-
Indhari ya UN ya kutokea maafa ya kibinadamu Ukingo wa Magharibi kutokana na hujuma za Jeshi la Israel
Mar 09, 2025 06:09Kufuatia kuendelea hujuma za jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya maeneo mbalimbali ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu imetoa indhari kupitia taarifa yake kwamba uvamizi na hujuma za jeshi hilo katika eneo la kaskazini la Ukingo wa Magharibi zina madhara na maafa makubwa ya kibinadamu.
-
Mkutano wa Jeddah; licha ya kukamilisha lakini ni zaidi ya mkutano wa Cairo
Mar 08, 2025 23:05Kufanyika mkutano wa dharura wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Kiislamu huko Jeddah mara baada ya mkutano wa dharura wa mawaziri wa Mambo ya Nje na Wakuu wa Nchi za Kiarabu huko Cairo, Misri kunaonyesha ushirikiano wa pamoja wa Ulimwengu wa Kiislamu katika kukabiliana na mpango wa kuwafukuza kwa nguvu wakazi wa Ukanda wa Gaza na wa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Shutuma na bwabwaja za uwongo za Wamagharibi dhidi ya miradi ya nyuklia ya Iran
Mar 08, 2025 07:17Sayyid Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa: Miradi ya nyuklia ya Iran inayofanyika kwa malengo ya amani haiwezi kuangamizwa kwa shambulio la kijeshi. Araqchi ameeleza haya akijibu uropokaji na uwongo wa Wamagharibi dhidi ya miradi ya nyuklia ya nchi hii.
-
Trump na kukandamizwa uhuru wa kusema huko Marekani
Mar 08, 2025 00:53Gazeti la Marekani la Washington Post limeandika makala likiashiria amri za utendaji zilizotolewa na Rais wa Marekani, Donald Trump, tangu aingie madarakani na kusema: Wakosoaji wanamtuhumu kuwa anakandamiza sana uhuru wa kujieleza na kukiuka Katiba ya Marekani.
-
Kwa nini Rwanda imeitaka Uingereza iilipe fidia?
Mar 07, 2025 07:04Suala la madai ya Rwanda ya fidia ya pauni milioni 50 kutoka kwa Uingereza kwa kuacha mpango wa kuwafukuza wakimbizi haramu nchini humo sasa limekuwa kadhia tata na ngumu kati ya nchi hizo mbili.
-
Onyo la Iran kwa Troika ya Ulaya kwa kukiuka Azimio la Umoja wa Mataifa na JCPOA
Mar 06, 2025 23:01Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa na Mashirika ya Kimataifa yaliyoko mjini Vienna, ametoa indhari kwa Troika ya Ulaya kuhusiana na ukiukaji wake wa Azimio la Umoja wa Mataifa na la Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA.
-
Mpango wa Ulaya wa kujibu mapigo kwa hatua ya upande mmoja ya Trump kuhusiana na vita vya Ukraine
Mar 06, 2025 03:53Viongozi wa nchi za Ulaya wameamua kuchukua hatua zaidi za kuandaa mkakati wa kuwa na mpango huru na wa kujitegemea kiulinzi kufuatia msimamo na uamuzi wa upande mmoja uliochukuliwa na Marekani kuhusiana na vita vya Ukraine.
-
Kwa nini Iran inakaribisha upanuzi wa ushirikiano na Afghanistan?
Mar 05, 2025 22:56Majadiliano na mikutano ya maafisa wa Iran na Afghanistan yanaendelea kwa lengo la kupanua uhusiano na kutatua masuala kati ya nchi hizi mbili.
-
Mpango wa Umoja wa Nchi za Kiarabu kuhusu Palestina unapingana na matakwa ya Marekani na Utawala wa Kizayuni
Mar 05, 2025 04:43Viongozi wa nchi za Kiarabu, katika mkutano wao mjini Cairo, wamepinga mipango na njama za kishetani za Marekani na utawala wa Kizayuni kwa kukataa hatua za kulazimisha uhamishaji wa Wapalestina.
-
Mkutano wa London, maonyesho ya nguvu na uungaji mkono kwa Ukraine bila dhamana ya utekelezaji
Mar 05, 2025 00:46Siku mbili baada ya kufedheheshwa Rais Zelensky wa Ukraine katika Ikulu ya White House na suala hilo kuakisiwa pakubwa kimataifa, viongozi wa nchi 19 za Ulaya, Canada na maafisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Ulaya na muungano wa NATO wamekutana mjini London kwa ajili ya kutangaza mshikamano wao na Ukraine katika vita vyake na Russia.