Gaza vinaweza kuwa mwanzo wa kuporomoka, lakini si kwa Wapalestina

    Al Jazeera: Vita vya Gaza vinaweza kuwa mwanzo wa kuporomoka, lakini si kwa Wapalestina

    Nov 27, 2023 23:02

    Mchambuzi mmoja maarufu wa televisheni ya Al Jazeera ya Qatar amesema kuwa, kama tunataka kuvichambua vita vya Gaza kwa kuzingatia matukio ya hivi karibuni, inatosha kwetu kuangalia siku nne kabla ya kufanyika operesheni ya #Kimbunga_cha_al-Aqsa na kabla ya HAMAS kushambulia maeneo ya kusini mwa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni.

  • Jeshi la Yemen laivurumishia makombora manowari ya US

    Jeshi la Yemen laivurumishia makombora manowari ya US

    Nov 27, 2023 07:16

    Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani katika eneo la Asia Magharibi (CENTCOM) limetangaza habari ya vikosi vya Jeshi la Yemen kuvurumisha makombora mawili ya balestiki na kulenga meli ya kivita ya Marekani ya 'USS Mason' katika Ghuba ya Aden.

  • Jihad Islami: Israel imeshindwa kuusambaratisha muqawama

    Jihad Islami: Israel imeshindwa kuusambaratisha muqawama

    Nov 27, 2023 07:14

    Mjumbe wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina mjini Tehran amesema utawala wa Kizayuni wa Israel haujafikia hata moja ya malengo yake ya kuanzisha mashambulizi ya kinyama dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza, hasa azma ya utawala huo ya kuusambaratisha mrengo wa muqawama.

  • Vita vya Gaza na kushadidi matatizo ya kiuchumi ya Israel

    Vita vya Gaza na kushadidi matatizo ya kiuchumi ya Israel

    Nov 27, 2023 04:09

    Vita vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ukanda wa Gaza vilisitishwa kwa muda baada ya takriban siku 50, katika hali ambayo, Tel Aviv imepata hasara kubwa za kiuchumi.

  • Sisitizo la UNICEF la kufikiwa usitishaji vita wa kudumu Gaza

    Sisitizo la UNICEF la kufikiwa usitishaji vita wa kudumu Gaza

    Nov 27, 2023 03:45

    James Elder, Msemaji wa Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) sambamba na kusisitiza kufikiwa usitishaji vita wa kudumu huko Gaza, amesema kuwa kitendo cha kushambuliwa kwa mabomu watoto huko Gaza hakipaswi kurudiwa tena.

  • Harakati ya Fat'h ya Iraq: Vita dhidi ya Wazayuni ndio kwanza vimeanza

    Harakati ya Fat'h ya Iraq: Vita dhidi ya Wazayuni ndio kwanza vimeanza

    Nov 26, 2023 08:33

    Mjumbe wa Muungano wa al Fat'h wa Iraq ameashiria jinsi makundi ya muqawama ya nchi hiyo yanavyoyaunga mkono makundi ya muqawama ya Palestina katika vita vya Ghaza na kusema kuwa, makundi hayo yataendelea kushambulia vituo vya wanajeshi vamizi wa Marekani nchini Iraq.