-
Mbunge wa Kongresi: Marekani iliwezesha mauaji ya halaiki Ukanda wa Gaza
Feb 15, 2026 02:49Mbunge wa chama cha Democratic katika Kongresi ya Marekani amesema kuwa, msaada wa kijeshi wa Marekani kwa Israel "usio na masharti" uliwezesha mauaji ya halaiki huko Gaza," akibainisha kuwa maelfu ya wanawake na watoto waliuawa katika matukio ambayo "yangeweza kuepukwa kabisa."
-
Ubepari na ukosefu wa utulivu wa kijamii
Feb 15, 2026 02:48Uhusiano kati ya ubepari na ukosefu wa utulivu wa kijamii ni mojawapo ya mada muhimu katika uwanja wa sayansi za jamii.
-
Je dunia kweli imekubali uongozi wa Marekani?
Feb 14, 2026 10:42Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa amedai dunia imekaribisha nafasi ya uongozi wa Marekani.
-
Reuters: Duru ya pili ya mazungumzo ya Iran na Marekani itafanyika Jumanne, Geneva
Feb 14, 2026 09:56Shirika la habari la Reuters limenukuu chanzo kimoja na kutangaza kuwa ujumbe wa Marekani unaojumuisha Steve Witkoff na Jared Kushner, utakutana na maafisa wa Iran mjini Geneva, Uswisi siku ya Jumanne wiki hii.
-
BNP kutangaza serikali mpya ya Bangladesh Jumapili, kuitaka India imrudishe Hasina
Feb 14, 2026 09:55Chama cha Taifa cha Bangladesh (BNP) kimetangaza kuwa kitaunda serikali mpya ifikapo kesho Jumapili, baada ya kupata ushindi wa kishindo wa theluthi mbili ya viti vya Bunge katika uchaguzi wa kwanza kufanyika nchini humo tangu mapinduzi ya Julai 2024 yaliyoing'oa madarakani serikali ya aliyekuwa waziri mkuu Sheikh Hasina.
-
Guardiola awatetea wahamiaji akijibu matamshi ya kibaguzi ya mmiliki wa Manchester United
Feb 14, 2026 05:57Meneja wa timu ya Manchester City, Pep Guardiola, amejibu maoni ya mmiliki wa Manchester United, Sir Jim Ratcliffe kuhusu uhamiaji, akisema kwamba kuna haja ya "kukumbatia tamaduni zingine ili kuifanya jamii iwe bora."
-
Palestine Action yapata ushindi muhimu wa kisheria dhidi ya ukandamizaji wa serikali ya Uingereza
Feb 14, 2026 04:31Mahakama Kuu ya Uingereza imetoa pigo kubwa la kisheria kwa jitihada za serikali ya nchi hiyo za kunyamazisha uungaji mkono wa wazi watu kwa Palestina, baada ya kutoa uamuzi kwamba hatua ya Wizara Mambo ya Ndani wa 2025 ya kupiga marufuku kundi la linalounga mkono Palestina la Palestine Action kwa madai kwamba ni shirika la kigaidi, ulikuwa kinyume cha sheria.
-
Rais wa mpito wa Venezuela: Maduro bado ndiye rais halali
Feb 14, 2026 02:22Rais wa mpito wa Venezuela, Delcy Rodríguez, amesema kwamba anaongoza nchi hiyo kwa kuzingatia vifungu vya Katiba, akikanusha madai kwamba Marekani inaendesha Venezuela, huku akisisitiza kwamba Nicolas Maduro anasalia kuwa rais halali wa jamhuri hiyo.
-
Maelfu waandamana Melbourne kulaani ziara ya rais wa 'Israel' nchini Australia
Feb 13, 2026 10:36Maelfu ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina walipaza sauti na kufunga barabara kadhaa mjini Melbourne, chini ya ulinzi mkali wa mamia ya polisi, wakati Rais wa utawala haramu wa Israel Isaac Herzog akihitimisha ziara yake iliyokumbwa na utata mkubwa nchini Australia.
-
Kremlin: Russia haina mpango wa kushiriki mkutano wa 'Bodi ya Amani'
Feb 13, 2026 02:03Ikulu ya Russia ya Kremlin imethibitisha kwamba maafisa wa nchi hiyo hawana mpango wa kuhudhuria mkutano wa kwanza wa Bodi ya Amani (ya Gaza) uliopangwa kufanyika Februari 19 huko Washington.