Rwanda yataka wakimbizi wa Burundi waondoke
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i1843-rwanda_yataka_wakimbizi_wa_burundi_waondoke
Rwanda imesema ni lazima wakimbizi wa Burundi walioko kwenye nchi hiyo wahamishiwe kwenye nchi ya tatu.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Feb 24, 2016 07:09 UTC

Rwanda imesema ni lazima wakimbizi wa Burundi walioko kwenye nchi hiyo wahamishiwe kwenye nchi ya tatu.

Rwanda inasema inafanya hivyo kuepuka kuendelea kuchafuliwa jina lake kutokana na kile inachokitaja kama propaganda za serikali ya Burundi kulifanya suala la wakimbizi kama la kisiasa. Burundi imekuwa ikilaumu Rwanda kuwapa silaha na mafunzo wakimbizi wa Burundi suala ambalo Rwanda imekuwa ikilikanusha.
Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivanus Karemera anaripoti zaidi.