-
EU yagawanyika juu ya kifurushi cha vikwazo dhidi ya Russia
Sep 21, 2025 23:14NATO imepeleka ndege tatu za kivita za Ufaransa huko Poland Mashariki kwa kile kilichotajwa kuwa ni sehemu ya kukabiliana na Russia. Wachambuzi wengi wanasema kuwa, ni vitendo kama hivyo vya jeshi la nchi za Magharibi NATO la kutanua uwepo wake karibu na Russia ndivyo vilivyozusha na kushadidisha mgogoro wa Ukraine.
-
Trump atoa vitisho dhidi ya Afghanistan endapo Taliban haitaikabidhi US kituo cha anga cha Bagram
Sep 20, 2025 23:54Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kuchukua hatua kali ambazo hakuzitaja iwapo serikali ya Taliban nchini Afghanistan itakataa kukabidhi kituo cha jeshi la anga cha Bagram, ambacho kilitelekezwa wakati majeshi ya Marekani. yalipoondoka kifedheha katika ardhi ya nchi hiyo.
-
Kupinga nchi za Magharibio azimio la kuondolewa vikwazo Iran
Sep 20, 2025 23:05Nchi za Magharibi zimezuia kupitishwa azimio katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililopendekezwa na Korea Kusini kuhusu kuongezwa muda wa kuondolewa vikwazo vya nyuklia Iran.
-
Ufaransa na nchi nyingine 9 kuitambua rasmi Palestina
Sep 20, 2025 08:18Katika hatua ya kihistoria, Ufaransa na nchi nyingine tisa zimetangaza kuwa zitalitambua rasmi taifa huru la Palestina.
-
Amnesty International: Kura ya turufu ya Marekani ni taa ya kijani kwa mauaji ya kimbari huko Gaza
Sep 20, 2025 07:52Shirika la Msamaha Duniani, Amnesty International, limekosoa vikali kura ya turufu ya Marekani dhidi ya azimio la kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza, likitaja hatua hiyo kama uungaji mkono wa moja kwa moja kwa jinai za kutisha za Israel.
-
Guterres: Ulimwengu haupaswi kutishwa na vitisho vya Israel kuhusu Palestina
Sep 20, 2025 07:48Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameonya kwamba vitisho vya Israel havipaswi kuzuia kutambuliwa rasmni kwa taifa la Palestina.
-
Brazil yaungana rasmi na Afrika Kusini katika kesi ya mauaji ya halaiki dhidi ya Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ)
Sep 20, 2025 04:07Brazil imewasilisha rasmi ombi la kujiunga katika kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini dhidi ya utawala wa Israel kuhusu vita vinavyoendelea tangu Oktoba 2023 ambavyo vinatambuliwa na wengi kuwa ni vya mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza.
-
Duru za Uturuki: Erdogan amefanya mazungumzo ya siri Istanbul na mwana wa kiume wa Trump
Sep 19, 2025 07:37Mwana mkubwa wa kiume wa Rais Donald Trump wa Marekani na ujumbe alioandamana nao wiki iliyopita walikutana na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan mjini Istanbul wiki katika ziara ambayo haikutangazwa. Hayo yameripotiwa na duru zilizodai kuwa na uelewa wa suala hilo.
-
Taliban yamjibu Trump: Tunaweza kuzungumza, lakini Marekani haitaruhusiwa kuwepo tena kijeshi Afghanistan
Sep 19, 2025 07:35Serikali ya Afghanistan inayoongozwa na Taliban imetupilia mbali wito wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kutaka jeshi la nchi hiyo lirejee Afghanista na kupatiwa tena kambi ya jeshi la anga ya Bagram.
-
Marekani yatumia kura ya veto kupinga azimio la kusitisha vita Gaza
Sep 19, 2025 00:26Marekani imetumia kura turufu kuzuia kupasishwa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linalotaka usitishwaji vita Gaza, kuwezesha ufikaji wa misaada ya kibinadamu na kuachiliwa kwa mateka.