-
Msalaba Mwekundu: Viwango vyote vya kisheria na kimaadili vimekiukwa huko Gaza
Jul 26, 2025 23:06Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu amezungumzia hali mbaya ya inayoshuhudiwa sasa katika Ukanda wa Gaza kutokana na mashambulizi ya jeshi la Israel na mzingiro mkubwa wa eneo hilo na kusisitiza kuwa, viwango vyote vya kisheria na kimaadili vimekiukwa katika Ukanda wa Gaza.
-
Hamas yaijibu Marekani kuhusu usitishaji mapigano, yamtaja Netanyahu kuwa ndiye kizuizi cha amani
Jul 26, 2025 23:05Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imewashutumu maafisa wa serikali ya Marekani kwa kupotosha umma kuhusu msimamo ya harakati hiyo katika mazungumzo ya kusitisha mapigano, na kulitaja baraza la mawaziri la Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu kuwa ndio kikwazo kikuu cha kufikiwa usitishaji mapigano.
-
Kwa nini umoja wa nchi za Kiislamu ni jambo la dharura kwa ajili ya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa Gaza?
Jul 26, 2025 22:56Sayyid Abbas Araqchiو Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amelaani vikali jinai za utawala wa Kizayuni Israel katika Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa, kuna haja ya kuchukuliwa hatua haraka na nchi za Kiislamu kufanya uratibu ili kusitisha mauaji ya kimbari na kuzuia maafa ya binadamu yanayoendelea huko Gaza.
-
Haaretz: Israel iliua watoto 1,000 wa Kipalestina mwezi uliopita
Jul 26, 2025 08:06Gazeti la Kizayuni la "Haaretz" limekiri Jumamosi ya leo kwamba, jeshi la utawala huo liliua watoto 1,000 katika mashambulizi yake katika Ukanda wa Gaza mwezi uliopita pekee.
-
Ayatullah Sistani: Mataifa ya Kiarabu na Kiislamu yachukue hatua kukabiliana na njaa kali Gaza
Jul 26, 2025 04:28Kiongozi mkuu Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Iraq, Ayatullah Sayyid Ali al-Sistani, ameelezea masikitiko yake makubwa kuhusu hali ya kibinadamu inayoendelea kuzorota katika Ukanda wa Gaza, hususan baa la njaa linalozidi kushika kasi, na kutoa wito kwa mataifa ya Kiarabu na Kiislamu kuchukua hatua za haraka kukomesha janga hili la kusikitisha.
-
Gideon Levy: Picha za njaa huko Gaza zinakumbusha mauaji ya Holocaust na kambi za mateso
Jul 25, 2025 22:58Mwandishi wa Israel, Gideon Levy amesema kuwa taswira na picha za njaa huko Gaza, ambazo zinafichwa na vyombo vya habari vya ndani vya Israel, zinakumbusha watu walionusurika katika kambi za mateso na mauaji ya Holocaust, akisisitiza kwamba kugeuza njaa kuwa silaha halali ya vita ni hatua ya kishetani zaidi ya vita vya sasa vya Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Njaa yashadidi Ukanda wa Gaza huku Israel ikiendelea kuzuia misaada
Jul 25, 2025 07:25Ofisi ya Habari ya Serikali katika Ukanda wa Gaza imezitaka nchi zote duniani kuvunja mara moja mzingiro dhidi ya Gaza, kufungua mipaka kwa njia ya kudumu, na kuingiza misaada ya dharura , hasa unga na maziwa ya watoto wachanga, kwa ajili ya watu zaidi ya milioni 2.4 walioko chini ya mzingiro mkali ambao unatekelezwa na utawala katili wa Israel.
-
Yemen yasisitiza msimamo mmoja wa Kiislamu na Kiarabu kuokoa maisha ya watu wa Gaza
Jul 24, 2025 23:13Mahdi Al-Mashat, Mkuu wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen ametoa wito kwa mataifa na serikali za nchi za Kiislamu na Kiarabu kuchukua msimamo na hatua madhubuti na za haraka ili kukabiliana na tishio kubwa la utawala wa kizayuni na kuokoa maisha ya wakazi wa Ukanda wa Gaza.
-
Oxfam yaonya kuhusu janga la binadamu Gaza
Jul 24, 2025 23:02Shirika la kimataifa la Oxfam limeonya kuwa, maafa ya binadamu katika Ukanda wa Gaza yamefikia kiwango kisicho na kifani na njaa imeenea katika eneo zima.
-
Haaretz: Gaza imeharibiwa zaidi kuliko Hiroshima
Jul 24, 2025 08:38Katika ripoti ya kushtua iliyotegemea simulizi, picha za satelaiti na takwimu za Umoja wa Mataifa, gazeti la Israel limetangaza kuwa Gaza imeharibiwa zaidi kuliko miji ya Hiroshima na Nagasaki baada ya mashambulizi ya mabomu ya atomiki ya Marekani dhidi ya Japan.