-
Mshindi wa Tuzo ya Nobel ampongeza Netanyahu kwa vita dhidi ya Gaza
Oct 19, 2025 03:02María Corina Machado, kiongozi wa upinzani wa Venezuela na Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel ametoa shukrani zake za dhati kwa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu kwa maamuzi yake 'magumu' wakati wa vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza.
-
Katibu Mkuu wa UN: Umoja wa Mataifa uko hatarini 'kufilisika' ikiwa nchi wanachama hazitalipa michango yao
Oct 18, 2025 23:11Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametahadharisha kuwa umoja huo ulioanzishwa miaka 80 iliyopita unaweza kufilisika ikiwa nchi wanachama hazitolipa michango yao kwa ukamilifu.
-
NAM yaonya kuhusu chokochoko za Washington; Je, Marekani iko mbioni kushambulia Venezuela?
Oct 18, 2025 23:10Wakati ripoti zikionyesha kuwa Pentagon inatayarisha machaguo ya kijeshi dhidi ya Venezuela, Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM), ambayo inaundwa na zaidi ya nchi 120, imeonya kwamba shambulio lolote dhidi ya nchi hiyo ya Amerika Kusini litakuwa ukiukaji wa wazi wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa.
-
Ripoti: Ufaransa inakiuka pakubwa haki za watoto wahamiaji
Oct 18, 2025 09:26Shirika moja la Umoja wa Mataifa limesema Ufaransa "imekiuka pakubwa na kwa utaratibu" haki za watoto wahamiaji, na kuwaacha wengi wao wakinyimwa huduma za afya na kukosa makazi.
-
Uhispania: Vikwazo vya silaha dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel vinaendelea
Oct 18, 2025 09:08Waziri Mkuu wa Uhispania amesema kuwa, licha ya makubaliano ya kusitisha mapigano Gaza, serikali ya Madrid itadumisha vikwazo vyake vya silaha dhidi ya Israel.
-
Chuo Kikuu cha Oxford chanufaika na makampuni yanayojishughulisha na uhalifu wa Israel
Oct 18, 2025 04:16Chuo Kikuu cha Oxford cha nchini Uingereza, ambacho kwa muda mrefu kinajulikana kama kilele cha elimu duniani, kinachunguzwa vikali baada ya kubainika wazi kwamba kimefanya uwekezaji kwa njia isiyo ya moja kwa moja katika makampuni yasiyopungua 49 yanayojihusisha na vitendo haramu vya Israel katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Wimbi la chuki dhidi ya Israel laongezeka sambamba na kupungua uungaji mkono kwa Tel Aviv nchini Marekani
Oct 18, 2025 01:04Wimbi la chuki dhidi ya utawala haramu wa Israel limeongezeka katika maeneo mbalimbali duniani sambamba na kupungua himaya na uungaji mkono kwa utawala huo nchini Marekani.
-
Taa ya kijani ya Trump kwa Israel; Je vita vya Gaza vitaanza tena?
Oct 17, 2025 22:59Rais Donald Trump wa Marekani ameionyesha Israel taa ya kijani ili ianzishe tena vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Indhari ya Human Rights Watch Ulaya-Mediterranean dhidi ya kuendelea Israel kutumia njaa kama wenzo wa mauaji ya halaiki
Oct 17, 2025 08:55Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Euro-Mediterania limetahadharisha katika taarifa yake kwamba, hatari ya njaa bado haijaondolewa huko Gaza, na kuendelea kupunguzwa kwa makusudi misaada ya kibinadamu kunadhihirisha kuwa utawala wa Israel unaendelea kutumia sera ya njaa kama wenzo wa mauaji ya halaiki.
-
Putin amuonya Trump kuhusu kuipa Ukraine makombora ya Tomahawk
Oct 17, 2025 03:35Rais wa Russia, Vladimir Putin amemuonya Rais wa Marekani, Donald Trump katika mazungumzo yao ya simu kwamba, kuipa Ukraine makombora ya masafa marefu ya Tomahawk kutaharibu zaidi uhusiano kati ya Moscow na Washington.