-
Mkuu wa White House akiri: Lengo hasa la kuzishambulia boti ni kumpindua Maduro
Dec 17, 2025 06:37Mkuu wa wafanyakazi wa Ikulu ya Marekani White House Susie Wiles ametamka kuwa, mashambulizi ya jeshi la Marekani dhidi ya boti zinazodaiwa kuwa ni za madawa ya kulevya yanayofanywa katika eneo la Amerika Kusini yanalenga hatimaye kumpindua Rais wa Venezuela Nicolas Maduro.
-
Lavrov: Iran haikuwahi kukanyaga makubaliano ya JCPOA
Dec 16, 2025 11:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesisitiza kwamba, Iran haijawahi kwenda kinyume na ahadi zake ndani ya makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, akisema kwamba Marekani ndiyo iliyoyachana na kuyatupa makubaliano hayo kwenye debe la taka.
-
Hungary: Mpango wa EU wa kuiba mali za Russia ni 'tangazo la vita'
Dec 16, 2025 06:30Waziri Mkuu wa Hungary, Viktor Orban ametahadharisha kuwa, hatua yoyote ya Umoja wa Ulaya ya kutwaa milki na fedha za Russia zilizozuiliwa bila idhini ya Budapest ni kukiuka sheria za Ulaya na itakuwa sawa na "tangazo la vita."
-
ICC yatupilia mbali rufaa ya Israel ya kuomba waranti wa kumkamata Netanyahu ubatilishwe
Dec 16, 2025 03:27Kitengo cha rufani cha Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kimetupilia mbali hoja za utawala wa kizayuni wa Israel za kupinga uhalali wa uchunguzi wa mahakama hiyo kuhusu jinai zilizofanywa Ukanda wa Ghaza kufuatia vita vya kinyama na vya mauaji ya kimbari ambavyo utawala huo haramu ulivianzisha Oktoba 7, 2023 dhidi ya Wapalestina wa ukanda huo uliowekewa mzingiro.
-
Makaburi ya Waislamu nchini Australia yanajisiwa baada ya ufyatuaji risasi huko Sydney
Dec 16, 2025 02:51Makaburi ya Waislamu nchini Australia yamenajisiwa kwa vichwa vya nguruwe vilivyokatwa kufuatia ufyatuaji risasi uliolenga hafla ya Kiyahudi mjini Sydney nchini humo.
-
Ana kazi lakini ana njaa; kwa nini wazazi wa Uingereza wanatafuta misaada ya chakula?
Dec 16, 2025 02:50Kadiri uchumi wa Uingereza unavyozidi kulegea na kuporomoka, takribani robo ya wazazi wenye ajira nao wanalazimika kutafuta msaada wa chakula cha bure kutoka mashirika ya hisani.
-
Shujaa Muislamu aliyejitolea kupambana na gaidi kuwaokoa Mayahudi Australia + VIDEO
Dec 15, 2025 06:56Shujaa Muislamu ambaye video yake imeenea mno mitandaoni ikimuonesha akijitolea kwenda katikati ya ufyatuaji risasi na kujikubalisha kupigwa risasi lakini aweze kupambana na kumnyang'anya silaha gaidi aliyekuwa anawafyatulia risasi Mayahudi huko Sydney, anaendelea kupongezwa kote duniani na kuambiwa kwamba ni shujaa ambaye kujitolea kwake kumeweza kuoko maisha ya watu wengi.
-
Vifaa vya tiiba vya Iran sasa kuzalishwa nchini Venezuela
Dec 15, 2025 03:06Wizara ya Sayansi na Teknolojia ya Venezuela imetangaza kusainiwa makubaliano ya kimkakati na kampuni ya Iran kwa ajili ya kuzindua njia nne za uzalishaji wa vifaa muhimu vya matibabu nchini Venezuela.
-
Waziri Mkuu wa Uhispania: Kampeni ya Marekani katika maji ya Karibi ni ukiukaji wa sheria za kimataifa
Dec 15, 2025 02:18Waziri Mkuu wa Uhispania amesema kwamba kampeni ya Marekani katika maji ya Karibi ni ukiukaji wa sheria za kimataifa.
-
Ripoti yatahadharisha: Mamilioni ya Waingereza Waislamu wako hatarini kuvuliwa uraia
Dec 14, 2025 09:45Mamlaka ya kunyang'anya uraia yanayoelezewa kuwa ni ya "kupindukia mpaka na yenye usiri" iliyopewa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Uingereza yanawaweka mamilioni ya Waislamu raia wa nchi hiyo katika hatari ya kuvuliwa uraia wao.