Israel inapanga njama ya kuwafukuza Wapalestina milioni moja Gaza
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i129786-israel_inapanga_njama_ya_kuwafukuza_wapalestina_milioni_moja_gaza
Utawala wa Israel umeanzisha “Kitengo cha Kuhamisha Watu” ili kupanga njama kwa makin kwa lengo la kuwafukuza Wapalestina kutoka Jiji la Gaza kupitia kampeni ya mabango, ujumbe mfupi wa simu, na mizinga, kulingana na vyombo vya habari vya utawala huo ghasibu.
(last modified 2025-08-20T23:33:55+00:00 )
Aug 20, 2025 23:33 UTC
  • Israel inapanga njama ya kuwafukuza Wapalestina milioni moja Gaza

Utawala wa Israel umeanzisha “Kitengo cha Kuhamisha Watu” ili kupanga njama kwa makin kwa lengo la kuwafukuza Wapalestina kutoka Jiji la Gaza kupitia kampeni ya mabango, ujumbe mfupi wa simu, na mizinga, kulingana na vyombo vya habari vya utawala huo ghasibu.

Maelezo yaliyosambazwa na gazeti la Israel Hayom yanaonyesha kuwa utawala wa Kizayuni uko karibu kuwatimua kwa nguvu takriban Wapalestina milioni moja kutoka eneo kubwa zaidi la mji wa Ukanda wa Gaza, wakiwa wanahamishwa kusini kuelekea Korido ya Netzarim.

Hii ni hatua kali zaidi hadi sasa katika mauaji ya kimbari ya utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina ambayo yalianza Oktoba 2023 na yanaendelea hadi sasa katika Ukanda wa Gaza

Operesheni hii kali ya uhamisho inasimamiwa na Kitengo cha Kuhamisha Watu cha Kamandi Kusini, ambacho uwepo wake umefichuliwa kwa mara ya kwanza.

Waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni, Israel Katz, alitangaza siku ya Jumanne kwamba alikubali mipango mipya ya operesheni pamoja na Mkuu wa Jeshi, Eyal Zamir, na wakuu wa mashirika ya kijasusi.

Mkakati huu unataka brigedi za kawaida kuzunguka jiji, ikilazimisha takriban wakazi milioni moja kuondoka.

Kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa, kabla ya mauaji ya kimbari, takriban 82% ya wakazi wa Gaza wanaishi katika maeneo ambayo utawala huo ulitaja kama “eneo la uhamisho.”

Kutoa msaada kwa mamilioni haya ya watu waliyoachwa ni sehemu muhimu ya kanuni ya uhamisho wa watu.

“Ili kuwashawishi wahame, lazima utumie si fimbo tu bali pia karoti,” alisema chanzo cha kijeshi kilichoacha kazi. Wizara ya Afya ya Gaza imeripoti kuwa takriban Wapalestina 1,924 wameuawa na zaidi ya 14,000 wamejeruhiwa wakati wakitafuta msaada katika vituo vya Kimarekani  GHF tangu Mei 27.

Wengi wao wamepigwa kwa makusudi na vikosi vya utawala haramu wa Israel  au “makandarasi wa usalama” wa Marekani waliokodiwa na GHF.